Chadema hela ya kufanyia mikutano wanatoa wapi?

Chadema hela ya kufanyia mikutano wanatoa wapi?

Wamepewa pesa toka kwa wafanyabiashara wa Ulaya. Ahadi waliyotoa mpaka wakapewa hizo pesa ni siri yao...
 
Yaani mtu kuuliza tu pesa zinatoka wapi ndio anashambuliwa kwa matusi makubwa namna hii!!!

Kwani kama hizo pesa ni halali kuna shida gani kutaja hivyo vyanzo?
 
Nyie si huwa mnasema FEDHA za CHADEMA zinatafunwa na DR. SLAA?!
Kumbe wakifanya mikutano mnapata majibu ya uongo wenu siyo?!
Njia ya mwongo ni fupi mkuu!
Waache CHADEMA watumie kidogo chao kuwaelimisha watanzania!
Za CCM sijui zinaenda wapi-kuhonga wapiga kura siyo?!
 
HATUNA MWANACHADEMA KAMA WEWE!
1. NILITEGEMEA UTA2WEKEA NYARAKA ZA UTAFITI WAKO,
2. UTATAJAJE KIAC CHA FEDHA KWA FEDHA YA KIGENI? NI ujinga na upumbavu 2mia Tsh ili na msomi wa chini aelewe. acha umbea kama kwel we ni msomi. unajua kuropoka ni ujng
 
Kwanza rekebisha kiasi cha pesa, umefanya makadilio ya chini sana kiasi cha kuhama kwenye uhalisia, kwa ufupi, mikutano ya CHADEMA ina husisha 'chopa', nadhani kwa makadilio ilipaswa uweke si chini ya milioni 100 kwa mkutano. Sasa uanze kuhoji, pesa wanatoa wapi?

Akili za kimwigulu mwigulu
 
Chadema ni ya wananchi inaendeshwa kwa sadaka ya wananchi.

Viongozi wa Chadema hawana tamaa ya fedha. wanahijaji pesa kidogo za chakula na malazi ili kufanya mikutano.

Pia baadhi ya viongozi wanatumia Pesa zao.
 
sisi wanachadema tunakichangia chama ndio maana mkutano ukiisha kuna box linapitishwa mwenye nacho anatoa!! pili Ruzuku inatusaidia.
Mleta mada amezoea mambo ya CCM kwamba kitu cha gharama ya 1,000/= kinaandikiwa 100,000/=
CHADEMA is a ZERO CORRUPT ZONE
 
Hii kasi inawatisha CCM. Hii kasi ya Chadema inahitaji watu ambao kweli wana mapenzi na chama na si wachumia tumbo kama wa CCM. CCM wanaogopa kwa kasi hii 2015 hawana chao
 
kwahiyo kumbe wanawakamua wananchi wavinjar na helkopta wakat wangeweza kutumia usafir wa barabara maana sasahv lami kila mahal

Acha ujinga wewe, stop kiding youself!!....Lami kila mahali!!!?? Unaishi wapi wewe ambako kila mahali unapotoka nyumbani kwako unatembea juu ya lami tu?? Unaifahamu au umewahi kufika Tabora wewe?? Niambie unapotoka huko "peponi" kuliko na lami kila mahali na labda umeamua kuja Tabora kisha uende Kigoma unapita lami ipi??...Stop fooling yourself!!....And for your information ni kwamba nchi hii ina ukubwa wa kilometa za mraba zaidi ya 900,000 na barabara za lami zilizojengwa na serikali ya CCM tangu uhuru mwaka 1961 si zaidi 4,500km na hizi maana yake changanya na za wakoloni wa kizungu,na hii hailingani na umri wa walioakaa madarakani wakiongoza serikali wa zaidi ya miaka 50!!

CCM wanakera sana kwani hii propaganda ya lami kila sehemu wanaitumia sana kutufanya sisi wananchi kama mafala flani hivi tusioelewa. Sasa we are ready to fight you everywhere mijini hadi vijini na tunahakikisha mwaka 2015 manaondoka wanaingia watu wapya toka chama kingine na hasa CHADEMA ili waje na mawazo mapya kwa ajili ya kuanza kuijenga nchi yetu ya Tanganyika upya!!
 
Nilitegemea jibu moja tu kwa mtu mwenye taarifa na mjadala ungekomea hapo ila ni kelele matusi na kejeli kibao!!!!

Siasa ya Tanzania ujengaji wa hoja bado chiiiiiniiiii saaaaaanaaaaa!!!!!!
 
Kwanza rekebisha kiasi cha pesa, umefanya makadilio ya chini sana kiasi cha kuhama kwenye uhalisia, kwa ufupi, mikutano ya CHADEMA ina husisha 'chopa', nadhani kwa makadilio ilipaswa uweke si chini ya milioni 100 kwa mkutano. Sasa uanze kuhoji, pesa wanatoa wapi?
Unaacha kuuliza mambo muhimu juu ya walioficha fedha Uswiss lini watatajwa na kurudisha fedha hizo zije zifanye shughuli za maendeleo kila mkilala,mkisinzia na mkiamka ni CDM tu.
 
Kwanza rekebisha kiasi cha pesa, umefanya makadilio ya chini sana kiasi cha kuhama kwenye uhalisia, kwa ufupi, mikutano ya CHADEMA ina husisha 'chopa', nadhani kwa makadilio ilipaswa uweke si chini ya milioni 100 kwa mkutano. Sasa uanze kuhoji, pesa wanatoa wapi?

Pesa tunazitoa benki. Na wakati mwingine mifukoni. CDM hawauzi sembe.
 
Why using $ currency? Mbulula ...

Mimi kama raia wa Tanzania ningependa kufahamu hela ya kufanyia mikutano ya CHADEMA inatoka wapi?

Kwa utafiti mdogo nilioufanya mikutano ya kitaifa inayofanywa na viongozi wa CHADEMA si chini ya dola za kimarekani 5000. Lakini cha ajabu CHADEMA wanaweza kufanya mikutano mingi sana bila ya kupumzika.

Nina nia nzuri sana ya kufahamu haya jamani. Mimi ni mwanachama hai wa CHADEMA na ningeomba viongozi au wanachama wenzangu mnijulishe kuhusu hili.
 
Hivi BAVICHA jinsia ya kike mnaifanya kama tusi?

Maana naona mnadhalilisha kweli mama na dada zetu. Kama huwezi kuitetea CHADEMA kwa hoja nenda kalime kijijini kwenu.

Ukiitwa mama ndo umetukanwa?
 
Kama kweli we mwanachama basi ndo umetokea CCM ambako mmezoea matumizi ya anasa. Hebu tupe mchanganuo wa hizo dola 5000,ndo tukuelimishe wapi ni sahihi na wapi si sahihi.
 
Back
Top Bottom