CCM’s svengali hold

Umeanalyse too brief but very brilliant arguments bro [emoji41] you never let me down as always and usual. Hakuna nyumbu alie too critical atakae eza kustand against those points narrated above, period.
Mara ya Kwanza nilipousikia wimbo wa 2pac WA 'how long will they mourn me' nikasema kwangu Mimi sijui km utatokea wimbo mwingine nitakaoupenda zaidi ya huo. Kabla sijakaa vizuri, dmx (r.i.p) akaachia Ile kitu 'who we be'. Nikajikuta najishangaa Kwa maneno yangu.

Ni vigumu kupangua hoja za nyani ngabu, lkn tusihitimishe hivyo haraka haraka tu......
 
Yaliyoongelewa kabla ya kutoka ,hakuna anayejua na kwa akili yangu ya Kinyakyusa najua hakwenda mwenyewe, bali alipelekwa ili yule mkuu aliyetoa shutuma BBC ajisafishe kwenye uso wa mabeberu
 
Hawa vijana wa shule za kata hawajui nguvu ya mazungumzo/kukaa meza moja.
Kwa mifano hiyo hapo juu uliyowatolea kwa ufupi,naamini hawataelewa chochote.
Kongole.
 
Kuna watu wanaandika upumbavu mpaka basi.
Mimi ni mhanga wa "umafia wa kidola" wa kuvamiwa kwa duka la kubadilisha fedha za kigeni.
Kuna wafanyabiashara wengi ambao tumekuwa wahanga wa uovu wa kidola wa mwendazake.
Watu wanaandika tu kwa kuwa hawajakumbwa na hayo mambo.
Katiba mpya ni suluhisho.
 
Sema unautetea Uislamu tu, hayo mengine yoote mbwembwe tu!
Argumentum ad hominem?!!!

😳😳Dini ya mtu inaingiaje katika maslahi kuntu ya nchi ?!!!

Taifa kwanza kabla ya hizo imani zilizoletwa....

Wewe unaitetea dini gani na kuliweka taifa nyuma?!!!
 
Kwa saa 24 nilitafakari nikidhani kuna kitu sielewi, baada ya kuliona bandiko wasi wasi umenitoka.

1. Wanopinga hoja za Nyani Ngabu sizioni hoja zao.
Kusema ana chuki tu bila kujibu hoja ni kukosa hoja.

2. Mbowe (FAM) hakupaswa kwenda Ikulu jana.
Sababu alizotoa NN ni za kweli na naongezea, kwamba, Mbowe aliomba kuonana na Rais SSH kabla ya kukamatwa ,barua haikuwahi kujibiwa.

Ni kwa mantiki gani anakwenda Ikulu kabla ya kuonana na waliompigania akiwa gerezani!

3. Kuna hoja kwamba '' watu walitaka FAM afanye nini''. Well, hakutakiwa kwenda Ikulu katika muda mfupi bila kujua mazingira ya nchi. Sijui kama alikutana na kamati kuu ya CDM.

4. ''Kwamba Mbowe hataki kulipa kisasi'' hakuna anayemtaka alipe kisasi, kujipa muda wa kutathmini si kulipa kisasi ni kujijenga kifikra baada ya mateso ya miezi 8.

5. Kwamba ''alijipa muda na kwenda nyumbani'', si kweli , aliwaambia watu hataongea hadi muda utakapofika, ilikuwaje muda wa kuonana na Rais SSH ulipatikana?

Kwa waliofuatilia kesi, kulikuwa na 'presha' kutoka ndani na nje ya nchi.
Mahakama ilikuwa ma wakati mgumu achilia mbali ilivyovurunda mwenendo wa kesi.

Rais SSH kukutana na viongozi wa dini ilikuwa njia tu ya 'kutokea''

Kwa hali yoyote CDM na Mbowe walikuwa na 'upper hand''. CCM, wakati mgumu.

Mbinu iliyotumiwa na CCM inamwacha FAM na swali '' kwanini alikwenda''

Rais SSH alijua Mbowe naungwa mkono, kitendo cha kutoka tu kinatosha kuongeza ari ya Chadema na Wananchi kudai haki ikiwemo katiba. FAM alikuwa na ''leverage' na ni wazi ame squander

Mbinu iliyotumiwa kwa Masheikh wakitoka wakae kimya haikufanya kazi kwa Mbowe.

Mbinu mpya ni kumwita 'kumtia adabu'' tunaweza kukuweka ndani na kukutoa!
Je hilo mnaliona sawa?

Mbinu ya kupiga picha na kutoa hotuba za maridhiano ni ''kumfunga Mbowe mdomo'' .

Mbinu ya kumwita ni kumlazimisha 'akiri kwamba amesamehewa''

Ukitaka kujua mbinu ya 'kusamehewa' imetumikaje, siku Mbowe anakwenda Ikulu ni siku hiyo hiyo vijana wa JKT wanasamehewa. Kwa maana kwamba Rais SSH ni mtu wa kusamehe.

Je, Mbowe alihitaji kusamehewa? Kwa kosa gani? Lilithibitishwa wapi? Je alipewa kujitetea?

CCM wanasema hizo ndizo siasa safi! kwamba wanamwambia Mbowe atulie , siasa chafu zitamrudisha kule, si ugaidi ni siasa ! hilo ndilo Mbowe alitesekea?

Kwa namna yoyote ile Chadema na uongozi chini ya Tundu Lissu wana la kueleza Wanachama wao likuwaje wakamwacha ''mfungwa'' akakimbilia Ikulu bila kumpa taarifa za chama na bila kumpa muda wa kutafakari!!!

''Mashtaka ya NN'' yana mashiko! kuna ''hoja za kujibu''

JokaKuu Pascal Mayalla
 
Hakuna adhabu kubwa kwa mkosaji kama msamaha.
 
Mkosaji ni nani hapa?
Nafsi ya hatia haiwezi kutulia mpaka angalau isikie NENO toka kwa aliyekosewa. Mwanamke akifumaniwa na mumewe na mume asichukue hatua yoyote, yaani ajifanye kama hakuna kilichotokea, hutamani hata apigwe au afokewe kwa kosa lingine. Mbowe kauweza sana huu mchezo, natoka gerezani na wewe ndo uliyenipeleka gerezani lakini nakusalimia tu katika jina la Yesu!! Mtu katoka Dodoma kwenda Dar kupata angalau NENO tu la mfungwa wa michongo mnaona ni jambo dogo hilo?
 
Hivi ulitaka Mbowe aanzishe maandamano baada ya kuachiwa?
Are you serious?
 
Umeanalyse too brief but very brilliant arguments bro [emoji41] you never let me down as always and usual. Hakuna nyumbu alie too critical atakae eza kustand against those points narrated above, period.
Analysis is parochial and addresses the simpletons way of thinking.
 
Teh teh haya maajabu yako Tanzania pekee yake tu.
 
Kwa namna yoyote ile Chadema na uongozi chini ya Tundu Lissu wana la kueleza Wanachama wao likuwaje wakamwacha ''mfungwa'' akakimbilia Ikulu bila kumpa taarifa za chama na bila kumpa muda wa kutafakari!!!
Inasemekana alialikwa kwenda huko na mweny nchi ?
 
Hata kama inaenda mrama, wapinzani are not capitalizing on it!

Very disappointing.
Watu wamechoshwa na hizi komedi za siasa!

Wapinzani hakuna bongo! Ni matawi madogo ya CCM, binafsi naamini hivyo!
Wote wachumia tumbo! Hakuna mwenye kuwaza masuala taifa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…