Elections 2010 CF: Kwanini Dr. Slaa ni Chaguo sahihi

Watu wamemsikiliza Lipumba, Kikwete (na watapata dose nyingine baadaye leo).. na Dr. Slaa je ni kweli basi kuwa Dr. Slaa ndiyo chaguo sahihi na chaguo bora?
 
Kwa sababu tunataka kujenga na kusomesha kwa warrant kama tulivyosoma sisi. I remember nilikuwa nasafiri toka Bukoba hadi Ifunda Iringa kwa warrant ya serilali ya Tshs 6.40 (!970 - 1974). Hayo yalipotea baada ya Kupelekwa Utumwani (UKOLONI MATUMIZI) Misiri:yield::yield::yield:
 
Mwanakijiji,

Baada ya kukisoma hicho kijalida ulichoambatanisha humu, naomba nitofautiane na wewe kama ifuatavyo.

1. Je Slaa (au CHADEMA) ni chaguo sahihi?

Kabla ya kutoa msimamo wangu, naomba nikukumbushe kuwa kiasi cha miezi miwili nyuma ulitoa mada humu ambapo ulitoa mawazo yako kuwa CHADEMA si chama sahihi kwa sasa na hata ulitoa tofauti ya Chama cha upinzani na Chama cha uongozi. Kama sikosei hitimisho lako lilikuwa kuwa CHADEMA si chama muafaka kwa sasa. Kama nimekunukuu vibaya ni bahati mbaya lakini hoja zangu hapa chini zinalenga kujenga msimamo wangu.

2. Slaa na viongozi CHADEMA kuandamwa
Umezungumzia kuandamwa kwa Dr Slaa. Sijui lengo ni nini lakini ukumbuke hiyo ndio siasa. Kwani mbona Kikwete na CCM wanaandamwa sana na hata humu JF hilo ni la kawaida. Sasa kuandamwa kwa Slaa au CHADEMA kuna jambo gani la ajabu?

3. Tofauti ya Slaa na Kikwete
Unatwambia kuwa Slaa ni bora kwa sababu anazungumzia mabadiliko (kuanza upya) wakati Kikwete anazungumzia maboresho.
Naomba nikukumbushe kuwa Kikwete anawakilisha chama kilichopo madarakani na ambacho sera zake ndizo zinatumika kwa sasa. Kwa hiyo yeye hawezi kuzungumzia kuanza upya kwa sababu tayari wana msingi wa sere zao. Kuanza upya kwao inawezekana tu kama sera fulani imethibitika na wao wenyewe kuwa imefeli. Kama hawajakiri hicho unategemeaje azungumzie kuanza upya. Jambo la kuzingatia ni kama mhusika anaona mapungufu na ameandaa maboresho. Hilo hata jarida lako ninakiri kuwa lipo. Kwa CCM kuzungumzia kuanza upya ni sababu tosha ya kuwabadilisha maana watakuwa wanafanya majaribio.

4. Sera za CCM zinajali uwingi

Hapa naelewa kuwa kuwa na vitu vingi ambavyo havikidhi viwango ni sawa na sifuri. Mh. Mkapa aliwahi kulizungumza hili na hasa katika elimu. Yeye alihoji, lipi bora tuanza na shule ambazo hata kama hazikidhi hivyo viwango ili tuendelee kuziboresha au tusubiri mpaka pale tunapokuwa na uwezo wa kutimiza hivyo vigezo ndio tuanze? Swali likaja, ni nani ambaye yuko tayari mtoto wake asubiri asipate elimu hadi hapo tutakapokuwa na uwezo wa kufanya hivyo? Jibu hakuna. Kwa hali hiyo, the only option ni kuwa na shule, hospitali na huduma zingine kila mahali na huku tukiendelea kuziboresha. Kwa hili sioni mbadala bado naamini CCM inafanya maamuzi sahihi.

5. Ahadi za CCM kutegemea wafadhili.

Nimekuwa nikifuatilia hizi ahadi. Katika kila ahadi ambayo JK ametaja wafadhili ni pale ambapo mradi husika upo katika hatua fulani ya utekelezaji. Hivyo kama hoja ya kero inajitokeza na utatuzi wake ulishaanza, amekuwa akisema hivyo na hata kutaja chanzo cha fedha ba hapo ndipo swala la wafadhili linapokuja.

