CHADEMA ime-savaivu, sasa nini?

Kama ni hivyo kwa nini wali kuwa wakipinga chochote alichofanya Magufuli?
 
CCM wanatumia dola kubaki madarakani. CHADEMA wana nguvu ya wananchi yakuwaweka madarakani. Muda utaongea.
Bado sana, usijiaminishe hivyo kirahisi rahisi. Kaa Chadema halafu ujihusishe na siasa za CCM kwa muda, utakuja kutuelezea tofauti ya hivi vyama na nguvu zake kwa wananchi. Tumepita huko kwa miaka zaidi ya Ishirini.
 
Aliyepania kuua hivi vyama, kaanza mwenyewe! hatari sana.....Mungu fundi.
 
Umeeleza vizuri sana kuhusu kupeleka chama mpaka ngazi ya chini kabisa, lakini kipimo changu huwa jimbo lá Hai ambapo mzazi wangu mmoja ni mkazi.

Kunatakiwa kuimarishwe sana, labda kwa kuwa Wilaya ya Hai uongozi wote kuanzia nyumba kumi, wajumbe na Madiwani pamoja ofisi za Chadema kutumikia kama vijiwe vya CCM tunashindwa kukaa na kupima matokea ya Chadema Msingi.
 
Nakushauri jitahidi kutembelea vijijini na hasa sehemu Chadema haina wafuasi sugu halafu utakuja kuandika ulichokiona.

Wakati Chadema inatawala mkoa wa Kilimanjaro CCM walikuwepo japo wsmepungua lakini wakiwa na Mapenzi ya chama chao ya kufa mtu.
CCM ina wapenzi wa kweli Kilimanjaro nadhani kuliko maeneo mengi. Iwe Upareni, Uchagani na hata maeneo mengine. Na wanajitoa kuliko vyama vingine.
 
Kama ni hivyo kwa nini wali kuwa wakipinga chochote alichofanya Magufuli?
Kama CHADEMA wangepinga kila alichofanya Magufuli, na Magufuli akawa hafanyi aliyoyaeleza huyo uliyemjibu , Stuxnet hapa, CHADEMA inawezekana wakati huu ingekuwa haipo kabisa!
Ingekuwa imekwishafutika na wananchi kuisahau kabisa.
 
Nimetembea sana vijijini mkuu..... Wakati wa kampeni za uchaguzi nilikua mikoa ya magharibi yaani Tabora,Kigoma, na Mpanda. Aiseee CHADEMA ina hard core followers wengi tu tena maeneo ambayo sikutarajia kabisa hasa vijana ambao ndio wengi nchini na wamezaliwa enzi za vyama vingi so to them CCM means nothing.
 
CHADEMA wanaweza kuwa wamejiridhisha kuwa wamekwishafanya kazi kubwa ya kukipeleka chama kwa wananchi, hadi huko mitaani; na kama hivyo ndivyo ilivyo kweli inabidi wajitafakari sana kwa sababu bado kuna alama zinazoonyesha kwamba juhudi zao hizo bado hazijawa na mafanikio ya kutosha.

Inaeleweka, mazingira magumu sana yaliyokuwa yakiwakabili kufanya kazi zao maeneo yote nchini, lakini ni lazima wawe na muda wa ku'evaluate' matokeo ya juhudi hizo, hasa wakati huu tunapoingia kwenye hali iliyo tofauti kidogo na iliyokuwepo miaka mitano iliyopita.

Ni lazima watafute njia za kujua CHAMA chao kina hali gani huko mashinani, na kurekebisha panapohitaji kurekebishwa. Wakati ndio huu, na hawahitaji kabisa kumtangazia yeyote kuwa kazi hiyo inafanyika.

Hawawezi kuwa wanajiaminisha tu kuwa wamekwishafanya kazi za kukieneza chama bila kuwa na matokeo/majibu ya uhakika wa kazi hiyo.

Wao wanapenda sana hizi siasa za kwenye majukwaa, kazi muhimu za mtu kwa mtu huko mitaani inawawia ngumu sana kuifanya.
 
Hai ni sample ndogo sana embu fika mkoa wa songwe au kigoma na Mara.... Huko kuna followers wengi sana shida ni kwamba hakuna tu mikutano ya siasa na uhuru wa kufanya siasa za ushindani kama enzi za kikwete but trust me chama kipo hai kabisa na nadhani uliona mapokezi ya Lissu yalivyokua kanda ya ziwa na magharibi!!

Credit to Mbowe na Mzee ndesamburo kwa kuleta chadema ni msingi and kuimarisha ofisi za kanda. Kufikia 2025 chama kitakua imara zaidi kuleta mabadiliko ya kweli.
 
Naomba ni object hili

Kata nayoishi huwa kila jumatatu wanakutana kufanya evaluation ya hali ya kisiasa kuanzia level ya kata,mtaa hadi kitongoji na uongozi upo kabisa ukiwa na kamati tendaji/sekretarieti functional kabisa.

Kwenye hivyo vikao hupeana milestones za kueneza chama, kukaribisha wanachama wapya, kujijenga mashinani kupitia PR nzuri, kufanya shughuli za kijamii n.k

Sasa kama haya yanafanyika wala 50% ya kata zote Tanzania then trust me CHADEMA ipo imara na kabla ya uchaguzi wowote tayari wana kura million 2 za kuanzia irrespective mgombea ni nani!!

