CHADEMA chatoa masaa 36 waliowavamia wabunge wake kukamatwa...

HARAKA HARAKA HAINA BARAKA, RPC Kasema wenye taarifa wapeleke nyie mnalazimisha akamate! Amkamate nani!? Kwani yeye alikuwepo kwenye tukio? Aliyekuwepo kwenye tukio ndo wa kutaja ni nani alikuwa na Panga na Shoka na awe tayari kuisaidia Polisi ili mtuhumiwa aweze kufikishwa mbele ya sheria.JF tuwe Great Thinker kweli sio kubwabwaja. Mfano kuna mtu kachangia hapa kwa kumtaja mtu hadi na namba yake ya Gari je, yuko tayari kwenda Polisi kuelezea? Je alishafanya hivyo!? Yuko tayari kwenda mbele ya Mahakama kutoa ushahidi huo!? Au ni chuki binafsi!? JF sio Polisi una uhakika kamuone RPC na ushahidi wako wa uhakika achukue maelezo ayafanyie kazi. Kusema itumike nguvu ya umma bado ni muendelezo wa uvunjifu wa amani kitu ambcho serikali yoyote haiko tayari maana azima itaingia kuwalinde wengine na hapo ndo LOH!

umesema vizuri mkuu.

wengi wanatanguliza ushabiki wa CDM halafu wanatelekeza utafakari wao.

Tanzania mambo yako hivi. Ukitendewa kosa, cha kwanza ni kwenda POLISI kufungua kesi, unapewa RB. Katika kufungua kesi, unataja tukio limetokea vipi, nani alihusika, alitumia nini, walikuwa wangapi na yanayofanan na hayo. ukisha fungua kesi, kinachofuata ni wewe kuonesha ushirikiano kuhakikisha wote waliohusika wanakamatwa. wakisha kamatwa, ushahidi unaandaliwa, wanaandikwa maelezo ndipo kesi inapelekwa kwa mwanasheria wa serikali, baada ya hapo kesi inapelekwa mahakamani na taratibu nyingine zinaendelea.

sasa hawa jamaa, wameshambuliwa usiku, tena wa manane, hatujajua kama wamefungua kesi na kama waliwataja wahusika, lakini wanataka wakamatwe. utamkamata nani wakati hana kesi inayomkabili? kama siyo kumuunea ni nini? fuata utaratibu ili uwe na sababu ya kulalamika.

lakini pia hawa wabunge waje watueleze kwa kina saa nane usiku walikuwa wanashughuli gani kwenye mitaa ya watu usiku
 
ukiwataja watu wenye ukwasi rpc mstaafu alfred gewe mtoe kabisa jamaa ni muadilifu na anaishi maisha ya kawaida sana hapo tabata kimanga,hajawahi kuwa fisadi kama great thinkers vema tukawa tunafanya utafiti kabla ya kuchafua watu

bora umesema mkuuu
 
mlanduka ndumu huyu, analopoka tu. hili saga wanalifahamu vizuri CHADEMA, na linaweza kula kwao. time will tel
Huna lolote tumeshawazoea kila wakati mnasema hivyo eti itakula kwao na CDM inazidi kusonga mbele. Kifupi jeshi la polisi limeoza hata ulitetee vipi, polisi inatakiwa kufanyia kazi clue inazopewa na wananchi na sio kusubiri kutafuniwa hadi wapelekewe majina ya wahalifu wao kazi yao ni nini sasa, kuua kwa risasi au.
 
''ni viumbe wawili tu dunian hawakuwa na nyongo ni Yesu na Muhammad'' by Livingstone Lusinde

Lusinde kweli hamnazo kabisa,jana nilikua namsikiliza mifano yake ku justify upuuzi wake,mwenyewe nikabaki nacheka tu,mara huo mfano wa Yesu na Mtume,mara mfano wa Sugu na Clouds!ila Kayanda alimbana vizuri sana akawa anajiuma tu,sio Kibonde kabaki na kauli zake za mnalipeleka wapi taifa ili,mara kama Lusinde ameomba msamaha ni uungwana kwa hiyo kama hawataki kumsamehe (c.d.m hasa viongozi) ilo ni juu yao,huyu kibonde nae hamnazo kweli,nini umuhimu wa uwepo wa mahakama?kama ni hivyo si kila mtu basi awe anatenda kosa na kuomba msamaha kwa kua ni uungwana!
 
umesema vizuri mkuu.

wengi wanatanguliza ushabiki wa CDM halafu wanatelekeza utafakari wao.

