CHADEMA haitalipa kisasi-Dr Slaa

CHADEMA haitalipa kisasi-Dr Slaa

Mungu akiwa upande wetu nani atatushinda
 
Asante Dr. Slaa kwa hekima na busara zako tunamwomba Mungu aendelee kukulinda na akukinge dhidi ya mashetani yasiyoitakia nchi yetu mema.
 
Wabunge wa mikoa inayolima pamba Tanzania fuatilieni kwa makini sekta hii muhimu sana jamani wakulima wanachezewa kama watoto na watabaki masikini na kama hamtapaza sauti kuwasemea wakulima sisi vijana wakakamavu tunatanganza kuwangoa Cheyo,Chenge,Limbu,Kamani,Masele,Opuruka,Shibuda,Kasulumbayi,Kahagi,Luaga,Mkono,Nyerere,Mawe matatu,Kigwangala,Kafumu,nk ungana mtetee kwa thati wakulima wananyonywa sana na matajiri waliohongwa na wazungu kwa kushirikiana na waziri wa kilimo,waziri mkuu na rais!!!!!!!!!!!!!
 
Inatia moyo sana kuona sasa umemjua Mungu. Wengi wataweza kujumuika na wewe kupata vinywaji maana ilikuwa ni wasiwasi mtupu; Mungu anedelee kuibariki Chadema na aipushe na watu waovu kama Lwakatare
Chama
Gongo la mboto DSM

Hicho kiherehere chako hicho.....!
 
Mkuu wangu Ben Saanane hiyo ni kauli nzito kutoka kwa mtu mzito.Kamanda anayejiandaa kuingia madarakani kwa kura za wananchi.

Ni kweli mkuu ila hili ni mojawapo ya maamuzi magumu sana.Nimejifunza sana hapa
 
Last edited by a moderator:
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema hawatalipa kisasi hata baada ya mahakama kumfutia kesi ya ugaidi Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama hicho, Wilfred Lwakatare, kwa kigezo kuwa mashitaka hayo yalikuwa hayajitoshelezi kuitwa kuwa ni ya ugaidi.

Akizungumza na gazeti hili baada ya hukumu hiyo iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na kuvutia hisia za watu wengi Dk. Slaa alisema: “Tumesema toka mwanzo, tunaanza na Mungu, tunaendelea na Mungu na tutamaliza na Mungu, hujuma zozote dhidi ya CHADEMA kamwe hazitashinda kwa uwezo wa Mungu.

CHADEMA tunapigania ukombozi wa pili wa taifa letu, tunawapigania wanyonge, tunawapigania walalahoi. Hatukuwa, hatuna na hatutakuwa na sababu ya ugaidi.

Source:Tanzania Daima

Statement hii ni ishara tosha ya Gaidi at work. Kwani aliyeshtakiwa ni Chadema au Kada wake. Je Chadema ina uwezo wa kulipiza kisasi dhidi ya Serikali. Kama jibu ni ndio watalipoza kwa njia gani.
 
mwigulu wapi sasa? Nakumbuka uliongea bungen uko tayari kutoa ushahidi hata mbinguni,haaaaah haaaaah hivi unafikiri we unaweza ingia mbinguni na roho yakishetani hivyo? Poleni wafa maji
 
well said dr mungu akupe afya njema kwani bado watanzania wanakuitaji katika ukombozi wa nchi hii.


"clever person solves a problem, a wise person avoid it" albert einsten.
 
Hicho kiherehere chako hicho.....!
Mkuu sina kiherehere ila nafarijika sana kuona watu wanabadilika; nataka kuona vijana tunashindana kwa hoja na sera; hivi huoni faraja kuona hata habibu mchange anakaa na wewe na kuburudika na vinywaji bila hofu yoyote? Wanasiasa wazee wapo tayari kufanya lolote ili mradi tu waingie madarakani; wewe bado kijana sana una nafasi ya kurekebisha mambo kabla hujawasikiliza hao wazee fikiria kwa makini azma zao.
Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
hawa lolote cdm nimagaidi tu.

Heri kijana mwenye akili kuliko mzee mpumbavu asiyekuwa na busara. CHADEMA ni chama kichanga (Kijana); Nyinyiemu ni chama kikongwe (Mzee)

Aibu mnayo nyie; na Chadema inao uwezo huo wa kulipa kisasi au ni maneno ya kuropoka tu?ChamaGongo la mboto DSM

Mkuu sina kiherehere ila nafarijika sana kuona watu wanabadilika; nataka kuona vijana tunashindana kwa hoja na sera; hivi huoni faraja kuona hata habibu mchange anakaa na wewe na kuburudika na vinywaji bila hofu yoyote? Wanasiasa wazee wapo tayari kufanya lolote ili mradi tu waingie madarakani; wewe bado kijana sana una nafasi ya kurekebisha mambo kabla hujawasikiliza hao wazee fikiria kwa makini azma zao.
Chama
Gongo la mboto DSM

Kutoka kwa rogo mpaka kwa ILUNGA.
 
tenende
Umepotea mkuu karibu utumwagie pumba
Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Shukrani kwa hilo katibu mkuu CHADEMA, muda ulopo ni kukijenga chama zaidi pia kupigania namna ya kumwondolea mwananchi matatizo yamzongayo.Hawezi kutumia jundo kuua ssmizi au hatushindani mpumbavu ili tusije fafanae.Wananchi wanataka ukombozi wa matatizo yao na wala si vinginevyo, pana kero nyingi ambazo bado hazina wa kuwatatulia.Tupambane kuuondoa huu utawala dhalimu unaowanyonya raia wake.
 
Kesi hii ilikuwa ni kugharamia zile kesi mbili za Igunga na Sumbawanga Mjini, attention yote imehamia kwenye kesi huku magamba yamejirudishia ubunge kiulaini bila hata kupata report za maana.
 
Kesi hii ilikuwa ni kugharamia zile kesi mbili za Igunga na Sumbawanga Mjini, attention yote imehamia kwenye kesi huku magamba yamejirudishia ubunge kiulaini bila hata kupata report za maana.

Mkuu umewaza mbali sana..!
 
Back
Top Bottom