CCM Wameonyesha Demokrasia

CCM Wameonyesha Demokrasia

Sijui kisheria hili limekaaje, lakini nanusa conflict of interest. Ingawaje ccm ipo pande mbili, kitakiba, Zanzibar na Tanganyika ni nchi mbili tofauti..inawakuwaje Raisi wa Tanganyika (ingawaje pia ni wa muungano) kusimamia mambo ya Nchi ya zanzibar ili hali Raisi wa Zanzibar amejikalia tu kama kibogoyo... mambo gani haya? Tanganyika ni kweli wanathamini muungano, lakini hili la kusimamia uchaguzi wa ccm ya zanzibar, nchi ya zanzibar, serikali ya wazanzibar na uraisi wa zanzibar, tafadhari waacheni wapumue kwa kweli.. mumewakalia sana kooni sana..
Kuna tofauti kati ya Nchi, Serikali na Chama cha Siasa. Nikurejeshe wewe na wenye mawazo kama yako kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT), 1977 na Sheria husika.

Ibara1: Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.

Ibara ya 3(1) Jamhuri ya Muungano ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa.

Ibara ya 4(1) Shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji, ...
(2) Vyombo vyenye mamlaka ya utendaji vitakuwa ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ...


Ibara ya 33(1) Kutakuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano

Ibara ya 39(1) Mtu hatastahili kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa
Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama:
(c) ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;


Ibara ya 103(1) Kutakuwa na Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ambaye ndiye atakuwa Rais wa Zanzibar na Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na vile vile Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar.

Sheria Ya Uchaguzi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (Na 4, 2018), Ibara ya 43 Kwa kuzingatia masharti ya Katiba, mtu atakuwa na sifa ya kuteuliwa kuwa Mgombea wa Urais iwapo:
(d) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa ambacho kimesajiliwa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa.
 
Kuna tofauti kati ya Nchi, Serikali na Chama cha Siasa. Nikurejeshe wewe na wenye mawazo kama yako kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT), 1977 na Sheria husika.

Ibara1: Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.

Ibara ya 3(1) Jamhuri ya Muungano ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa.

Ibara ya 4(1) Shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji, ...
(2) Vyombo vyenye mamlaka ya utendaji vitakuwa ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ...


Ibara ya 33(1) Kutakuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano

Ibara ya 39(1) Mtu hatastahili kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa
Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama:
(c) ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;


Ibara ya 103(1) Kutakuwa na Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ambaye ndiye atakuwa Rais wa Zanzibar na Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na vile vile Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar.

Sheria Ya Uchaguzi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (Na 4, 2018), Ibara ya 43 Kwa kuzingatia masharti ya Katiba, mtu atakuwa na sifa ya kuteuliwa kuwa Mgombea wa Urais iwapo:
(d) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa ambacho kimesajiliwa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa.
Asante kwa kuelewesha, lakini kuna utata kidogo, tafadhari tusaidie, katiba ya Zanzibar inasemaje ndugu kuhusu vipengele vya:
1. Nchi
2. Serikali
3. Chama

kumbuka, kinacho ulizwa hapa si utendaji wa serikali au mamlaka ya nchi zinavyopatikana ,hizo ibara zote umefanya kazi bure kuzitaja.
Kinacho ulizwa ni upatikanaji wa viongozi wa kuongoza:
1. Jamhuri ya muungano na
2. Zanzibar ( yenye nchi na mamlaka yao Kamili kama katiba yao ya sasa inavyosema)
3. Serikali zote
4. Chama - sehemu zote
5. Hivi ccm imo katika mambo ya muungano? Imetajwa? Kama haimo, je kuchanganya Udongo ndio mkataba?
6. Huo mkataba Wa muungano kama upo, ulilidhiwa na pande mbili?
7. inakuwaje Raisi wa muungano ambaye ndiye kiongozi wa muungano ahusike kumpata kiongozi wa nchi ya Zanzibar ( tafadhari tupe reference ya katiba ya Zanzibar kama inaruhusu hilo) .
8. Mwisho, kiongozi wa muungano hupigiwa kura na wananchi wa pande mbili za muungano, kama Raisi wa muungano anahusika katika uchaguzi wa Zanzibar, ni kwa nini basi wananchi wote wa muungano wasihusike kumpigia kura huyo kiongozi wa Zanzibar? Huoni hapo kuna mkanganyiko au ni ubaguzi wa wao Zanzibar kuhusika kumpigia kura Raisi wa Muungano ambaye pia ni wa tanganyika halafu wananchi wa tanganyika hawana fursa sawa katika kumpigia kura huyo kiongozi wa nchi na Taifa la Zanzibar ?

