CCM yaitisha Kamati Kuu kwa dharura

CCM yaitisha Kamati Kuu kwa dharura

heshima ya KIKWETE NA CCM YAKE ITAKUMBUKWA DAIMA VIZAZI NA VIZAZI PINDI TU WATAKAPO SIMAMAMIMARA KAMA NYERERE MWAKA 1995 NA KUFUTILIA MBALI MITANDAO YOTE YA WEZI NDANI YA CCM WANAOTUMIA KIVURI CHA CCM KUTAFUTA MADARAKA NA NAFASI ZA KUFANYA BIHASHARA.
 
Jakaya fanya ufanyavo wa Tanzania hawamtaki Mgombea wako, Rafiki yako, Mwanamtandao wa Zamani na mchezaji mwenzako wa Basket ball, Mjeshi mwenzako mstaafu, mteule wako alieongoza moja ya mihimili ya serikali,Iache Demokrasia ichukue mkondo wake.

Ambaye Ni Mr. Parkinsons Disease EL.
 
Hiyo CC 'maalum' itakuwa imeitishwa kwa dharura baada ya kuona 'spidi' ya mzee wa mamvi katika safari yake ya matumaini haidhibitiki.

Kwa hiyo wanatafuta 'mwoarobaini' ya namna ya kuli-delete jina lake.

Watumie tiketi ya ufisadi kukata jina lake..
 
Ungaunga mwana ,chama hakina staha tena,CCM wamevaa nguo lkn ni transparent...hii ni tia maji tia maji...Maji lita 50 unga robo kilo..
 
Kufuatia kupanda kwa joto la kumsaka mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia CCM na songombingo la Zanzibar, Kamati Kuu ya CCM (CC) imeitishwa kwa dharura. Nyaraka za kikao hicho zinaonesha kuwa CC itajadili songombingo la Zanzibar na kuanza kupanga nondo za kuchambua na kuchuja watiania wa CCM. Kikao hicho cha dharura kinatazamiwa kuongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete na kitafanyika Dodoma.

Kulingana na taarifa nilizonazo,kikao kitafanyika kesho.CC inagusia pia malalamiko ya rushwa toka kwa watiania waliorejesha fomu. Yametolewa malalamiko lukuki yachomayo kama mkuki hasa juu ya wakati wa kusaka wadhamini mikoani. Ni kutoka kwa watia nia wenyewe. Wapo waliowasilisha nyaraka na shahidi nyinginezo kushuhudia rafu za baadhi ya watiania.JF will be the first to know kitakachojiri kikaoni!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Wanasema eti wewe ni mbea na mnafiki
 
Pia mwenyekiti ataelezea kukerwa kwake na tamko la chama kutangazia uma ushindi wa 'goli la mkono'! Kuna uwezekano mkubwa makondakta akateuliwa kama katibu mpya wa itikadi na uenezi, nawasilisha.
 
Cha ajabu napata taarifa hapa dodoma kama upo nyumba ya wageni na hauhusiki kwenye mkutano unapewa pesa kama ulilipa na kutakiwa kuondoka.
Maana wajumbe na wapambe wa watia nia washalipia guest na hotel zote kwa kipindi cha mkutano.

Makundi yote ya Lowasa kam 4U movement , Friends of Lowasa , Team Lowasa Dar wote walisha book kwenda Dodoma kushinikiza mtu wao apite .Ni mbumbu wale hawajui kuna sheria na kanuni za CCM .Mimi nawambia wamesha mharibia mzee wa Mvi mapema
 
Kikwete na cc yako tumieni mbinu aliyoitumia nyerere mwaka 1995 kuondoa genge la majambazi ndani ya ccm
 
[h=1]CCM yaitisha Kamati Kuu kwa dharura[/h]
11011068_10153396973174339_3192336319760529972_n.jpg

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete (pichani)ameitisha kikao cha dharura cha Kamati Kuu (CC) kitakachofanyika kesho mjini Dodoma, huku ajenda kuu ikiwa ni kupitisha majina ya wagombea nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC), zilizo wazi kutokana na sababu mbalimbali.

Kitengo cha Mawasiliano cha CCM kimethibitisha uwapo wa kikao hicho ambacho pia kitapitia orodha ya makada wa chama hicho wanaowania urais.

Kikao hicho kitatanguliwa na kikao kingine cha sekretarieti kinachofanyika leo ambacho kitaongozwa na Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana.

Mpaka sasa, makada 40 wamejitokeza kuomba nafasi ya kuipeperusha bendera ya CCM katika kiti cha urais, kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, wengi wanaendelea na kazi ya kukusanya wadhamini katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Juzi, wakati akizungumza na Televisheni ya Taifa (TBC), Makamu Mwenyekiti wa CCM - Bara, Philip Mangula aligusia kidogo juu ya wagombea urais na kusema atakayepitishwa hatajiuza mwenyewe, bali atauzwa na chama hicho alichodai kuwa kina wanachama milioni saba nchi nzima.

Chama hicho tawala kinakabiliwa na wakati mgumu wa kupitisha jina la mgombea urais kutokana na idadi kubwa ya waliojitokeza kuwania nafasi hiyo jambo ambalo halikujitokeza wakati wa upitishwaji wa mgombea urais wa chama hicho mwaka 1995 na 2005.

Taarifa kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa huenda kikao hicho kikahudhuriwa na wajumbe wachache kutokana na kuitishwa kwa dharura.

Ilieleza kuwa kuna nafasi zilizo wazi kutokana na sababu mbalimbali, kuanzia ngazi za wilaya mpaka taifa na kwamba lazima zijazwe katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu ili kila mtu atimize wajibu wake.

“Kuna nafasi za makatibu na wenyeviti ambazo ziko wazi kuanzia wilayani mpaka taifa. Kikao hicho kinakwenda kuzibainisha na kisha kuzijaza,” kilieleza chanzo hicho.

Suala jingine litakalojadiliwa katika kikao hicho ni mabadiliko ya uongozi katika nafasi ya Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Uhuru, Joseph Kulangwa ambayo imesababisha mgomo wa wafanyakazi wanaopinga uamuzi huo. Gazeti hilo ni la chama hicho tawala.

Kwa mujibu wa ratiba ya chama hicho, Kamati ya Usalama na Maadili itafanya kikao chake Julai 8 na kufuatiwa na Kamati Kuu Julai 9 ambayo inatarajiwa kuchuja wagombea hao 40 na kupata watano ambao majina yao yatawasilishwa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) itakayofanyika Julai 10 kuchuja wagombea hao na kubaki watatu watakaopigiwa kura na mkutano mkuu kumpata mmoja. Mkutano huo mkuu utafanyika Julai 11 na 12 .

source:CCM yaitisha Kamati Kuu kwa dharura - Kitaifa
 
Kutokana na hali ya wasiwasi uliopo kwa huyu jamaa EL kuhisi hujuma kwa jinsi ambavyo anakaliwa kooni na Makongoro[\COLOR] anajaribu kutumia nguvu siasa za kila aina.
Makundi yote ya Lowasa kam 4U movement , Friends of Lowasa , Team Lowasa Dar wote walisha book kwenda Dodoma kushinikiza mtu wao apite .Ni mbumbu wale hawajui kuna sheria na kanuni za CCM .Mimi nawambia wamesha mharibia mzee wa Mvi mapema
 
kbm

watanzania mwaka huu au uchaguzi huu hatutachagua chama,tutachagua mtu so hilo mlijue kabisaaaaaaaaaa,wakati bado ni mapemaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom