Nakukubalia respect wa boda. Ila mtego wa Utaifa kwa waislamu ndi Mtego uliwagharimu Waislamu katika nchi hii kwa kiwango kikubwa sana. Tafadhali fuatilia historia ya WATEMI Wailio pigania uhuru, Vita vya MAJI MAJI, TANU, EAMWS, BAKWATA na Julius Kambarage kuandikwa peke yake Katika historia rasmi ya nchi hiii.
Ah mkuu sasa ninyi hao wazee wote walikuwa wapi mpaka Nyerere akaandikwa peke yake kwenye historia rasmi ya nchi hii huoni kwamba madai yako yanawalakini au kutengeneza maswali mengi.?
Karibia mara zote, Waislamu wa nchi hii wamekua wakiweka Utaifa kwanza na Uislamu Baadae. Kinyume chake kimekuwa kwa Viongozi wakirsto na wakirsto waliopewa dhamana katika nchi hii. Mara zote wameweka Ukristo kwanza na Utaifa baadae.
Unaweza kutupa mfano moja wapo kwamba wakristu walitangiliza ukristu mbele na kuacha maslahi ya taifa nyuma?
Tumekuwa tukitoa maelezo mengi sana juu ya hali hiyo katika Munakasha mbalimbali ikiwemo hapa JF. Kwa bahati mbaya sana, kuna baadhi ya Waislamu bado hawajitambui. Wao wameweka Maslahi ya Matumbo yao Kwanza kuliko hata huo utaifa wenyewe. Hivyo Basi hua wanapopata fursa ya kuwekwa kwenye decisions boards, hua ni watu wakuburuzwa tu.
Sasa hapa kama hujitukani nadhani umeamua kuwadhalilisha watu bila kujijua Hapa unatitjibitishia kwamba wale waislam waliokuwa kwenye tume ya Warioba walitanguliza matumbo yao mbele na kusahau maslahi ya uislam bila shaka ndivyo unavyomaanisha.
Kwani katika hilo Bunge la CCM linaendelea ambalo limekosa uhalali wa kisiasa, waislamu hao bado wamo. Alhamdulahi, mwanasheria mkuu wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othaman kesha shtukia dili lao, kaamua kujitoa.
Sidhani kwamba ni sababu za kidini zilizosababisha mwanasheria wa Zanzibar akajitoa bali ni kuchakachuliwa kwa maoni ya wananchi naomba usichanganye vitu hivi.
Pamoja kua temesikia katika vyanzo vya siri kua Wabunge Waislamu wanajipanga kujitoa katika bunge linalo endelea kama Mahakama ya Kadhi haitatambuliwa, kama ambavyo waliamamua katika mikutano ya mabaraza ya kanisa kua kama mahakama ya kadhi ingepitishwa na kamati ya Mheshimiwa Brigedia Hassan Ngwilizi nao wangejitoa.
Mkuu wewe ni mtu mzima kwanini uongee vitu vya kufikirika lini haya madai yako yalitajwa ama kuwekwa wazi? mbona sisi wengine hatujawahi kusikia wewe ulisikiasikia wapi mkuu?
Mimi nadhani hili jambo lazima lijadiliwe kwa kina, faida na hasara zake kwa jamii ya watanzania kabla hali haijakua mbaya.