Huu ni ubaguzi na pia ni breach of fundamental rights, haki ya kuwachaguwa viongozi wote kisawa. Kama wananchi zanzibar wanawachagulia Tanganyika kiongozi basi na wananchi wa Tanganyika pia wahusike kumpigia kura kiongozi wa Zanzibar.

Ibara 1 uliyoitaja: kama Jamhuri ni nchi moja, yanini basi kuwa na Maraisi wawili? Mbona kuna ukimya katika katiba ya muungano wa kusema kwamba wananchi wa tanganyika pia nao wahusike kupiga kura kumchagua kiongozi wa Zanzibar ? Ni hayo- hebu tueleweshe wakwetu...
 

Uchaguzi ndani ya CCM leo hii umeonyesha jinsi chama hicho kikongwe kilivyo bora katika kufanya shughuli zake pale walipomchagua mgombea wa Urais wa Zanzibar Dodoma leo hii.

Mwniyi ndiye atakiwakilisha chama chake mwaka huu. Je, vyama vya upinzani wanaweza kujifunza lolote? Je, CCM walipanga mbinu hii ili kuwahadaa upinzani?
Mzee umeandika kitu gani hiki? Vipi mgombea wa urais bara kapatikana vipi?
 
Demokrasia au udikteta kamili?
Hakuna kumpingaagufuli na aliyejaribu amekiona cha mtema kuni....

Mzee mwinyi alisema anatamani magufuli atawale milele kwa hiyo huo uteuzi wa mgombea wa Zanzibar ni kiini macho tu bali uhalisia ni kua magufuli alifurahia sn kauli ile ya mzee so hiyo ni hisani na mkakati wa kudumu kwa ajili ya nia ovu
Kwahiyo Magufuli hakumtaka Mbarawa kama mlivyoaminishwa na yule taahira wenu kule twiter?
 
Kuna tofauti kati ya Nchi, Serikali na Chama cha Siasa. Nikurejeshe wewe na wenye mawazo kama yako kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT), 1977 na Sheria husika.

Ibara1: Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.

Ibara ya 3(1) Jamhuri ya Muungano ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa.

Ibara ya 4(1) Shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji, ...
(2) Vyombo vyenye mamlaka ya utendaji vitakuwa ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ...


Ibara ya 33(1) Kutakuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano

Ibara ya 39(1) Mtu hatastahili kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa
Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama:
(c) ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;


Ibara ya 103(1) Kutakuwa na Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ambaye ndiye atakuwa Rais wa Zanzibar na Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na vile vile Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar.

Sheria Ya Uchaguzi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (Na 4, 2018), Ibara ya 43 Kwa kuzingatia masharti ya Katiba, mtu atakuwa na sifa ya kuteuliwa kuwa Mgombea wa Urais iwapo:
(d) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa ambacho kimesajiliwa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa.
Sasa wewe unaongelea kukiukwa sheria au unaongelea nini?
Maana mwenzio kakuletea vipengele vinavyofanya hayo yatokee,
Wewe unaleta habari za kama kule hivi na huku iwe hivi! Hayo ndio yapo kwenye katiba?
 
