CCM Wameonyesha Demokrasia

CCM Wameonyesha Demokrasia

Sijui kisheria hili limekaaje, lakini nanusa conflict of interest. Ingawaje ccm ipo pande mbili, kitakiba, Zanzibar na Tanganyika ni nchi mbili tofauti..inawakuwaje Raisi wa Tanganyika (ingawaje pia ni wa muungano) kusimamia mambo ya Nchi ya zanzibar ili hali Raisi wa Zanzibar amejikalia tu kama kibogoyo... mambo gani haya? Tanganyika ni kweli wanathamini muungano, lakini hili la kusimamia uchaguzi wa ccm ya zanzibar, nchi ya zanzibar, serikali ya wazanzibar na uraisi wa zanzibar, tafadhari waacheni wapumue kwa kweli.. mumewakalia sana kooni sana..
Una point kwa mbali ila HUJAIELEWA POINT YA ULIYEMWUOTE BILA SHAKA...
 
Demokrasia au udikteta kamili?
Hakuna kumpingaagufuli na aliyejaribu amekiona cha mtema kuni....

Mzee mwinyi alisema anatamani magufuli atawale milele kwa hiyo huo uteuzi wa mgombea wa Zanzibar ni kiini macho tu bali uhalisia ni kua magufuli alifurahia sn kauli ile ya mzee so hiyo ni hisani na mkakati wa kudumu kwa ajili ya nia ovu

Hizi zimebaki kama zilipendwa mkuu.
 

Uchaguzi ndani ya CCM leo hii umeonyesha jinsi chama hicho kikongwe kilivyo bora katika kufanya shughuli zake pale walipomchagua mgombea wa Urais wa Zanzibar Dodoma leo hii.

Mwniyi ndiye atakiwakilisha chama chake mwaka huu. Je, vyama vya upinzani wanaweza kujifunza lolote? Je, CCM walipanga mbinu hii ili kuwahadaa upinzani?
Nauliza kwa nini Prof Mbarawa Mnyaa walimtoa mapema? Nilikuwa nadhani ndio angekuwa mshindani wa Dr. Hussein Meinyi au imeakaje hii?
 

Uchaguzi ndani ya CCM leo hii umeonyesha jinsi chama hicho kikongwe kilivyo bora katika kufanya shughuli zake pale walipomchagua mgombea wa Urais wa Zanzibar Dodoma leo hii.

Mwniyi ndiye atakiwakilisha chama chake mwaka huu. Je, vyama vya upinzani wanaweza kujifunza lolote? Je, CCM walipanga mbinu hii ili kuwahadaa upinzani?
Demokrasia ndani ya ccm nje ya ccm ni kuzuia mikutano ya vyama vya upinzani
 
Uongo mkuu mi nilijua ni Mbarawa
Basi utakuwa upo mwisho wa dunia.Mwinyi aliandaliwa mapema sana.ndio maana hata yeye hakuwa na wasi wanataka wafanye kama baba yake apige mitano alafu haje huku, halafu huyo mbarawa ashike huko.
Mijinga sana ccm.
 
haaa,,,we jamaa umenichekesha sana eti kuprint form moja!!.
mbona CDM 2015 mliprint form moja ya Edlow tu.
Kumbe hujui chochote 2015 kulikuwa na ukawa.vyama vinavyo unda ukawa ndio viliamua wamsimamishe lowasa kwa tiketi ya chadema.😁😁😁😎😎😎😎😂😂😂😂 kumbe huna hulijualo kazi kupuyanga tu
 
Kumbe hujui chochote 2015 kulikuwa na ukawa.vyama vinavyo unda ukawa ndio viliamua wamsimamishe lowasa kwa tiketi ya chadema. kumbe huna hulijualo kazi kupuyanga tu
wewe ndo hujui kitu.makubaliano ya ukawa yalikuwa ndani ya vyama wafanye uchaguzi kisha kila chama kitoe mgombea mmoja kisha wagombea washindanishwe achaguliwe mgombea mmoja awakilishe ukawa.
Lakini ndani ya cdm Lowasa alipitishwa kwa nguvu pia na mpaka kwenye ukawa akapitishwa kwa nguvu.matokeo yake Lowasa kaacha ukawa imevurugika kawakimbia.mazuzu nyie.
 
Hamna demokrasia. wangeliwacha wazenji wakachaguwa mtu wao. Kura ziligawanyika vibaya sana na kuonyesha mpasuko. Khalid alipigiwa na wakaskazini na Nahoda kapigiwa na wakusini. Hussein kapigiwa na wenziwe wa tanganyika. Hio ndio demokrasia ya CCM. sasa kama kweli munataka demokrasia, leteni NEC na ZEC zilizo wazi na zenye kutenda haki. Hapo tutajua demokrasia ipo. Venginevo ni kufanya watanzania wajinga.
 
wewe ndo hujui kitu.makubaliano ya ukawa yalikuwa ndani ya vyama wafanye uchaguzi kisha kila chama kitoe mgombea mmoja kisha wagombea washindanishwe achaguliwe mgombea mmoja awakilishe ukawa.
Lakini ndani ya cdm Lowasa alipitishwa kwa nguvu pia na mpaka kwenye ukawa akapitishwa kwa nguvu.matokeo yake Lowasa kaacha ukawa imevurugika kawakimbia.mazuzu nyie.
Acha ujuha fomu zilitoka ndani ya chadema na wakampitisha lowassa.ila ndani ya ccm mwaka huu fomu ili printiwa moja na mkapiga mkwara kwa yeyote atakae tia nia.
 
Acha ujuha fomu zilitoka ndani ya chadema na wakampitisha lowassa.ila ndani ya ccm kwaka huu fomu ili printiwa moja na mkapiga mkwara kwa yeyote atakae tia nia.
Form ilitoka moja tu ya Lowasa peke yake na ofisi ya ufipa ikapigwa kufuli.
 
Yeah nimependa Mwenyekiti Mgombea kusimamia process nzima yeye mwenyewe
CCM imeonesha kuwa unawezekana, jatika mfumo uliopo, kuwa na uchaguzi ulio huru na wa haki.

Badala ya kudai Tume Huru ya Uchaguzi, ili kulinda kura za wagombea, mawakala wahusishwe kwenye kuhesabu kura, kama ilivyofanyika leo katika uchaguzi wa mgombea wa Urais Zanzibar, kwa tikiti ya CCM.

Ili pasiwepo na udanganyifu au wizi wa kura, wakala apokee kura za mgombea wake, kisha baada ya kuzihesabu, awape mawakala wenzake, ambao kila mmoja wao atahakiki hesabu ya kura hizo, hadi mawakala wote wamejiridhisha. Baada ya hapo kura zitajumlishwa na wao (Mawakala) kuweka sahihi za kukubali matokeo hayo.
 
Demokrasia kwa nchi nyingine? Hapa kwao aameshindwaje kuweka viongozi wengine akina Membe akajipima mabavu
Membe, pamoja na kufukuzwa kwenye chama, anaendelea kuonesha uchanga wake kisiasa kwa kuvunja kanuni za mIsingi ya demokrasia. Moja ya hizo ni kukata rufaa badala ya kunung'unika na kulaumu, kama afanyavyo kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari. Ama anatafuta HURUMA ya jamii au AMEKATA TAMAA.
 
Back
Top Bottom