Wapendwa wana JF, nimesikia mara nyinyi CHADEMA wakihusishwa na Udini, Ukanda, Dhuluma na sasa Ufisadi. Inaniumiza sana, maana nina imani sana na CDM, lakini kama hizo hoja ni za kweli
....mmmmm.
Jana nilikuwa na mkongwe wa siasa na mwanazuoni maarufu sana hapa Tanzania, katika zungumza yake alisema na ninamnukuu CHADEMA is a gang of criminals, am just deeply sorry for Dr. Slaa, Zitto Kabwe and my great comrade Prof. Baregu
You know, CDM is not a political party rather
..a group of frustrated and disparate individuals under the umbrella of politics
.. Ukweli niliumia sana kimoyomoyo na nikaamua kutoka mahala pale. Kwa hiyo nimeona ni vema nijaribu kujua zaidi juu ya CDM.
Kwa yeyote mwenye takwimu au ufahamu naomba anisaidie kujua yafuatayo:
1. Uwiano wa waislamu kwa wakristo miongoni mwa wabunge wa CDM
2. Uwiano wa waislamu kwa wakristo miongoni mwa wajumbe wa Halmashauri Kuu na Sekretariat ya CDM
3. Kati ya wabunge wote wa CDM ni wabunge wangapi wa CDM wanatoka Kanda ya Kaskazini hususani mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara+ na Singida?
4. Je ni kweli Mh. Mbowe kawauzia CDM magari 3 yaliyotumika kwa TSh 480,000,000?
5. Kama ni kweli, ni magari mangapi, aina gani (kama ni Fuso truck, je ni 4ton au 10ton) na ya mwaka gani?
6. CHADEMA ati wamewadhulumu watu wengi waliojitoa kupiga kampeni kwa matarajiyo ya kurudishiwa japo kidogo walichotumia, hii ni kweli? Mfano ni yule M/kiti wa CDM aliyekimbilia CCM majuzi...na wengine wengi wanalalamika....