Kasoma upepo kulinda maslai ya familia yake
Yah .......ndio maana pia amepanga kuvunja katiba ili afanye Mambo yake ya hovyo alafu kajiwekea kinga ya kutoshitakiwa akivunja katiba....
 
Yah .......ndio maana pia amepanga kuvunja katiba ili afanye Mambo yake ya hovyo alafu kajiwekea kinga ya kutoshitakiwa akivunja katiba....
Kinga ya kutoshtakiwa hamkingi mtu dhidi ya mabaya uwatendeao wenzake,Kinga sio msahafu ajae anaweza ibadili na ukastakiwa.Karma huwa haizuiliki na chochote,Kinga ni makaratasi.
Japo dhamira yao si njema juu yetu thus wamejiwekea Kinga ili watushugulikie lakini lenye mwanzo Lina mwisho
 
Sijui kisheria hili limekaaje, lakini nanusa conflict of interest. Ingawaje ccm ipo pande mbili, kitakiba, Zanzibar na Tanganyika ni nchi mbili tofauti..inawakuwaje Raisi wa Tanganyika (ingawaje pia ni wa muungano) kusimamia mambo ya Nchi ya zanzibar ili hali Raisi wa Zanzibar amejikalia tu kama kibogoyo... mambo gani haya? Tanganyika ni kweli wanathamini muungano, lakini hili la kusimamia uchaguzi wa ccm ya zanzibar, nchi ya zanzibar, serikali ya wazanzibar na uraisi wa zanzibar, tafadhari waacheni wapumue kwa kweli.. mumewakalia sana kooni sana..
Mkuu hawa marais wa wili lazima wawe wanaelewana vingenevyo muungano wenyewe utavunjika tu
 

Uchaguzi ndani ya CCM leo hii umeonyesha jinsi chama hicho kikongwe kilivyo bora katika kufanya shughuli zake pale walipomchagua mgombea wa Urais wa Zanzibar Dodoma leo hii.

Mwniyi ndiye atakiwakilisha chama chake mwaka huu. Je, vyama vya upinzani wanaweza kujifunza lolote? Je, CCM walipanga mbinu hii ili kuwahadaa upinzani?
ILA JAMANI SARE ZA CCM HAZINA MVUTO KABISA HASA KWA VIJANA. UKIVAA SARE YA CCM HATA KAMA UNA MIAKA 20 UNAONEKANA BABU KABISA. WEWE MWONE JIWE NA WENZAKE WANAVYOONEKANA KUCHOKA.
 
Sasa wewe unaongelea kukiukwa sheria au unaongelea nini?
Maana mwenzio kakuletea vipengele vinavyofanya hayo yatokee,
Wewe unaleta habari za kama kule hivi na huku iwe hivi! Hayo ndio yapo kwenye katiba?
Crimea rejea maudhui ya bandiko kuu na majadiliano ambapo kunajengwa hoja kuwa Mgombea wa URais wa Serikali ya Mapindizi Zanzibar hapaswi kupendekezwa/kuchaguliwa na Vikao vya juu vya Chama na tena nje ya Zanzibar. Dhana/hoja hii ni potofu, nje ya Katiba ya JMT (1977), kwa Ibara nilizonukuu, na inalenga kupandikiza chuki kati ya WaZanzibari na WaTz bara.
 
Asante kwa kuelewesha, lakini kuna utata kidogo, tafadhari tusaidie, katiba ya Zanzibar inasemaje ndugu kuhusu vipengele vya:
1. Nchi
2. Serikali
3. Chama.

Ibara 1 uliyoitaja: kama Jamhuri ni nchi moja, yanini basi kuwa na Maraisi wawili? Mbona kuna ukimya katika katiba ya muungano wa kusema kwamba wananchi wa tanganyika pia nao wahusike kupiga kura kumchagua kiongozi wa Zanzibar ? Ni hayo- hebu tueleweshe wakwetu...

