NYAMKANG'ILI
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 223
- 112
Prof Shivji aliwahi kusema nguzo za KATIBA TANZANIA, na hivyo nguzo za utawala wa CCM ni: (1) chama kimoja CCM; (2) MUUNGANO TZ na ZANZ; na (3) urais wa kifalme (imperial presidency). HAYA yalikuwa ya kale, yaliwahi kuwapo na zilikuwa nguzo za kweli za CCM.
Kwa sasa nguzo za CCM za kuvunja ili kuingia ikulu CDM ni hizi: (1) urais wa kifalme ambao umempatia RAIS mamalaka makubwa ya uteuzi wa watu lukuki ktk nafasi za madaraka, huu umefanya watendaji wa serikali wasitumikie wananchi na nchi kwa ujumla wake na badala yake wanatumikia RAIS, na kwa kuwa RAIS ni m/kiti wa CCM basi wanatumikia CCM badala ya kutumikia wananchi. Watu wanajipendekeza ili wateuliwe au wasiondolewe kwenye nafasi walizopewa; (2) ufisadi kama wa EPA, MEREMETA, DEEPGREEN nk ambao unaipatia CCM pesa chafu za kufanyia siasa ambazo vyama vingine havina. Mfumo wa ufisadi unatumiwa sana kukandamiza wapinzani kwani CCM inawaambia watumishi kuwa iwapo kitatoka madarakani CDM kitawanyang'anya mali zote walizopata kupitia ufisadi, kinawatia hofu ya mabadiliko na kuahidi kuwalinda na mali zao za wizi; (3) vyombo vya habari ambavyo vingi vinamilikiwa na mafisadi wa CCM, vyombo hivi vinatumika kuhakikisha hakuna ajenda ya maana inayopita na kuwafikia wananchi; NA (4) vyombo vya mabavu kama polisi, TISS, PCCB na JWTZ ambavyo makamanda wake wote ni CCM damu na baada ya kustaafu wanakwenda kugombea ubunge kupitia CCM, na wengine hata wanagombea wakiwa bado kazini mfano mzuri ni maafisa wa PCCB 5 waliogombea ubunge 2010 kupitia CCM na mmoja wao aligombea (kura za maoni CCM) jimbo la mzee MZINDAKAYA na waliposhindwa walirudi kazini, hawa wanapambana kuhakikisha CCM inabaki. Kamati ya MKAMA iliyochunguza kwa nini CCM ilipata matokeo mabaya uchaguzi 2010, pamoja na mambo mengine, iliinyoshea kidole PCCB kwamba ni moja ya sababu ikidai kuwa inakamata watu wao na kuitangaza CCM kuwa ni ya mafisadi, hii inajibu swali kwa nini mwaka huu 2012 kwenye chaguzi za CCM zinazoendelea PCCB haijaonekana mpaka sasa, inatii maelekezo ya CCM.
Kwa sasa nguzo za CCM za kuvunja ili kuingia ikulu CDM ni hizi: (1) urais wa kifalme ambao umempatia RAIS mamalaka makubwa ya uteuzi wa watu lukuki ktk nafasi za madaraka, huu umefanya watendaji wa serikali wasitumikie wananchi na nchi kwa ujumla wake na badala yake wanatumikia RAIS, na kwa kuwa RAIS ni m/kiti wa CCM basi wanatumikia CCM badala ya kutumikia wananchi. Watu wanajipendekeza ili wateuliwe au wasiondolewe kwenye nafasi walizopewa; (2) ufisadi kama wa EPA, MEREMETA, DEEPGREEN nk ambao unaipatia CCM pesa chafu za kufanyia siasa ambazo vyama vingine havina. Mfumo wa ufisadi unatumiwa sana kukandamiza wapinzani kwani CCM inawaambia watumishi kuwa iwapo kitatoka madarakani CDM kitawanyang'anya mali zote walizopata kupitia ufisadi, kinawatia hofu ya mabadiliko na kuahidi kuwalinda na mali zao za wizi; (3) vyombo vya habari ambavyo vingi vinamilikiwa na mafisadi wa CCM, vyombo hivi vinatumika kuhakikisha hakuna ajenda ya maana inayopita na kuwafikia wananchi; NA (4) vyombo vya mabavu kama polisi, TISS, PCCB na JWTZ ambavyo makamanda wake wote ni CCM damu na baada ya kustaafu wanakwenda kugombea ubunge kupitia CCM, na wengine hata wanagombea wakiwa bado kazini mfano mzuri ni maafisa wa PCCB 5 waliogombea ubunge 2010 kupitia CCM na mmoja wao aligombea (kura za maoni CCM) jimbo la mzee MZINDAKAYA na waliposhindwa walirudi kazini, hawa wanapambana kuhakikisha CCM inabaki. Kamati ya MKAMA iliyochunguza kwa nini CCM ilipata matokeo mabaya uchaguzi 2010, pamoja na mambo mengine, iliinyoshea kidole PCCB kwamba ni moja ya sababu ikidai kuwa inakamata watu wao na kuitangaza CCM kuwa ni ya mafisadi, hii inajibu swali kwa nini mwaka huu 2012 kwenye chaguzi za CCM zinazoendelea PCCB haijaonekana mpaka sasa, inatii maelekezo ya CCM.