Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,660
- 218,148
Tumekwishaandika humu mara kadhaa kwamba wale wote waliosababisha uchafu kwenye nchi hii hawapaswi kuwa Mabalozi, Hii ni kwa sababu Balozi ni Mwakilishi wa Nchi yetu kwenye mataifa mengine, yaani Balozi ndio Taswira ya Nchi yetu kule Ugenini.
Mtu kama Gellasius Byakanwa, mtu mwenye roho mbaya na msiginaji mkubwa wa Katiba ya nchi hapaswi kuwa mwakilishi wa Tanzania popote, Uchafu alioutenda mtu huyu wakati wa awamu ya 5 hakuna aliyeusahau, huyu kuwa Taswira ya Tanzania Ugenini ni Aibu kwa nchi yetu, hapa Mamlaka ya Uteuzi imeteleza au imewadharau wananchi wa Tanzania kutokana na Kiburi cha madaraka.
Wakati wa uteuzi kama huu wa Humphrey Polepole niliweka andiko lenye kila ushahidi kwamba mtu yule hakupaswa kuwa balozi, na leo narudia tena kwa huyu Byakanwa, uteuzi huu unadhalilisha nchi.
Serikali iache kuwadharau raia wake kwa kuwateulia watu wasio na maadili yoyote, kwa vile raia hawana la kuwafanya, ikumbuke kwamba yupo Mungu ambaye hajawahi kukubali Ujinga.
Mtu kama Gellasius Byakanwa, mtu mwenye roho mbaya na msiginaji mkubwa wa Katiba ya nchi hapaswi kuwa mwakilishi wa Tanzania popote, Uchafu alioutenda mtu huyu wakati wa awamu ya 5 hakuna aliyeusahau, huyu kuwa Taswira ya Tanzania Ugenini ni Aibu kwa nchi yetu, hapa Mamlaka ya Uteuzi imeteleza au imewadharau wananchi wa Tanzania kutokana na Kiburi cha madaraka.
Wakati wa uteuzi kama huu wa Humphrey Polepole niliweka andiko lenye kila ushahidi kwamba mtu yule hakupaswa kuwa balozi, na leo narudia tena kwa huyu Byakanwa, uteuzi huu unadhalilisha nchi.
Serikali iache kuwadharau raia wake kwa kuwateulia watu wasio na maadili yoyote, kwa vile raia hawana la kuwafanya, ikumbuke kwamba yupo Mungu ambaye hajawahi kukubali Ujinga.