CCM Yakalia kuti kavu Ukonga

CCM Yakalia kuti kavu Ukonga

Greenwhich

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
1,337
Reaction score
968
Jimbo la Ukonga ni kati ya majimbo ambayo CCM ina hali ngumu sana na hii ni kutokana na maendeleo duni katika jimbo hilo. Mbunge wa Jimbo hilo Eugene Mwaiposa ni kati ya wabunge ambao hawaongei chochote cha kupigania Jimbo lake. Ni mbunge ambaye ameshindwa kufanya mkutano wowote wa hadhara Jimboni kwake kwa aibu ya kuzomewa na kushindwa kujibu kero za wananchi.

Jimbo la Ukonga barabara zake asilimia 90% ni mbovu na hazipitiki kabisa kipindi cha mvua.Kutokana na ubovu wa barabara hizo kipindi cha mvua wananchi wanatozwa mpaka shilingi 1000/- kutoka kituo kimoja hadi kingine. Hali hiyo imekuwa ni kicheko na mbeleko kubwa kwa chama cha CHADEMA. Kwa sasa CHADEMA ndio inashikilia siasa za Ukonga na wamekuwa wakifanya mikutano mfululizo kwenye matawi na Kata. Kunawiri kwa CHADEMA Jimboni Ukonga kunachangiwa pia na viongozi wa chama hicho ngazi ya Jimbo kushirikiana kwa pamoja kuimarisha chama kwa kufanya kazi bila kuchoka.

CHADEMA wamekuwa wakiwaeleza wazi wananchi kwamba mateso yao yanatokana na kuichagua CCM kwenye uchaguzi uliopita. CHADEMA imekuwa ikiwapa mfano wa majimbo ya Ubungo na Kawe yanayoshikiliwa na CHADEMA jinsi wabunge wake wanavyopiga kelele na jinsi kulivyo na maendeleo makubwa katika majimbo yao. Ni ukweli ulio wazi kwa hali ya CCM jimboni Ukonga ni ya kusikitisha sana.Matawi mengi yanafungwa na kugeuzwa kuwa ngome za CHADEMA.

Na endapo hali ikiendelea hivi hivi ni wazi CHADEMA itapata ushindi mkubwa kwenye jimbo hili uchaguzi ujao na idadi kubwa ya madiwani. Wanachpaswa CHADEMA tu ni kuteua wanachama wanaokubalika kugombea nafasi za Ubunge na Udiwani.

Hii ni Tathmini yangu binafsi baada ya kuzunguka kata zote za Ukonga kwa ziara binafsi kwa kipindi cha wiki mbili.
 
Nyie endeleeni kuwafumbua macho tu, acha hivyo mpaka 2015 cdm ilichukue, sasa wewe unaropoka tena, anaweza akasikia akafanya maajabu kwa hii miaka miwili iliyobaki, walio lala usiwaamsheeeeeeeeeeeeeeeeeeeee?????
 
...hii ni tabia ya wabunge wote walioshinda kwa rushwa na uchakachuzi ,hawafikirii wananchi wao...
 
Nyie endeleeni kuwafumbua macho tu, acha hivyo mpaka 2015 cdm ilichukue, sasa wewe unaropoka tena, anaweza akasikia akafanya maajabu kwa hii miaka miwili iliyobaki, walio lala usiwaamsheeeeeeeeeeeeeeeeeeeee?????

Chadema hawafanyi mambo kwa siri bali kwa uwazi na mikutano inayofanywa haifanywi mvunguni mwa kitanda bali majukwaani mbele ya vyombo vya habari.

Ukweli siku zote haufichwi...
 
Mazingira mazuri kwa kamanda Anselim Tryphon Ngaiza aka Soggy Dog Anter aka bichwa kuchukua ubunge.
 
Jerry anajiandaa kugombea Ukonga
 
Jerry anajiandaa kugombea Ukonga

Huyu Jerry si ndiye meya wa Ilala aliyeshindwa hata kutoa greda ya kutengeneza barabara za Ukonga kipindi cha mvua? Ukonga si iko Ilala?

You are Joking! Wananchi wa Ukonga si wapumbavu kiasi hicho.
 
Haya Professor J, Goli hilooo shindwa mwenyewe. Binafsi nataka chadema vijana DSM nzima. Prof nitakupigia debe na kula mtu wetu.
 
Back
Top Bottom