Sasa kwa nini siyo CHADEMA?

i) Hulka ya viongozi wake:
Ukiangalia vizuri hulka ya viongozi wa CHADEMA ni watu wanaosukumwa zaidi na visasi bila kujali athari katika jamii. Hii inadhihirishwa na ahadi kubwa ya kuwashughulikia watu fulani pindi waingiapo madarakani. Hawatuelezi kuwa nchi hii ina sheria na tutahakikisha utawala wa sheria. unaweza kudhani kuwa unaweza kumshughulikia mtu kwa jambo fulani kumbe sheria haikuruhusu.

Mfano unaposema ntafuta mikataba yote, unasahau kuwa hilo si jambo la upande mmoja. Lazima sheria husika zifuatwe. Kinyume chake unajipalia makaa mabaya zaidi.

2. Kutojali Sheria kwa viongozi.
Hoja yangu hapo juu inathibitisha kuwa viongozi wa CHADEMA hawaheshimu au wanajiandaa kutoheshimu sheria zilizopo ili kukudhi haja zao. Mfano halisi ni hili sakata la Dr Slaa na mke wa mtu. Hakuna aliye msafi sisi sote ni watenda dhambi. Lakini je tunamchukuliaje mtu ambaye hata baada ya kuambiwa hicho si sawa, unaamua kusema potelea mbali tutapambana mbele kwa mbele. Watu wa hivi ni hatari sana. Mara nyingi hufanya maamuzi ya kufurahisha bila kujali athari za kisheria. Idi Amin ni mfano hai. Yeye kwa kutaka umaarufu alifukuza wahindi na kuamuru wazungu wambebe bila kujali sheria zilizopo. Matokeo wote tunayafahamu.

3.Viongozi kutokuwa makini.

Hoja za Slaa kuwa anaweza kushusha cement hadi 5,000 wakati wastani wa gharama za usafiri ni karibu 6,000 bila kujali gharama za uzalishaji ni mfano wa kukosa umakini katika kujenga hoja.

Hata lile sakata la kusema matundu manne yamegharimu 700m wakati ni laki saba ni dalili ya kukosa umakini. Katika hali ya kawaida mtu ulipaswa kujiuliza mara mbili maana hata kama ni ufisadi unabidi ujiridhishe. Kwa hiyo aidha siyo makini au ni viongozi wanaopenda umaarufu.
 
Hata lile sakata la kusema matundu manne yamegharimu 700m wakati ni laki saba ni dalili ya kukosa umakini. Katika hali ya kawaida mtu ulipaswa kujiuliza mara mbili maana hata kama ni ufisadi unabidi ujiridhishe. Kwa hiyo aidha siyo makini au ni viongozi wanaopenda umaarufu.

Haiwezekani hata MKANDARASI HUWE WEWE MWENYEWE HUWEZI CHIMBA NA KUJENGA MATUNDU 4/8 YA CHOO KWA LAKI 7. wachakutufanya sisi atujuhi ujenzi.
 
Mwanakijiji,

Baada ya kukisoma hicho kijalida ulichoambatanisha humu, naomba nitofautiane na wewe kama ifuatavyo.

1. Je Slaa (au CHADEMA) ni chaguo sahihi?

Kabla ya kutoa msimamo wangu, naomba nikukumbushe kuwa kiasi cha miezi miwili nyuma ulitoa mada humu ambapo ulitoa mawazo yako kuwa CHADEMA si chama sahihi kwa sasa na hata ulitoa tofauti ya Chama cha upinzani na Chama cha uongozi. Kama sikosei hitimisho lako lilikuwa kuwa CHADEMA si chama muafaka kwa sasa. Kama nimekunukuu vibaya ni bahati mbaya lakini hoja zangu hapa chini zinalenga kujenga msimamo wangu.

2. Slaa na viongozi CHADEMA kuandamwa
Umezungumzia kuandamwa kwa Dr Slaa. Sijui lengo ni nini lakini ukumbuke hiyo ndio siasa. Kwani mbona Kikwete na CCM wanaandamwa sana na hata humu JF hilo ni la kawaida. Sasa kuandamwa kwa Slaa au CHADEMA kuna jambo gani la ajabu?

3. Tofauti ya Slaa na Kikwete
Unatwambia kuwa Slaa ni bora kwa sababu anazungumzia mabadiliko (kuanza upya) wakati Kikwete anazungumzia maboresho.
Naomba nikukumbushe kuwa Kikwete anawakilisha chama kilichopo madarakani na ambacho sera zake ndizo zinatumika kwa sasa. Kwa hiyo yeye hawezi kuzungumzia kuanza upya kwa sababu tayari wana msingi wa sere zao. Kuanza upya kwao inawezekana tu kama sera fulani imethibitika na wao wenyewe kuwa imefeli. Kama hawajakiri hicho unategemeaje azungumzie kuanza upya. Jambo la kuzingatia ni kama mhusika anaona mapungufu na ameandaa maboresho. Hilo hata jarida lako ninakiri kuwa lipo. Kwa CCM kuzungumzia kuanza upya ni sababu tosha ya kuwabadilisha maana watakuwa wanafanya majaribio.

4. Sera za CCM zinajali uwingi

Hapa naelewa kuwa kuwa na vitu vingi ambavyo havikidhi viwango ni sawa na sifuri. Mh. Mkapa aliwahi kulizungumza hili na hasa katika elimu. Yeye alihoji, lipi bora tuanza na shule ambazo hata kama hazikidhi hivyo viwango ili tuendelee kuziboresha au tusubiri mpaka pale tunapokuwa na uwezo wa kutimiza hivyo vigezo ndio tuanze? Swali likaja, ni nani ambaye yuko tayari mtoto wake asubiri asipate elimu hadi hapo tutakapokuwa na uwezo wa kufanya hivyo? Jibu hakuna. Kwa hali hiyo, the only option ni kuwa na shule, hospitali na huduma zingine kila mahali na huku tukiendelea kuziboresha. Kwa hili sioni mbadala bado naamini CCM inafanya maamuzi sahihi.

5. Ahadi za CCM kutegemea wafadhili.

Nimekuwa nikifuatilia hizi ahadi. Katika kila ahadi ambayo JK ametaja wafadhili ni pale ambapo mradi husika upo katika hatua fulani ya utekelezaji. Hivyo kama hoja ya kero inajitokeza na utatuzi wake ulishaanza, amekuwa akisema hivyo na hata kutaja chanzo cha fedha ba hapo ndipo swala la wafadhili linapokuja.

Sasa kwa nini siyo CHADEMA?

i) Hulka ya viongozi wake:
Ukiangalia vizuri hulka ya viongozi wa CHADEMA ni watu wanaosukumwa zaidi na visasi bila kujali athari katika jamii. Hii inadhihirishwa na ahadi kubwa ya kuwashughulikia watu fulani pindi waingiapo madarakani. Hawatuelezi kuwa nchi hii ina sheria na tutahakikisha utawala wa sheria. unaweza kudhani kuwa unaweza kumshughulikia mtu kwa jambo fulani kumbe sheria haikuruhusu.

Mfano unaposema ntafuta mikataba yote, unasahau kuwa hilo si jambo la upande mmoja. Lazima sheria husika zifuatwe. Kinyume chake unajipalia makaa mabaya zaidi.

2. Kutojali Sheria kwa viongozi.
Hoja yangu hapo juu inathibitisha kuwa viongozi wa CHADEMA hawaheshimu au wanajiandaa kutoheshimu sheria zilizopo ili kukudhi haja zao. Mfano halisi ni hili sakata la Dr Slaa na mke wa mtu. Hakuna aliye msafi sisi sote ni watenda dhambi. Lakini je tunamchukuliaje mtu ambaye hata baada ya kuambiwa hicho si sawa, unaamua kusema potelea mbali tutapambana mbele kwa mbele. Watu wa hivi ni hatari sana. Mara nyingi hufanya maamuzi ya kufurahisha bila kujali athari za kisheria. Idi Amin ni mfano hai. Yeye kwa kutaka umaarufu alifukuza wahindi na kuamuru wazungu wambebe bila kujali sheria zilizopo. Matokeo wote tunayafahamu.

3.Viongozi kutokuwa makini.

Hoja za Slaa kuwa anaweza kushusha cement hadi 5,000 wakati wastani wa gharama za usafiri ni karibu 6,000 bila kujali gharama za uzalishaji ni mfano wa kukosa umakini katika kujenga hoja.

Hata lile sakata la kusema matundu manne yamegharimu 700m wakati ni laki saba ni dalili ya kukosa umakini. Katika hali ya kawaida mtu ulipaswa kujiuliza mara mbili maana hata kama ni ufisadi unabidi ujiridhishe. Kwa hiyo aidha siyo makini au ni viongozi wanaopenda umaarufu.

The Following User Says Thank You to The Good For This Useful Post:
Ama (Today)

ONLY AMA!!! stay blessed!!
 
Back
Top Bottom