Nimetoa experience yangu kwa ngazi ya kata yangu so naweza conclude kuwa hatutegemei siasa za majukwaani otherwise tusingeweza toa challenge kwa CCM despite mazingira magumu ya 2020
 
Mkuu, nikupongeze kwa hali hiyo hapo ulipo.
Kama hali ndivyo hivyo kwenye 40%, acha hiyo 50% unayoitaja, CHADEMA watakuwa wapo kwenye hali nzuri sana, tena sana mkuu wangu!

Mimi siwezi kukukatalia kwenye haya unayoandika hapa, in fact ninaweza hata kujibandika cheo cha 'agent provocateur' katika hili kwa ajili ya manufaa ya chama chenu, na hata pengine kwa taifa zima.

Njia nzuri ya kujua ni wapi mlipo, ni hiyo niliyoitaja hapo juu. Tafuteni njia nzuri sana ya kupata 'feedback' juu ya uhai wa chama sehemu zote nchini. Hii ni lazima ili muweze kuweka mipango na mikakati endelevu kuzidi kukiimarisha chama.

Natambua ugumu wa kazi hiyo, hasa kuifanya bila nyenzo muhimu. Lakini nyezo iliyopo sasa hivi ni hao watu wenu waliopo huko.
 

kwa sasahv nawashauri mjikite kumsafisha lowasa aje kugombea tena 😂
 
kwa sasahv nawashauri mjikite kumsafisha lowasa aje kugombea tena 😂
Inawezekana sana kuna kitu ulichosoma kwenye hayo maandishi yangu kilichokuumiza sana hisia zako.

Unakijua mwenyewe.
 
Inawezekana sana kuna kitu ulichosoma kwenye hayo maandishi yangu kilichokuumiza sana hisia zako.

Unakijua mwenyewe.

mm sio mgeni apa, na wewe sio mgeni tunajuana vizuri, kwenye mada wa kumsafisha mbowe na ofisi yake mpo vizuri, nlisoma tu title nkajua ni takataka maana icho chama nlishakihama mda mrefu na hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza fanya siasa kwenye hio ofisini yenu ya leo 1+1=2 kesho 1+1=3, miaka nenda rudi lowasa fisadi kipindi cha uchaguzi lowasa msafi, wafunge akile hao wengine mliobaki
 
Wewe siku zote najua ni mpuuzi.
Kwa hiyo sina muda na kupoteza wewe.
 
CHADEMA.

Kwanza kabisa eleweni kuwa muda wa ku- gloat juu ya kifo cha Magufuli umeshapita!
Kwa hili naomba nisiseme zaidi.

Pili, msichukulie mawaidha mazuri kama ya huyu mleta uzi kuwa ni criticism dhidi ya chama na kuanza ku-generate hadithi nyingi za kuji-defend. Badala yake, yaangalieni maoni haya katika mwanga chanya. Mwanga wa kujenga, na myafanyie tathmini makini.

Tatu, ni kweli kwamba the late Magufuli na ma-satellite wake walikivuruga sana hiki chama kwa kubomoa misingi yake ya kiitikadi kupitia kuwanunua viongozi wake, na hata kujaribu kuwa- eliminate wengine kuiba sera, na pia kubomoa uchumi wa viongozi wake wenye ukwasi ili waache kuwekeza kwenye chama. Hizo ni figusu figusu za kawaida kwa CCM dhidi ya upinzani lakini marehemu alizipeleka kwenye level ambayo ilikuwa haijafikiwa hapo mwanzoni.

Pamoja na hayo, chama bado kilikuwa na madhaifu mengi hata kabla ya fujo za Magufuli.

Hakuna political machines zilizoenea nchi nzima.

Hakuna ma-ideologists walioweza kubuni sera za kuwatia hamasa wafuasi wenu mpaka wawe radhi kujitoa mali na uhai kwa ajili ya chama, au hata kutengeneza mikakati inayowavutia kiasi ambacho commitment yao kwa chama haitikiswi ije mvua au jua( hapa nam-excempt Slaa ambaye hata hivyo mlimpoteza kizembe, na siongelei kuhusu rabble rousers wengine).

Yapo mengi. Hapo sijaongolea tuhuma za nepotism na ukanda zinazopigiwa kelele sana na wapinzani wenu kama sehemu ya propaganda zao of course, lakini ambazo ni rahisi kuaminiwa na wananchi wasiojua kwasababu ya utetezi dhaifu.

Hivyo endeleeni kukijenga chama.

Sera ya majimbo, kwa mfano ni solid sana kwa ustawi wa nchi hii lakini msipoifafanua vizuri, CCM watakuja na hoja nyepesi kwamba mnataka kuligawa taifa, watawazomea kidogo, watawapiga ile mipasho yao na mtanywea hapo hapo.

Nyuma yenu wapo watu wengi sana wanaoamini katika demokrasia ya vyama vingi na afya inayoletwa na ushindani wa kisiasa katika nchi, ambao ndio unaosimamisha utawala wa sheria.

Lakini pia wapo wengi ambao hawaelewi faida za hii mifumo na huyumbishwa kirahisi sana na watawala waliopo madarakani kwa kutishiwa kidogo tu au kwa kulambishwa pipi na kudanganywa.

Nafurahi kuwa mme- survive!

Kwangu mimi kuuachia upinzani uwe compromised utakuwa ni usaliti.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…