CCM yaunga mkono Maridhiano ya kisiasa

CCM yaunga mkono Maridhiano ya kisiasa

.. Hii style alikuwa anaitumia zaidi JK. Iko hivi wameona hakuna haja ya kuangaika na watu wasio na madhara,sana sana ni kuleta attention kwa wafadhili wazungu bila sababu ya msingi. Hii style ilitumika sana kipindi cha JK. Na watakaofaidi hayo mnayoyaita maridhiano ni Mbowe na waliomzunguka.. FULL STOP. Ila mwananchi wa Tandahimba na Nyangulukulu mfuasi wa CHADEMA hayatamuhusu hata kidogo. Ukitaka kuamini hilo,hata akina Mdee watakaa bungeni hadi 2025 na story ya katiba mpya ndo imefika mwisho. Hakuna mkate mgumu mbele ya chai, ila mwisho wa movie watakaoathirika kisaikolojia ni wafuasi wa vyama wanaochukulia siasa kama ushabiki wa Simba na Yanga.

Suala la akina Mdee chadema walishalimaliza, Ni wao wanaitumia mahakama na kwa msaada wa spika kuendelea kukaa bungeni kinyume Cha sheria.
 
Mtu anayevunja sheria makusudi halafu mpaka leo bado analeta hadithi za sungura na fisi badala ya kufuata sheria siwezi kumuamini kamwe.
 
Hii ni mbinu ya ngapi maana wanazo zaidi ya 1000

Shida mnaipa CCM sifa isizo kuwa nazo. Wangekuwa na mbinu wasingekubali kuharibu uchaguzi wa 2020 na 2019. Wangekuwa na hizo mbinu wasingekubali wankopa kwa mabeberu. CCM ilishaishiwa ipo kwasababu sheria na vyombo vya ulinzi vinaipendelea.
 
Shida mnaipa CCM sifa isizo kuwa nazo. Wangekuwa na mbinu wasingekubali kuharibu uchaguzi wa 2020 na 2019. Wangekuwa na hizo mbinu wasingekubali wankopa kwa mabeberu. CCM ilishaishiwa ipo kwasababu sheria na vyombo vya ulinzi vinaipendelea.
Wangekuwa na mbinu hizo Jiwe asingeongoza nchi
 
2015, CCM waligeuka Mwafaka wao na CUF. Maalim alipomshinda Shein kwenye sanduku la kura, wakafuta matokeo ya uchaguzi. Huu mwafaka wa CHADEMA na CCM utakuwaje tofauti? Hili ni swali ambalo kila anayeifahamu CCM vizuri anajiuliza.
Huo ni muafaka wa Mbowe na Ccm, hivyo mnufaika ni Mbowe maana ataanza kulamba asali.
Tindo JokaKuu
 
Hahaaaa....CHADEMA imebaaanaaa,imeachia. Mbowe alishasoma upepo kwamba kupitia kwa mama Samia atapata Mali zake zilizopotea. Amekuja na gear ya maridhiano ya kisiasa.

Jiulize kwani Kuna tatizo miongoni mwa watanzania. Hayo maridhiano ni baina yake na serikali wala sio kwa niaba ya watanzania.
#hatamboweamelambaasali

Mazungumzo sio ya mbowe elewa. Haya ni mazungumzo Kati ya Mwenyekiti wa CCM na viongozi wa CHADEMA. Kuna hadidu za rejea za mazungumzo. Usidhani Ni mazungumzo ya kijiweni tu.

Chadema imetoka mbali, kutoka kupambana na mihimili mitatu mpaka kwenye meza ya mazungumzo sio Jambo dogo.
 
.. Hii style alikuwa anaitumia zaidi JK. Iko hivi wameona hakuna haja ya kuangaika na watu wasio na madhara,sana sana ni kuleta attention kwa wafadhili wazungu bila sababu ya msingi. Hii style ilitumika sana kipindi cha JK. Na watakaofaidi hayo mnayoyaita maridhiano ni Mbowe na waliomzunguka.. FULL STOP. Ila mwananchi wa Tandahimba na Nyangulukulu mfuasi wa CHADEMA hayatamuhusu hata kidogo. Ukitaka kuamini hilo,hata akina Mdee watakaa bungeni hadi 2025 na story ya katiba mpya ndo imefika mwisho. Hakuna mkate mgumu mbele ya chai, ila mwisho wa movie watakaoathirika kisaikolojia ni wafuasi wa vyama wanaochukulia siasa kama ushabiki wa Simba na Yanga.

Sina tatizo na mashaka yako kwani hata mimi nina mashaka na haya mazungumzo, ili haya ndio matamanio yako, na hasa ukizingatia ww ni mfaidika wa siasa chafu ndani ya nchi hii.
 
Sahau,acheni mahakama ifanye kazi.Maridhiano siyokuingilia mihimili mingine
Hakuna mahakama, bali kuna majengo ya mahakama yanayoendeshwa na makada wa CCM, na kazi yao ni kutumika na watawala wa CCM kukomoa washindani wao kisiasa.
 
Kuweni makini... ccm na wanachama wake akina Paskali hawaridhishwi na kinachoendelea!

Kabisa maana wanajua dhalimu atazidi kudharauliwa kwa siasa zake za kihayawani. Wanataka mtu afanye kama yeye ili ionekane style ile ndio sahihi ya utawala. Sasa wakiona kinyume chake haiwalipi.
 
Back
Top Bottom