DJ CHOKA FREDY
Member
- Apr 9, 2011
- 38
- 3
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Tanga kimewashukia viongozi wake waliohamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kusema kuwa ni waroho wa madaraka.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara katibu wa chama hicho Khalid Rashid, amemponda aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Tanga, Mohamed Waziri Kinomina na wenzake waliokihama chama hicho na kuhamia CCM.
Kadhalika amewaponda kwa kudanganya nyadhifa walizokuwa wakishikilia ndani ya chama hicho huku mmoja wao akidai kuwa alikuwa ni mwenezi wa chama hicho Wilaya ya Tanga, ambao hivi karibuni walihama CHADEMA kwa kile walichodai kuwa kimetawaliwa na udini na ukabila.
Katibu huyo alidai kuwa mwenyekiti huyo wa zamani wa CHADEMA wa Wilaya ya Tanga, Kinomi na wenzake, Aufi Kidege ni waroho wa madaraka na kamwe CHADEMA haitakubali kukumbatia watu ambao wanaifuata kwa masilahi yao binafsi badala ya kuangalia matatizo ya wananchi.
CCM wamedanganywa nao wanakubali eti wamepokea vigogo kutoka CHADEMA, nani kigogo? Mohamed Waziri Kinomi kwetu si kitu na tuliliona hilo mapema, anahama kila chama, CCM kama hawajui hakutoka CHADEMA tu alianzia vyama vingine na kote huko anatafuta madaraka tu na si kingine, alisema.
Aliongeza kuwa CHADEMA ipo kwa lengo la kuwatumikia wananchi na si kushughulikia masuala ambayo ni ya kibinafsi.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara katibu wa chama hicho Khalid Rashid, amemponda aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Tanga, Mohamed Waziri Kinomina na wenzake waliokihama chama hicho na kuhamia CCM.
Kadhalika amewaponda kwa kudanganya nyadhifa walizokuwa wakishikilia ndani ya chama hicho huku mmoja wao akidai kuwa alikuwa ni mwenezi wa chama hicho Wilaya ya Tanga, ambao hivi karibuni walihama CHADEMA kwa kile walichodai kuwa kimetawaliwa na udini na ukabila.
Katibu huyo alidai kuwa mwenyekiti huyo wa zamani wa CHADEMA wa Wilaya ya Tanga, Kinomi na wenzake, Aufi Kidege ni waroho wa madaraka na kamwe CHADEMA haitakubali kukumbatia watu ambao wanaifuata kwa masilahi yao binafsi badala ya kuangalia matatizo ya wananchi.
CCM wamedanganywa nao wanakubali eti wamepokea vigogo kutoka CHADEMA, nani kigogo? Mohamed Waziri Kinomi kwetu si kitu na tuliliona hilo mapema, anahama kila chama, CCM kama hawajui hakutoka CHADEMA tu alianzia vyama vingine na kote huko anatafuta madaraka tu na si kingine, alisema.
Aliongeza kuwa CHADEMA ipo kwa lengo la kuwatumikia wananchi na si kushughulikia masuala ambayo ni ya kibinafsi.