Tanzania mambo yako hivi. Ukitendewa kosa, cha kwanza ni kwenda POLISI kufungua kesi, unapewa RB. Katika kufungua kesi, unataja tukio limetokea vipi, nani alihusika, alitumia nini, walikuwa wangapi na yanayofanan na hayo. ukisha fungua kesi, kinachofuata ni wewe kuonesha ushirikiano kuhakikisha wote waliohusika wanakamatwa. wakisha kamatwa, ushahidi unaandaliwa, wanaandikwa maelezo ndipo kesi inapelekwa kwa mwanasheria wa serikali, baada ya hapo kesi inapelekwa mahakamani na taratibu nyingine zinaendelea.

sasa hawa jamaa, wameshambuliwa usiku, tena wa manane, hatujajua kama wamefungua kesi na kama waliwataja wahusika, lakini wanataka wakamatwe. utamkamata nani wakati hana kesi inayomkabili? kama siyo kumuunea ni nini? fuata utaratibu ili uwe na sababu ya kulalamika.

lakini pia hawa wabunge waje watueleze kwa kina saa nane usiku walikuwa wanashughuli gani kwenye mitaa ya watu usiku

Kwani nchi ina curfew kuzuia kutembea baadhi ya miji au mitaa usiku wa manane?pili we unajuaje kama hawa wabunge kama hawakutoa taarifa polisi juu ya tukio ilo?kwa hiyo walienda kutibiwa Bugando kinyemela tu bila ya kua na Pf.3 ?na mpaka R.C.O anasema kua uchunguzi wa tukio ilo unaendelea na wahusika watatiwa nguvuni ina maana tukio halijaripotiwa tu kama unavyotaka kutuaminisha wewe?
 
umesema vizuri mkuu.

wengi wanatanguliza ushabiki wa CDM halafu wanatelekeza utafakari wao.

Tanzania mambo yako hivi. Ukitendewa kosa, cha kwanza ni kwenda POLISI kufungua kesi, unapewa RB. Katika kufungua kesi, unataja tukio limetokea vipi, nani alihusika, alitumia nini, walikuwa wangapi na yanayofanan na hayo. ukisha fungua kesi, kinachofuata ni wewe kuonesha ushirikiano kuhakikisha wote waliohusika wanakamatwa. wakisha kamatwa, ushahidi unaandaliwa, wanaandikwa maelezo ndipo kesi inapelekwa kwa mwanasheria wa serikali, baada ya hapo kesi inapelekwa mahakamani na taratibu nyingine zinaendelea.

sasa hawa jamaa, wameshambuliwa usiku, tena wa manane, hatujajua kama wamefungua kesi na kama waliwataja wahusika, lakini wanataka wakamatwe. utamkamata nani wakati hana kesi inayomkabili? kama siyo kumuunea ni nini? fuata utaratibu ili uwe na sababu ya kulalamika.

lakini pia hawa wabunge waje watueleze kwa kina saa nane usiku walikuwa wanashughuli gani kwenye mitaa ya watu usiku
Nafikiri wewe sio mtanzania, kama ungekuwa mtanzania ungekuwa na habari kuwa jeshi la polisi linashika namba moja kwa rushwa, ungejua pia kuwa hata huo utaratibu unaosema wa kuanzia RB hadi kesi kwenda mahakamani ni rushwa tupu.

