Chadema acheni kutuchezea... nendeni mahakamani tu...!

When you you have no reasoning ability this is what we get.................................no reasons but gushing anger.........and frustrations but can not explain why.......................................The cost of ignorance is always visible to the knower...........

when analysis is based on emotions....this is what you bubble out....we read you and indeed we can tell how you think...piece of advise....you don't worth to be called policy analyst....ohhh....you branded yourself policy analyst....poor you!

 
Ipo sheria ya uchaguzi ambayo NEC hawakuifuata na mahakama inayohaki kama ikiombwa kuchunguza jambo hili...........................ushauri ..[/QUOTE]

Upo uwezekano wa CHADEMA kuhoji kazi ya NEC mahakamani. Ila tukirudi katika Katika hali ya kawaida ya mahakama zetu kweli unategemea mahakama iseme kuwa kwenye matokeo ya uchaguzi wa urais tume ilikosea? Hiyo iliwezekana tu wakati wa uhai wa kina Lugakingira na kwa hali ilivyo sasa itatuchukua miaka mingi kupata uamuzi kama huo kama katiba ya nchi haitabadilika.

Wenzetu Kenya sasa kwenye katiba yao wameweka kabisa kuwa baada ya matokeo tume itamtangaza aliyeshinda kura ila kuna zaidi ya siku 28 ambazo ni za kusikiliza malalamiko yoote ndipo anatangazwa kuwa rais na ndipo anaapishwa. Ni vigumu kwa nchi zetu za kiafrika nafikiri hata zilizoendelea kuendesha kesi inayomhusu rais aliyepo madarakani hata kama katiba na sheria zinaruhusu.

Kama CHADEMA wataenda mahakamani yafuatayo ndo yatatokea
1) Kesi itakuwa inapigwa tarehe na wataambiwa wasiongelee suala lililopo mahakamani,
2) Kama kesi itasikilizwa kwe PH wataambiwa kuwa kesi haina tija kwa maendeleo ya nchi hii,
3) Au itasikilizwa taratibu na ifikapo mwaka 2014 hukumu itatolewa ikisema hili ni suala la kisiasa lipelekwe bungeni.

Kwa maoni yangu naishauri CHADEMA ilalamikie uchaguzi wa madiwani na wabunge mahakamani. Hili la uraisi iendelee kumsusia mpaka atakapoanza mchakato wa kuunda tume huru ya uchaguzi. Othe approaches are kineticaly feasible but are not thermodynamicaly feasible.
 
Nimepata kuwa na mjadala na Ruta (mweka thread hii) juu ya katiba na suala la kupinga mahakamani maamuzi ya NEC. Jamani, nashangaa suala hili bado linazidi kuchanganya tu watu. KATBA YETU HAIRUHUSU KWENDA MAHAKAMANI KUPINGA KILE NEC ILICHOFANYA. MI SIELEWI TATIZO LIKO WAPI. SIELEWI. TUTAISHIA KUWALAUMU CHADEMA BURE. MTU AKITAKA KWENDA MAHAKAMNI ATAISHITAKI NEC AU JK AU CCM? KATIBA INASEMAJE? SOMENI KATIBA JAMANI............!!!!!
 
Chadema tumewachagua kutuwakilisha bungeni na wala siyo vinginevyo......wasipokwenda bungeni kwa visingizio vyovyote vile hapo watakuwa wanamkomoa mpigakura na wasifikiri tutawachagua tena........................next time tutakaa nyumbani na wacha hao CCM waendelee kututesa maana yawezekana kabisa taifa hili Mwenyezi Mungu kalilaani................

Kama Chadema wana ushahidi wa ya kuwa kura za vituoni zinatofautiana na zile ambazo NEC ilizitangaza sasa ni nini kinawazuia kulalamika mahakamani? Hicho kiji-Ibara cha katiba cha kuzuia matokeo ya kura za Uraisi yaliyotangazwa na NEC kuhojiwa mahakamani msikisome kijuu juu tu........Hakizuii hoja za kimsingi kusikilizwa na mahakama zetu na huo ni msimamo wao wa tangu mwaka 1995........Kumbukeni kazi ya kutafsiri sheria ni ya mahakama......nendeni huko mkadai haki yenu na kama mahakama ikikataa kuwasikiliza sasa ndiyo mrudi kwetu na hapo tutajua ya kuwa hata mahakama zinadi ukarafati mzito..

