CCtv za ma bank yetu humu nchini hazitunzi picha

Jethro

JF-Expert Member
Mar 23, 2009
2,219
370
Wana JF,

Katika safari zangu huko kasikazini mwa tanzania na huku kanda ya ziwa nilikuja kutana na matatizo katika Bank zetu hizi na nikagundua kwa silimia fulani hizo camera walizo zifunga ndani ya ma Bank zina urakini wa ku record data au niseme "daily activities "

Kwa wengeine wanaweza dhani ni utani au kuto amini ila nasema haya kwa matukio niliyo kutana nayo,

Tukio la kwanza katika moja ya Bank huko kasikazini wakati natoa pesa kwa ATM hazikutoka na kesho yake nikaingia Bank ndani kuhoji kulikoni? wakaniambia pesa ilitoka "kwa jinsi system yao inavyosema" me nikwaomba tu tukague kwa kuangalia CCTV waka sema ooh bro tutacheck then tutakujurisha na jioni yake nilipo pita kwa ATM nikakuta pesa na nikazitoa vyema tuu.

Tukio la Pili ni huku kanda ziwa Rafiki yangu alichukua pesa na mtoa pesa akadhani alimzidishi na alipo itwa kwa mahojiano yeye akawaambia tupitie CCTV tuone ukweli halisi maana yeye alisema hakuzidishiwa napo wakapiga chenga ila uzuri kumbe ni mteja wao mzuri tu alizidishiwa pesa that day na akazirudisha,

Katika hali hii ni jinsi gani inavyo onyesha kuna uzembe mkubwa kuanzia makao makuu Dar hizi Bank za mikoani zina puuziwa sana na ndizo zina wateja wengi pia kufanya Bank zetu kuendelea kutupa huduma lakini kama inafika mahali wanapuuzi hadi CCTV hazi wezi kusave daily activities duuu hii ni hatari sana.

My Take;


Police wawe na kikosi au Kitengo maarumu cha kukagua CCTV za kwenye Ma bank au maeneo husika kwa watu walio weka CCTV wajiandikishe ili kukitokea kitu kuwe na upelelezi wa kitaalamu utumike sio police wabahatishe tuu kazi ya kuchunguza.
--"Au Kampuni fulani ipewe nguvu kisheria kusimamia na kudhibiti wale wote walio funga CCTV nchi kama UK mfumo huo upo kuweka CCTV lazima kuji register kuwa una mfumo wa CCTV kwako au kwenye kiwanda chako au biashaza zako"

Makao makuu"ALL BANKS HQ" ni umefika muda sasa wa kuchukua action na kuwajibika kwa Bank za mikoani na sio kukaaa Dar na kula viyoyozi, Future Action plan zenu na Budget zenu kweli zina timilizika au ni mboyoyo nanyi mumeingiliwa na jinamizi la ahadi za kisiasa?

Ma branch Manager wengi wa ma Bank zetu huko mikoani nao wamebweteka sana na hivyo vyeo vyao wawe makini huwezi kweli ukakaa tu bila kujua CCTV ina record au hai record ndani ya branch yako.

Karibuni mchangie hoja

Thanks
 
Michuzi anakwambia bongo tambalare yani bongo mambo yanajiendea tu fresh hakuna anayejari. Au anakwambia Yale yaleeeeeeeee kwamba hatujifunzi kutokana na matatizo tunayokutana nao
 
Nahisi kama mchezo mchafu wa ma IT wa benki vile ili waweze kutuibia,sijui lakini napita tu!
 
Nahisi kama mchezo mchafu wa ma IT wa benki vile ili waweze kutuibia,sijui lakini napita tu!

Mkuu,

kwanza nakupa tu taarifa Ban zetu nyingi ajira zote hutokea HQ-Dar na tatizo kubwa kabisa kwa Bank Zote ni kushindwa kabisa nio jinsi gani ya kuendesha kitengo cha ICT a.k.a "IT" Department , IT wote huajiriwa na kubakia Dar HQ period na hii sio tu kwa Ma Bank hata TRA the good example na ndio maaana kuna uozo mkubwa sana.

Kwahiyo kwa point yao kuna asilimia fulani kuna ukweli haiwezekani Bank kama NBC iwe na IT Department Dar HQ na ndio wanweze ku control Branch zote na ndio maana kuna wizi mwepesi wa kuchukuwa pesa online.

Wanao Install CCTV hupitishwa ki deal tenda ya fulani inapitishwa na wana penda sana vitu cheap kweli kweli na wanavipandisha bei kweli. Bank zetu kweli zinashindwa kuwa na Data Storage kweli at least after 6month mnaamisha record kwingine kuna bakiwa na space kazi ya ku record inaendelea.

My Take;
Security yetu humu nchini kwakweli ina uzembe mkubwa sana hata kutoa ushauri haiwezi imekaaa tu kupeleka umbea tuuu wa siasa vitu muhimu kama Bank zetu kuwa kwenye usalama wala hawajishughurishi kabisaaaa


 


Mkuu,

kwanza nakupa tu taarifa Ban zetu nyingi ajira zote hutokea HQ-Dar na tatizo kubwa kabisa kwa Bank Zote ni kushindwa kabisa nio jinsi gani ya kuendesha kitengo cha ICT a.k.a "IT" Department , IT wote huajiriwa na kubakia Dar HQ period na hii sio tu kwa Ma Bank hata TRA the good example na ndio maaana kuna uozo mkubwa sana.

Kwahiyo kwa point yao kuna asilimia fulani kuna ukweli haiwezekani Bank kama NBC iwe na IT Department Dar HQ na ndio wanweze ku control Branch zote na ndio maana kuna wizi mwepesi wa kuchukuwa pesa online.

Wanao Install CCTV hupitishwa ki deal tenda ya fulani inapitishwa na wana penda sana vitu cheap kweli kweli na wanavipandisha bei kweli. Bank zetu kweli zinashindwa kuwa na Data Storage kweli at least after 6month mnaamisha record kwingine kuna bakiwa na space kazi ya ku record inaendelea.

My Take;
Security yetu humu nchini kwakweli ina uzembe mkubwa sana hata kutoa ushauri haiwezi imekaaa tu kupeleka umbea tuuu wa siasa vitu muhimu kama Bank zetu kuwa kwenye usalama wala hawajishughurishi kabisaaaa


Nimekusoma,mkuu! Kuna ile benki inayoitwa ya MAKABWELA,yaani hawa jamaa wakata hela vibaya mno kwenye ATM zao,we acha tu.Nafikiria kuweka akiba ndani maana benki wizi mtupu!
 
hili ninaliunganisha na wizi unaofanyika na baadhi ya wafanyakazi wa bank hizi za kwetu,,, unaweka pesa kwenye akaunti then unakuta hazipo kwenye akaunti yakoo,,, nakuunga mkono kuwa system za cctv ni mbovu na ni kweli nyingi hazifanyi kazi
 
camera wameweka kama tishatoto tu usishangae kukuta mwezi mzima hazikuwa zikifanya kazi
 
Back
Top Bottom