Zanzibar 2020 CCM yaibwaga ACT Wazalendo Jimbo la Konde Pemba

SautiYaMnyonge

JF-Expert Member
May 13, 2018
439
742
Ndugu Shekha Mpemba Fakhi kwa tiketi ya CCM ameibuka mshindi katika uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo la Konde wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba.

Ikumbukwe Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndugu Shaka Hamdu Shaka kupitia taarifa kwa umma aliyoitoa hapo jana alieleza CCM inauhakika wa ushindi katika jimbo hilo na kata mbili zilizofanya uchaguzi hii leo kwa sababu ya aina ya wagombea iliyowasimamisha, aina ya kampeni walizofanya na mapokeo makubwa yenye hamasa yalioneshwa na wapigakura kwao.

Hili ni Jimbo la tatu (Muhambwe, Buhigwe na Konde) CCM kushinda tangu Sekretarieti mpya ya CCM inayoongozwa na komredi Daniel Chongolo ianze majukumu yake. Kizuri zaidi Jimbo la Konde wanalirejesha kutoka upinzani (mikononi mwa ACT-Wazalendo) lilikodumu kwa miaka 15!

#ChamaImara
#SerikaliImara
#KaziIendelee


IMG-20210718-WA0029.jpg
 
  • Kicheko
Reactions: BAK
Mgombea wa CCM katika uchaguzi mdogo wa Ubunge wa Konde, Zanzibar, Sheha Faki ametangazwa mshindi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), uliofanyika Jumapili 18 Julai 2021.

E6mg2t1WQAIRQ5G.jpg
E6mg3W3XMAIeVwJ.jpg
 
Nilisikia vyama 12
Ni vyama vipi hivyo hujitokeza kwenye uchaguzi tu
 
Pemba. Mgombea ubunge wa Jimbo la Konde kupitia ACT Wazalendo, Mohamed Said Issa ametoka ndani ya ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni yanapofanyika majumuisho ya uchaguzi akidai kutokuwa na imani na kitakachotangazwa.

Amefikia hatua hiyo baada ya msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, Yassin Khamis kueleza kwamba kinachofanyika sasa ni kuweka matokeo hayo kwanza kwenye mfumo kabla ya kutangaza mshindi

Ndipo Issa aliamka na kueleza dukuduku lake akisema katika baadhi ya vituo mawakala wake hawakusaini matokeo ya uchaguzi kutokana na taratibu zilizokiukwa

"Mheshimiwa mimi sina imani na matokeo haya, kwasababu mawakala wangu hawakuyasaini kwenye vituo walinyimwa fomu kwahiyo mimi sina sababu ya kuendelea kukaa humu maana siwezi kuamini kinachofanyika hapa," amesema na kuondoka nje

Hata hivyo kabla hajatoka nje, msimamizi wa uchaguzi amemueleza kuwa vituo anavyolalamikia wakala wake kutosaini lakini karatasi zinaonyesha zimesainiwa na mawakala wake.

Hata hivyo Issa aliendelea kupinga mawakala wake kusaini karatasi hizo akidai kama zitakuwa zimesainiwa basi wamesaini watu wengine ambao hawawatambui.

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Konde, Yassin Khamis ametangaza Shekha Fakhi Mpemba kuwa mshindi wa jimbo hilo kwa kupata kura 1796.

Mpemba amewashinda wenzake 11 akifuatiwa na Mohamed Said Issa wa ACT Wazalendo aliyepata kura 1373.

Khamis amesema kura zilizopigwa ni 5050, kura halali ni 5020 na kura 30 zimekataliwa.

 
Chama dola bila vyombo hivi hakiwezi kushinda uchaguzi wowote ule,mabadiliko yatakuja hata kama sio wakati huu wa generation hii ya walalamikaji wa kwenye social networks.
 
Jamaa wanaambiwa kila siku CCM ni ile ile hawataki kusikia, wacha waendelee kutandikwa mpaka wapate akili, wameshapoteza jimbo, wanadhani kuunda serikali ya mseto na CCM ndio watalegezewa, siku zote CCM kwenye maslahi yao hawana urafiki na yeyote, namshauri Zitto aendelee kumsifia mama kwa hii kazi nzuri anayowafanyia.
 
Back
Top Bottom