CDM Kuongoza Nchi 2015

Noboka

JF-Expert Member
Nov 12, 2011
1,246
626
Kwa jinsi nilivyoaangalia kipindi cha wabunge kuchangia jana taarifa za fedha za mashirika ya umma, kwa michango waliyotoa wabunge bila kujali itikadi za vyama vyao, CDM mna kila sababu ya kuongoza nchi 2015 kama mkijipanga vizuri.
Mh. Zambi, Ester Bulaya, Selukamba, Kessy, kaboyonga n.k unaona kabisa wamekataa tamaa. Waliyoeleza jana unawaona kabisa hawana amani ndani ya mioyo yao, lakini CCM yao ndiyo iko ICU.
Kama walivyosema jana kwamba waende kujifungia kama wabunge wa CCM ili warudi na maamuzi magumu kuhusu mawaziri, kama wakishindwa kuwawajibisha(Rais ameshadhihirisha kuwa hawezi), basi CDM hiyo tena ni kete kwenu kwani tunajua kabisa wenye uwezo wa kupitisha maamuzi magumu ni wabunge wa CCM na jana wamesema hawaweze kusemea bungeni kweupe wataenda kukutana, sasa tunasubiri!
 
Back
Top Bottom