Uongozi wa juu wa Sasa wa CCM umesheheni makada toka pande tajwa hapo juu.
Kanda ya Ziwa, Kati na Nyanda za Juu kusini hawaaminiwi na watu wa pwani. Waliaminiwa na mwendazake wakati huo wanaoaminiwa sasa wakiwa wametengwa.
Je, kuna CCM mbili ndani ya chama kimoja? Tusubiri tuone.
Uko sahihi ila sio Bagamoyo ambako wanaipenda sana ccm kama akitajwa JPM na cuf kama akitajwa Maalimu Seif.
Pwani ya Chalinze, Mkuranga na Kibiti ndio wanategemea CCM lakini sio Kisarawe, Kibaha na Bagamoyo
CCM ya sasa imesheheni watu wa kaskazini mashariki Hata hivyo Tanga, Muheza, Handeni Na Pangani hawamwelewi kiongozi wa nchi kabisa kwa sasa
Wananchi wa kawaida huko Kilimanjaro hamwelewi kabisa kiongozi wa nnchi na wanalalamika vibaya mno.
Wanufaika wengine wa utawala huu ni Kigoma ambao awali walikuwa wakiyumbishwa na vuguvugu la CDM na ACT kwa sasa wana lamba asali.
Wanaomwelewa kiongozi wa nchi huko Mbeya ni wale wanaotoka Rungwe Tukuyu pekee wengine wote hawataki hata kusikia.
Iringa na Njombe hawamwelewi kabisa pamoja na kwamba kuna chawa wengi wakitokea huko lakini wananchi wa kawaida hawataki kusikiliza maneno matupu bila vitendo halisia.
Kanda ya Ziwa au kaskazini magharibi huko ndio manunda watupu ukienda wanajifanya kukuchekea lakini moyoni wana lao jambo lisilo la kwaida na ni vigumu kuwabadilisha wakiwa na uamuzi wa sirini.
Dodoma ni aibu tupu na ndio mara kwanza CCM itapasuliwa uchaguzi ujao na kukoksa baadhi ya majimbo labda waended waombe msamaha kwa akina agwe.
Singida huko wanavizia tu akitolewa mtu wao kutoka kwenye baraza la walamba asali wataamua la kufanya.
Morogoro kuna misimamo mikali isiyo yya kawaida ukiwakosea inatarajiwa watabadilisha sura za wabunge karibu wote wa mkoa huo kwenye uchaguzi ujao.