Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 141,518
- 284,002
ajira ngapi zimeletwa ?wakina Mbowe kinawauma zile mali na miradi yao ambayo ilibanwa kwelikweli na nyingine mpaka kupigwa mnada hii iliwauma kwelii hapo wakaona wamefanyiwa udikteta wa hali ya juu wakasahau kuna wafuasi wao walikua wanashinda bila hata kula hukoo mikoani kwa ajili wa matumbo yao rukuku ya kila mwezi lakini walirudi kwa wafuasi wao na kupitisha tena bakuri kwa ajili ya chama kifupi walikua wanajari maslahi yao hawakujua kula na vipofu kabisaa ila kwa fimbo hii imewapiga kweli kweli sijui watakuja na sera gani tena sidhani kama wanaweza muhubiria mwananchi kuhusu demokrasia wakati tayari wameshaonja utamu wa kasi ya hayati JPM uongozi uliokua na msingi wa kazi mbele kwa Maslahi mapana ya Taifa
Bi Samia hawezi kukubali chama kifie mikononi mwake kwa hiyo suala la katiba mpya na tume huru hawezi hata kuvigusia. Sahau mkuuMbona Chadema wanakuwaga na sera nzuri kuliko vyama vingine vyote, Mfano ilani ya Uchaguzi mkuu mwaka 2015 ya CHADEMA ilikua moja ya sera zilizokua zinakitisha chama cha kijani kuondoka madarakani, hata hivyo kura hazikutosha ila uchaguzi uliofanyika hivi 2020 ulikua uchafuzi.Bi samia atuletee katiba mpya ikiwa na tume huru ya uchaguzi
Chadema inaongea Ccm inatenda, hapo ndipo tofauti inapokuja.Huko unakotaka twende tulishafika na kumaliza kazi , hii ndio sababu ya Mahera kupokea maagizo ya ccm ( Bashiru , Polepole na Magufuli ) ya kuondoa wagombea wa Chadema nchi nzima na kwingine kupeleka kura za mabegi , labda nikutoe shaka , Chadema imo mpaka ndani ya ccm na atakayejaribu kuihujumu atakiona cha mtemakuni , nimemaliza
Nyoko wenu hayupo kapewa kibano na Mungu kupitia korona anafukiwa futi 6 chini ya ardhi. Sasa uwanja wa mapambano umebadilika. Uaminifu kwenu umebakia kwa wadhaifu wachache ambao nao muda wao unayoyoma. TUTAELEWANA TU NA KUONGEA LUGHA MOJA. Sisi wenye chama cha CHADEMA hatutachoka kuwasitiri viongozi wetu kwa hali na mali na kuwakabidhi kwa Mungu.wakina Mbowe kinawauma zile mali na miradi yao ambayo ilibanwa kwelikweli na nyingine mpaka kupigwa mnada hii iliwauma kwelii hapo wakaona wamefanyiwa udikteta wa hali ya juu wakasahau kuna wafuasi wao walikua wanashinda bila hata kula hukoo mikoani kwa ajili wa matumbo yao rukuku ya kila mwezi lakini walirudi kwa wafuasi wao na kupitisha tena bakuri kwa ajili ya chama kifupi walikua wanajari maslahi yao hawakujua kula na vipofu kabisaa ila kwa fimbo hii imewapiga kweli kweli sijui watakuja na sera gani tena sidhani kama wanaweza muhubiria mwananchi kuhusu demokrasia wakati tayari wameshaonja utamu wa kasi ya hayati JPM uongozi uliokua na msingi wa kazi mbele kwa Maslahi mapana ya Taifa
mkuu, hii muda utaongea ni miaka mingapiCCM wanatumia dola kubaki madarakani. CHADEMA wana nguvu ya wananchi yakuwaweka madarakani. Muda utaongea.
Kama una watoto wanaosoma ungejua kama kuna elimu bure au kuna utopoloChadema inaongea Ccm inatenda, hapo ndipo tofauti inapokuja.
Chadema walileta habari za elimu bure ccm ikazifanyia kazi, hapo ndipo wanapowawini raia
Lini ulishakuwa na tatizo na mimi? Zaidi ya kuwa unamwaga pumba kama hizi. Chadema itasavaivu kwa kuwa na kiongozi kama Mbowe?Sina tatizo na wewe tena mkuu!
Yamekwishatimia sasa.
CCM itaendelea kutawala kwa muda mrefu sana.
ninao wawiliKama una watoto wanaosoma ungejua kama kuna elimu bure au kuna utopolo
Upinzani ungali imara,Amekufa yeye mkuu.
Uzuri wataalamu wa kuiba kura Mungu kawapangia majukumu mengine, ikiwemo kuongoza malaika.Ccm hawana jipyaKwa kutumia mtutu wa bunduki labda si kupitia uchaguzi huru na wa haki.
SawaHakuna shaka yeyote, na sidhani kwamba kuna mtu anayeweza kuhoji uwepo wa CHADEMA kama chama cha kisiasa kilicho na ushindani mkubwa hapa nchini licha ya misukosuko mingi iliyoelekezwa kwao ili kuwamaliza kabisa katika miaka mitano na zaidi sasa iliyopita.
Ni sawa kabisa kusema kwamba CHADEMA wamepitia kwenye tanuru la moto mkali, na wamepikika sawasawa kuweza kuendelea na pilkapilka zao za kisiasa na kutafuta njia ya kuliongoza taifa hili.
Sioni mbele yao, kupata hujuma tena, kama walizozipata miaka hii ya karibuni chini ya utawala wa Marehemu Magufuli. Tanzania itakuwa na bahati mbaya sana, kama patatokea hivi karibuni misukosuko iliyolitingisha taifa kama ilivyotokea wakati wa serikali ya Magufuli.
Watu wanaweza kuhoji kwamba kuendelea kuwepo kwa CCM madarakani hiyo ndiyo hatari kubwa kwa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani.
Mimi hilo silioni hivyo kwa sasa, na hata katika CCM ya enzi za Kikwete. Hatari iliongezeka zaidi alipoingia madarakani Magufuli na kutangaza waziwazi kutopenda uwepo wa vyama vya upinzani.
CCM wenyewe kama chama, hila zao zilikuwa ni za kawaida, mradi tu wanapata ushindi, hawakuwa na lengo maalum la kuua upinzani.
CHADEMA wafanye nini (samahani kwa kuwasema CHADEMA, badala ya vyama vya upinzani, kwa sababu vingine ndio hivyo tena vimetekwa).
Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.
Kati ya sifa chache, lakini muhimu alizojijengea Magufuli (sio CCM) ni kuonekana kuwa mtetezi wa mali na utajiri wa nchi hii na maendeleo ya wananchi wake.
Amejitambulisha bila shaka yoyote, kwamba yeye alikuwa ni mtetezi mkubwa wa maslahi ya Tanzania na wananchi wake. Amejenga hata ukuta, kulinda Tanzanite yetu iliyokuwa inatoroshwa kwenda nchi za nje na kuwanufaisha hao zaidi ya sisi tulivyokuwa tunanufaika kwayo.
Swala la madini aliliwekea mkazo sana; hata kama ilionekana kama kulikuwa na makosa katika juhudi hizo, lakini wananchi walielewa madhumuni yake. Kuna mifano mingi kuhusu msimamo wake juu ya mali za Tanzania.
Hatujui kuhusu mikataba mbalimbali nchi yetu iliyoiingia na nchi na mashirika mbalimbali ya kimataifa, lakini bado inaelekea wananchi waliamini kwamba mikataba hiyo ilikuwa ni kwa maslahi yao.
Jambo ambalo inawezekana hakulifanya vizuri ni kuhusu mashirikiano yetu na nchi mbalimbali duniani kwa vile alikazia zaidi "ubeberu" na mambo mengine kama masimango yao.
Nimeyaandika haya, ili CHADEMA watambue kwamba kama sera zao hazieleweki kwa wananchi, kazi yao itaendelea kuwa ngumu zaidi kuwashawishi wananchi hao kuwapa madaraka. Ni lazima wajieleze waziwazi kwa wananchi, wao ni nini hasa wanakisimamia kama chama cha siasa, na nchi yetu itafaidika vipi na misimamo yao hiyo kama watapewa ridhaa ya kuongoza serikali.
Kwa hiyo, nadhani ni halali sasa kusema kwamba adui mkubwa aliye mbele ya CHADEMA ni CHADEMA yenyewe. CCM wataendelea na hadaa zao kwa wananchi, hadaa za "Hawa ni Wenzetu" kama ilivyowahi kuwa huko nyuma, na wananchi kama hawaoni mbadala wa kuwapa madaraka, watarudi huko huko kwenye chama kilichooza ndani kwa ndani.
Niseme hapa, sijui kama Samia atakuwa na nguvu za kukibadilisha hiki chama kiwe chama cha wananchi wenyewe kwelikweli. Sijui.
Hatujui
Umesema sawa kabisa. Tatizo, inaelekea CHADEMA wenyewe wanachoamini ni kwamba wanafeli kwa sababu tu ya kuibiwa kura na hujuma zingine zinazofanywa na CCM. Sidhani kama wanaweka mkazo kwenye kuhakikisha wana sera mbadala zinazoeleweka kwa wananchi.
Mkuu nimependa hoja yako lakini hili suala lilifanyiwa kazi tokea 2012 ilipoanzishwa CHADEMA ni msingi na ndio iliopelekea hata kuimarishwa kwa kanda ili chama kishuke kwenye grassroots.Kazi kubwa iliyo mbele yao (CHADEMA), ni kuwaendea wananchi walipo,huko mitaani. Wasitegemee sana hizi siasa za majukwaani.
CCM imetumia udhaifu wao huo kwa vile wao CCM wako kila sehemu mitaani.
CHADEMA inabidi warekebishe muundo wao wa chama ili ngazi za mashina ziwe na sehemu muhimu zaidi ndani ya chama hicho.
Kazi kubwa iliyo mbele yao (CHADEMA), ni kuwaendea wananchi walipo,huko mitaani. Wasitegemee sana hizi siasa za majukwaani.
CCM imetumia udhaifu wao huo kwa vile wao CCM wako kila sehemu mitaani.
CHADEMA inabidi warekebishe muundo wao wa chama ili ngazi za mashina ziwe na sehemu muhimu zaidi ndani ya chama hicho.
Mkuu CHADEMA ilijijenga kupitia Agenda ya kupigania haki za wananchi hasa kiuchumi pale walipopambana na ufisadi, pingana na mikataba ya kinyonyaji na sheria kandamizi bungeni na majukwaani.Hilo linawezekana kama vyama vingine vya siasa vitaruhusu iwe hivyo.
Kuruhusu kunatokana na sababu mbalimbali, kama vyama hivyo kutoweka bidii kuwaondoa CCM.
Wananchi hawawezi kukabidhi nchi kwa chama chochote kisichokuwa tayari kulinda maslahi mapana ya nchi yao.
Kumbuka, ni wananchi wenyewe ndio wenye mamlaka ya mwisho, sio mtu mmoja tena au kikundi cha watu wachache walio na mabunduki na mabomu ya kutoa machozi.
Tanzania hatutegemei kurudi tena kiongozi wa aina hiyo hivi karibuni.
Dr slaa? Mbona jimboni kwake waliipa CHADEMA kuanzia ubunge hadi halmashauri? Sidhani kma hyo ni sababu....... Otherwise Lissu asingepata mapokezi ya kishujaa vile Karatu.Kimeozaje mkuu. Kujidanganya kwako ndo kosa kubwa sana. Unaongea as if CHadema imejaaa kila kitu safi na haki. Hapo ndo unaonekana mjinga. Kuwa mkweli hata kama inauma ndo dawa ya kweli. Kosa kubwa sana. MlifanyA kwa Dr slaa. Kama mbunge alifanya kazi kubwa jimboni kwake. Hivyo watu walimwamini. Sio maneno maneno ambayo ukiuliza kafanya Nini ohhhh anajua kutukana.