Watu wamekatwa mapanga tena viongozi wa wananchi unataka kutuambia polisi hawawezi kuwatafuta wahalifu hadi kesi ifunguliwe, kwani imekuwa kesi ya madai. Hata kama polisi hawakuwepo siku ya tukio ile kusikia taarifa tu inatosha kwa jeshi kufuatilia. Lakini sikushangai kwa jinsi unavyowatetea kwa vile natambua kwenye jamii yeyote watu wa aina yako wanaotetea utendaji mbovu wa serikali legelege lazima wawepo.
 
Kwani nchi ina curfew kuzuia kutembea baadhi ya miji au mitaa usiku wa manane?pili we unajuaje kama hawa wabunge kama hawakutoa taarifa polisi juu ya tukio ilo?kwa hiyo walienda kutibiwa Bugando kinyemela tu bila ya kua na Pf.3 ?na mpaka R.C.O anasema kua uchunguzi wa tukio ilo unaendelea na wahusika watatiwa nguvuni ina maana tukio halijaripotiwa tu kama unavyotaka kutuaminisha wewe?
Unajua kuna watu ni kama wametiwa ufunguo kwamba nenda katetee, hajui hata pa kuanzia na aseme nini. Hajui kuwa wabunge walipata pf3, hajui kuwa kuna askari walikuwepo kwenye tukio, hajui kuwa kuna majina yameshatajwa sasa yeye anakuja kulalamika eti CDM wameficha majina. Mtu wa aina hii lazima atakuwa na matatizo.
 
HARAKA HARAKA HAINA BARAKA, RPC Kasema wenye taarifa wapeleke nyie mnalazimisha akamate! Amkamate nani!? Kwani yeye alikuwepo kwenye tukio? Aliyekuwepo kwenye tukio ndo wa kutaja ni nani alikuwa na Panga na Shoka na awe tayari kuisaidia Polisi ili mtuhumiwa aweze kufikishwa mbele ya sheria.JF tuwe Great Thinker kweli sio kubwabwaja. Mfano kuna mtu kachangia hapa kwa kumtaja mtu hadi na namba yake ya Gari je, yuko tayari kwenda Polisi kuelezea? Je alishafanya hivyo!? Yuko tayari kwenda mbele ya Mahakama kutoa ushahidi huo!? Au ni chuki binafsi!? JF sio Polisi una uhakika kamuone RPC na ushahidi wako wa uhakika achukue maelezo ayafanyie kazi. Kusema itumike nguvu ya umma bado ni muendelezo wa uvunjifu wa amani kitu ambcho serikali yoyote haiko tayari maana azima itaingia kuwalinde wengine na hapo ndo LOH!

Wewe usiongee mambo kama vile haujuhi utendaji mbovu na ubambikaji wa kesi unaofanywa na jeshi la polisi la nchi hii,kwanza kuhusu hayo majina na namba ya ilo gari lililotelekezwa ni maelezo yaliyotolewa na Mh Kabwe na vyombo vya habari na hata R.C.O Burlow alithibitisha juu ya gari lenye number hizo kutelekezwa,akabanwa na muandishi wa habari kua kwa nini wanashndwa kuwakamata wahusika kama tayari kuna viashiria kama hivyo,yeye akawa mkali !ahiitaji kuwa na uelewa wa sheria kujua kua hao watu ndio prime suspects kama alivyosema Zitto,labda uwe na ubongo mgumu sana kama jiwe la milima urugulu!pili mkuu ili jeshi letu la polisi limejaa magumashi tupu,yaani ukienda kichwa kichwa ujifanye unataka kutoa ushahidi na wewe ni mtu kapuku tu,unageuziwa kesi wewe na unakwenda jela,nakuambia hivyo sababu mimi ilishanitokea,kuna mtu alitaka kutumia kijicheo chake kunitapeli kiasi changu kadhaha,nikareport ili suala polisi urafiki,siku ya kwanza polisi walinipa ushirikiano vizuri mpaka mtuhumiwa akakamatwa,ila kesho yake baada ya jamaha na mkewe kuanza kuwakatia noti polisi,kesi yangu wakawa wanairusha rusha na mwisho wa siku wakanigeuzia mimi kibao,bahati kwangu ni kua kuna moja ya ndugu yangu anajuana na Adadi Rajabu kipindi hiko akiwa bado askari,kwa hiyo baada ya Adadi kupiga simu na kutaka kujua sakata zima walistuka na kujifanya hakuna shida wao wanalishughulikia,baada ya kujua ni msala wale askari wakawa ni rafiki wa upande wangu,na wakambana yule mtu kua either kesi ipelekwe mbele au arudishe pesa,jamaha nae baada ya kuona mambo sio ikabidi akubali kulipa hiyo pesa kwa awamu mbili ndani ya mwezi,hapo ndipo nikapata haki yangu!je ningekua sijuani na mtu yeyote maana yake si ningekua nimedhulumiwa pesa yangu na pengine kua jela sasa?msiongee kama vile hamjui uozo wa jeshi la polisi wakati mpaka mkuu wa nchi anapigia kelele ilo
 