Umehoji mambo mengi ambayo kimsingi yamekuwa yakihojiwa, na yataendelea kuhojiwa km Zanzibar ni nchi au la, na kuhusu aina ya muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Vifungu vya Katiba ya JMT (1977) na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (Na. 4, 2018), zimeanisha sifa za mtu kuchaguliwa kuwa Rais.

Kwamba Zanzibar ina Katiba yake si jambo la kuzua ubishi kwa sababu Taasisi yoyote yenye viongozi wa uwakilishi, moja ya masharti ya uendeshaji wake ni kuwepo kwa Katiba - naamini unajua maana ya Katiba.
 
Umehoji mambo mengi ambayo kimsingi yamekuwa yakihojiwa, na yataendelea kuhojiwa km Zanzibar ni nchi au la, na kuhusu aina ya muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Vifungu vya Katiba ya JMT (1977) na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (Na. 4, 2018), zimeanisha sifa za mtu kuchaguliwa kuwa Rais.

Kwamba Zanzibar ina Katiba yake si jambo la kuzua ubishi kwa sababu Taasisi yoyote yenye viongozi wa uwakilishi, moja ya masharti ya uendeshaji wake ni kuwepo kwa Katiba - naamini unajua maana ya Katiba.

Ndugu, asante, maana ya katiba naifamu... nilichotaka kusema ni kwa ufupi tu, sisi watanganyika na viongozi wetu, kwa nini hatuoni ukakasi kushiriki vikao vinavyoamua mambo ya wanzibari? Hivi mchakato huo (wa kumpata mgimbea wa Uraisi wa zanzibar ) ukihojiwa mahakamani kwamba hauna legal legitimacy kwa kuwa tu Raisi wa Tanganyika arishiriki, huoni itakuwa kizungumkuti ?

Hayo ya kuhoji nchi au sio nchi, waendelee tu kuhoji, mimi langu ni hilo la tuwaache wazanzibari wajichagulie Raisi wao wenye hata humo ndani ya ccm ya Zanzibar ( sio ccm ya bara). CCM bara ikae kando na iwaache ccm Zanzibar wamchague wanaye mtaka... ni hayo tu... Asante kwa kuelimisha uma Mwengeso
 
Kinga ya kutoshtakiwa hamkingi mtu dhidi ya mabaya uwatendeao wenzake,Kinga sio msahafu ajae anaweza ibadili na ukastakiwa.Karma huwa haizuiliki na chochote,Kinga ni makaratasi.
Japo dhamira yao si njema juu yetu thus wamejiwekea Kinga ili watushugulikie lakini lenye mwanzo Lina mwisho
Sure........wacha watambe sn sasa na kufanya kufuru za kila aina lkn sisi tupo tunawela rekodi sawa watalipa kutokana na matendo yao maovu
 
Sure........wacha watambe sn sasa na kufanya kufuru za kila aina lkn sisi tupo tunawela rekodi sawa watalipa kutokana na matendo yao maovu
Sasa hayo malipo utafaidika wewe au vilembwe?
 
Kilichofanyika ni kumpitisha au kumuidhinisha au kumthibitisha na siyo uchaguzi. Unachagua nini wakati hakuna mbadala au mshindani mwingine? Jifunzeni CHADEMA wenzenu wale ndio wanachagua kweli. Nafasi ya uenyekiti wa chama kuna kuwa na wagombea wakati CCM hakuna wagombea isipokuwa mtu mmoja tu ndiye anapitishwa na kuthibitishwa. Kwenye urais wenzenu CDM wana wagombea. Ninyi mmemuweka mmoja kwakuwa ni rais na mwenyekiti. Mlichofanya siyo kuchagua ila ni kumuidhinisha aliyepitishwa bila washindani. Halafu bila aibu itashangaa CCM matango wanasema Mbowe ni dikteta!
 
Wangekuwa wa maana sana kama wangekuwa hawaibi kura, lkn kwa tabia yao hii ya kutegemea tume iwabebe inafanya yote uliyoandika yaonekane takataka tu.
 
Back
Top Bottom