CCM ya Matumaini

CCM ya Matumaini

britanicca

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
17,893
Reaction score
45,415
Ninafarijika,

CCM imerudi kwenye Mikono salama,

Angalizo
Pamoja na CCM kukiuka baadhi ya Misingi 2015-2020 ila rushwa ya hadharani haikuwepo,
Nisingependa Kusikia
1. Wizi wa keki ya Taifa
2. Ubaguzi wa wengine
3. Tukubali Kukosolewa
4. Wapinzani ni ndugu zetu
5. Isimamie Serikali kuleta umoja
6. Isimamie serikali kuajiri

MAMA SAMIA TUNAKUSIHI SANA ULETE MSHIKAMANO

Britannica
 
Baada ya kujaribu madaraka kwa mtu asiyekuwa na maono ya umoja wa kitaifa, aliyeamini katika ubabe na kupora chaguzi. Ni wakati wa kupigania katiba mpya na taasisi huru nchini.

Katiba iliyopo isipobadilishwa inaweza kuleta tena janga kuliko tulilokuwa nalo
 
Wapinzani waache hila na ukorofi wa zama za Lema, kila siku kutaka maandamano. Wananchi wataka siasa safi inayoleta maendeleo. Siyo kupinga kila kitu.
 
Ninafarijika,
CCM imerudi kwenye Mikono salama,
Angalizo
Pamoja na CCM kukiuka baadhi ya Misingi 2015-2020 ila rushwa ya hadharani haikuwepo,
Nisingependa Kusikia
1.Wizi wa keki ya Taifa
2.Ubaguzi wa wengine
3.Tukubali Kukosolewa
4.Wapinzani ni ndugu zetu
5.Isimamie Serikali kuleta umoja
6.Isimamie serikali kuajiri

MAMA SAMIA TUNAKUSIHI SANA ULETE MSHIKAMANO

Britannica
...mnafiki mkubwa wewe!
 
Ngoja tuone kama MATAGA watakubali kirahisi kumuacha atimize majukumu yake kwa misingi ya kikatiba!

Wakifanikiwa tu kumteka nyara kwa ule unafiki wao wa kumtukuza na kumharibu kiongozi kupitia mapambio na ngonjera za kika aina, basi tutarudi tulikotoka.
 
Baada ya kumpata makamu wa Rais hapo ndio tutajua kama Samia ndiye Rais wa jamhuri au kawekwa boya na wanaoendesha serikali wakiwa nje ya IKULU!!!
 
Naona sasa dawa imewaingia mmeanza kunyooka ndani ya mda mfupi tu. Sijui baada ya miaka minne mtakuwa mnasemaje.
 
Jamaa alikua mbabe mpaka aliitwa mungu na yesu hadharani tena na watu wenye wajukuu.
 
Huyo Spika sijui nini na yeye atasepa? ili Mama asipate usumbufu
 
Mikono salama ipi hiyo?

1. Mtandao wa JK.

au

2. Ule wa Lowassa.

Hamna kitu hapo, Katiba Mpya ndio mkombozi wa wanyonge wa nchi hii.

CCM siku zote ni ile ile, cha tofauti ni sura zao tu.
 
Mkuu hayo uliyoyapa kipaumbele ndiyo Magufuli alikua akiyatenda

Magufuli alikuwa na mapenzi mema na nchi yake kwa kiasi kikubwa lakini tatizo lilikuwa jinsi alivyokuwa anatekaleza mambo yake kufikia hayo malengo mazuri.!!! He had no empathy!
 
Back
Top Bottom