Unajua kuna watu ni kama wametiwa ufunguo kwamba nenda katetee, hajui hata pa kuanzia na aseme nini. Hajui kuwa wabunge walipata pf3, hajui kuwa kuna askari walikuwepo kwenye tukio, hajui kuwa kuna majina yameshatajwa sasa yeye anakuja kulalamika eti CDM wameficha majina. Mtu wa aina hii lazima atakuwa na matatizo.

Ni kweli mkuu,ila sishangai,hao ndio vijana wengi ambao bado wanakumbatia u****a unaofanywa na magamba,maana hata argument zao utajua tu ni mtu wa aina gani hata kama haujamuona!ni kutojielewa tu,tusiwalaumu wala kuwatusi,twende nao taratibu maana wanahitaji ukombozi wa kifikra kwanza!
 
umesema vizuri mkuu.

wengi wanatanguliza ushabiki wa CDM halafu wanatelekeza utafakari wao.

Tanzania mambo yako hivi. Ukitendewa kosa, cha kwanza ni kwenda POLISI kufungua kesi, unapewa RB. Katika kufungua kesi, unataja tukio limetokea vipi, nani alihusika, alitumia nini, walikuwa wangapi na yanayofanan na hayo. ukisha fungua kesi, kinachofuata ni wewe kuonesha ushirikiano kuhakikisha wote waliohusika wanakamatwa. wakisha kamatwa, ushahidi unaandaliwa, wanaandikwa maelezo ndipo kesi inapelekwa kwa mwanasheria wa serikali, baada ya hapo kesi inapelekwa mahakamani na taratibu nyingine zinaendelea.

sasa hawa jamaa, wameshambuliwa usiku, tena wa manane, hatujajua kama wamefungua kesi na kama waliwataja wahusika, lakini wanataka wakamatwe. utamkamata nani wakati hana kesi inayomkabili? kama siyo kumuunea ni nini? fuata utaratibu ili uwe na sababu ya kulalamika.

lakini pia hawa wabunge waje watueleze kwa kina saa nane usiku walikuwa wanashughuli gani kwenye mitaa ya watu usiku


Ni mara yangu ya kwanza nakuona unachangia very low kiasi hiki.

Wabunge walishahojiwa na polisi siku ile ile ya tukio na bado tena polisi wamekwenda kuwahoji hospitalini walikolazwa.

Akili ya kawaida ilitosha kukufahamisha kwamba huwezi kupokelewa hospitali na kutibiwa majeraha kama yale bila kuwa na form ya polisi PF3, sasa kama unafahamu utaratibu wa polisi wanapotoa PF3 ungefahamu kwamba lazima kuna mahojiano, ama taarifa za awali za kushambuliwa kwao zilitolewa.

Pili ni muhimu ukatuliza akili yako ukapima kauli kinzani na tata zinazotolewa na rpc barlow na rco wake. Kama hata gari moja imekamatwa eneo la tukio kwani polisi wameshindwa nini kuanza na huyo mwenye gari? Nini maana ya wao kuwa jeshi la polisi kama hawawezi kufanya uchunguzi hadi wananchi wawapelekee ushahidi, mbona wakisikia maandamano ya chadema wanakurupuka na taarifa za kiintelijensia? kwanini katika matukio yanayowahusisha wanaccm kuwashambulia wapinzani kunakuwa hakuna taarifa za kiintelijensia?

Halafu hii ya kusema walikuwa wanafanya nini usiku wa manane nimeisikia tena kwako kama walivyoisema rco na rpc, mnatumia sheria za wapi ninyi wenzetu? Yani mnajaribu kuhalalisha uhalifu uliofanywa na ccm kwa visingizio vya kitoto kabisa. Wabunge wetu wameshambuliwa na mungiki ya ccm mbele ya polisi, kwanini tusiwatilie shaka polisi kwamba walishirikiana na mungiki wa ccm kuwahujumu wabunge wetu? ni dhahiri kwamba hizi danadana za kauli tata za rco na rpc inaashiria kushirikiana kwa ccm na polisi kutaka kuwaua wabunge wetu.
 
Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza fanyeni kazi Kamanda Baro please usijizalilishe kwa hili onyesha ukomavu wako katika utumishi wa umma siyo wa ccm.
 
huyu jamaa sijui ni muuaji? sikuelewi sijui huo u ccm wako unakupeleka wapi hadi unapunguza huwezo wako wakuhoji,kama we nimfatiliaji ukusikia walichokuwa wanakifanya usiku ule! kwa hiyo unatumia jukwaa letu kubariki matukio yasiyo yakibinadamu? ni meshangazwa sana na wewe.ni bora ulete hoja nyingine sio hii,haikubariki.
 
Unyama huu hauvumiliki kamwe kwani sasa imekuwa ni kawaida kwa wale wasiopeenda chama cha magamba kuchalangwa mapanga. ilitokea Igunga, mtu kamwagiwa tindikali huko Arumeru na sasa Mwanza. kwa vile polisi wamehindwa, basi nguvu ya umma itumike maana polisi always ni kulinda tabaka tawala.
 
Polisi ndo walitakiwa wawapeleke hao wahalifu kwenye vyombo vya sheria, sasa kama wanashindwa kazi yao inatakiwa uma ichukue nafasi kwani wao ndo wamewaajiri. wewe mfanyakazi wako nyumbani akishindwa kufanya kazi uliomwagiza unampleka mahakamani au unamtimua make ameshindwa kazi na kuifanya hiyo kazi au kumwajiri mtu mwingine. UMMA ufanye kazi ili kuimkumbusha polisi na serikali wajibu wake make inaonekana wako likizo.MAKAMANDA HAKUNA KULALA MPAKA WAHALIFU WASHUGHULIKIWE. PEOPLE's POWER.
 
Nguvu ya uma ifanye kazi yake kwani polisi wetu ni ccm waliacha wabunge wetu wapigwe mapanga. Polisi wetu wanachojua ni kukanusha tu.
 
Mimi naamini kama tukio hili lingetokea upande mwingine yaani kama wafuasi wa CDM ndio wangefanya vile, basi kwa wakati huu viongozi wengi sana wa CDM wangekuwa ndani kuanzia M/kiti wa CDM Mwanza, wabunge, hata viongozi wengine wa kitaifa wangehusishwa kuwa walibariki au kuagiza.

Ninachokiona hapa ni kuwa kama serikali isipoingilia kati unyanyasaji huu wa wazi unaofanywa na jeshi la polisi basi tuendako si salama, maana watu watachoka na kuamua kuingia kwa familia za kina Barlow na kulipiza kisasi. Sitaki tufike huko lakini ni angalizo kwa watawala wetu.
 
Wameshatajwa wahusika wengine ni viongoz wa ccm na uvccm na magari yaliyotumika yametajwa lakin polisi wamekamatwa dagaa wakawaacha wavuvi na sasa wanawataka wabunge wawapelekee ushahidi kituoni.
 
ndg CDM acheni ushabiki panapo sheria kama mnawajua watuhumiwa kweli pelekeni taarifa zao polisi na sio vitisho
 
Back
Top Bottom