Katiba yetu iliweka dhana ya kuwa matokeo yaliyotangazwa na NEC kulingana na taratibu za kisheria ndiyo tu ambayo mahakama haiwezi kuyahoji lakini katiba yetu haikukusudia ya kuwa NEC wavunje sheria za uchaguzi katika kuyatangaza matokeo hayo na mahakama zinapolalamikiwa zikae kimya........................la hasha.................siyo hivyo hata kidogo........

Madai ya chadema kama yana ushahidi ni lazima yafikishwe mahakamani na hoja ya muhimu ni kuwa NEC haikufuata sheria ya uchaguzi na taratibu zake kwa kuyadharau matokeo ya kura kama zilivyopigwa na wananchi na wao kujitangazia matokeo wayatakayo tu wenyewe.........................Mahakama ikipata ushahidi wa kutosha na kuridhika itayatengua matokeo ya Uraisi kwa sababu hayakuheshimu ridhaa ya wapigakura.....................

Nje ya kuufuata utaratibu huu wa kisheria Chadema nasema acheni kutuchezea watu wazima na nendeni bungeni mkafanye kazi tuliyowatuma kama hamtaki semeni na chaguzi za majimbo mliyoshinda zirudiwe na wanaotaka kutuhudumia hata kama ni kutudhulumu wache wafanikiwe kwenye malengo yao.....................

What we asking from Chadema is leadership but not a bunch of endless complaints

Kwa pumba hizi huwezi kuwa ulichagua mabadiliko kwa sababu mabadiliko yanaletwa na wanaharakati ambao daima wanatafuta njia ya kufikisha ujumbe kwa wahusika ili kuhamasisha mabadiliko. rudi home ukasome katiba inasemaje...stop that bunch of nosenses!
 
Kama CHADEMA wataenda mahakamani yafuatayo ndo yatatokea
1) Kesi itakuwa inapigwa tarehe na wataambiwa wasiongelee suala lililopo mahakamani,
2) Kama kesi itasikilizwa kwe PH wataambiwa kuwa kesi haina tija kwa maendeleo ya nchi hii,
3) Au itasikilizwa taratibu na ifikapo mwaka 2014 hukumu itatolewa ikisema hili ni suala la kisiasa lipelekwe bungeni.

Kwa maoni yangu naishauri CHADEMA ilalamikie uchaguzi wa madiwani na wabunge mahakamani. Hili la uraisi iendelee kumsusia mpaka atakapoanza mchakato wa kuunda tume huru ya uchaguzi. Othe approaches are kineticaly feasible but are not thermodynamicaly feasible.

Hizi ni hisia ambazo huwezi ukazithibitisha...................na kama kesi itacheleweshwa kwa makusudi na mahakama hii itakuwa ni sababu nyingine ya kudai ufumbuzi wa mfumo mzima wa kimahakama.................tatizo la pendekezo lako la kumsusia hilo kwa JK ni sawasawa kabisa na msemo usemao .....dua ya kuku haimpati mwewe.....................atawapuuza....lakini Chadema wakienda mahakamani atawaita kutafuta suluhisho nje ya mahakama.......................kwa njia ya mazungumzo ya kuirekebisha katiba....................
 
Kwa pumba hizi huwezi kuwa ulichagua mabadiliko kwa sababu mabadiliko yanaletwa na wanaharakati ambao daima wanatafuta njia ya kufikisha ujumbe kwa wahusika ili kuhamasisha mabadiliko. rudi home ukasome katiba inasemaje...stop that bunch of nosenses!

Tatizo lako ni darasa dogo...........ningependa kufahamu elimu ulionao....................maana naona hutoi hoja yoyote ila unabeza tu....................hizi ni sifa za mbumbumbu tu..................................pole sana.................

Soma Ibara ya 41(5) ambayo imeweka bayana NEC ni lazima iheshimu sheria ya uchaguzi na taratibu zake katika kumpata Raisi wa Jamhuri ya Muungano........................Hili NEC hawakulifuata sasa kwa nini Mahakama isiwasikilize Chadema?

Ibara ya 41 (7) ambayo wengi wenu mnaisoma kijuujuu imeweka bayana ya kuwa Raisi aliyechaguliwa kulingana na Ibara hii ya 41 ikimaanisha na Ibara ndogo ya 41(5) imejumuishwa..............................sasa kama NEC haikuiheshimu Ibara ndogo ya 41(5) ni kuwa hawakuwa na mamlaka ya kisheria ya kumtangaza JK kuwa Raisi na mahakama inayo mamlaka chini ya Ibara ya 41(7) kuchunguza ni kwa nini NEC haikuheshimu maangalizo yaliyomo katika Ibara ya 41(7) ambayo ni kuwa mchakakto mzima wa Uraisi ni lazima uzingatie Ibara nzima ya 41 ya Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.................
 
Nimepata kuwa na mjadala na Ruta (mweka thread hii) juu ya katiba na suala la kupinga mahakamani maamuzi ya NEC. Jamani, nashangaa suala hili bado linazidi kuchanganya tu watu. KATBA YETU HAIRUHUSU KWENDA MAHAKAMANI KUPINGA KILE NEC ILICHOFANYA. MI SIELEWI TATIZO LIKO WAPI. SIELEWI. TUTAISHIA KUWALAUMU CHADEMA BURE. MTU AKITAKA KWENDA MAHAKAMNI ATAISHITAKI NEC AU JK AU CCM? KATIBA INASEMAJE? SOMENI KATIBA JAMANI............!!!!!
Pole sana kasome Ibara Na 41(5) ya Katiba ambayo yasema NEC ni lazima iheshimu taratibu za kisheria za sheria ya uchaguzi zilizowekwa katika kumpata Raisi..........................na baada ya hapo rudia kusoma Ibara Na. 41(7) ambayo imeweka bayana kuwa matokeo ya Uraisi hayatahojiwa na chombo cho chote kama yalipatikana kulingana na maelekezo ya Ibara hii ya 41......................

Swali ambalo unapaswa kujiuliza hivi NEC walizingatia Ibara 41(5) ya katiba katika kumtangaza JK kuwa ni Raisi? Jibu ni hapana.........sasa kama ni hapana maangalizo yaliyotolewa na katiba ya aina gani ya matokeo ya Uraisi ambayo mahakama haiwezi kuyahoji imetimizwa? Jibu ni hapana............Sasa hoja ya kuwa Ibara 41(7) imekataza mahakama kuingilia NEC inatoka wapi?

Labda kwa manufaa ya ambao hawajui Ibara hii ya 41(5) ninainakili hapa:-

"All the other matters concerning to the procedures for the election of the President, shall be as provided for in law enacted by Parliament in that behalf,..............................

Sasa Ibara ya 41(7) ambayo wengi humu wanaikimbilia kutetea ututusa uliomo ndani ya Chadema ni hii hapa:-

"When a candidate is declared by the Electoral Commission to have been duly elected in accordance with this Article, then no court of law of law shall any power to inquire into the election of that candidate."

Maeneo niliyoyawekea alama nyekundu ndiyo ambayo mahakama itabidi iyachunguze ya kuwa je NEC iliheshimu Ibara ndogo 41(5) kabla ya kumtangaza JK kuwa Raisi wetu na hivyo kuinyima mahakama uhuru wa kuchunguza matokeo hayo? Na matokeo ambayo mahakama haiwezi kuyachunguza ni yale tu ambayo mahakama itajithibitishia ya kuwa hayakukiuka Ibara yote ya 41 kama angalizo hili lisemalo.................................."...........to have been duly elected in accordance with this Article....................."

Acheni kutetea ututusa wa kishera ndani ya Chadema na hii siyo mara yao ya kwanza...................Kumbuka katika chaguzi ndogo ya kule Mbeya waligoma kwenda mahakamani wakidai chaguzi kuu ilikuwa karibu...........What a nonsense!!!........Hii ilitokana na NEC kuliondoa jina la mgombea wake wa Chadema kwa visingizio hakuweka sahihi na mhuri wa hakimu kama sheria ndogo ya uchaguzi inavyoelekeza............mzimu huo wa kutokwenda mahakamani umewasababishia Chadema madhara ya wagombea wake wengi kwenye chaguzi kuu waliokuwa wakidai wanaisubiria na hivyo kuenguliwa kwa tatizo ambalo mahakama ingekuwa imelifuta siku nyingi la kukataza sheria ndogo ndogo kuwanyima wapigakura haki ya kimsingi ya kikatiba ya kuchagua viongozi wao.........Dosari ndogo ndogo za sheria za uchaguzi zilipaswa kutumika kuwapa waliokosea angalau nafasi moja ya kwenda kuzirekebisha badala ya utaratibu wa hivi sasa kuwa ni nyundo ya kuwanyang'anya wapigakura haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi wao wawapendao.
 
Back
Top Bottom