CCM waijibu CHADEMA

fikirini

Senior Member
May 24, 2011
114
22
Mbunge wa CCM ameibuka na kuwajibu wapinzani wakati akichangia mjadala wa bajeti leo. Alimjibu Mbunge wa Mbozi kwa tiketi ya Chadema David silinde aliyesema kuwa ni miaka 50 sasa tangu uhuru na Tz haina maendeleo. Zungu amesema Tz inamaendeleo na mafanikio makubwa na isingekuwa hivyo basi hata yeye(Silinde) asingeweza fika bungeni angebakia huko huko na degree yake(mmmh, hapa kuna uhusiano kweli?) mimi nilivyomuelewa silinde au kwa mtazamo wangu ni kuwa maendeleo tuliyonayo Tz si kiwango stahiki, hatustahili kuwa hapa tulipo ukilinganisha na rasilimali kibao ambazo nyingi wanazichezea wachache walioko madarakani na zingine wageni wanagawiwa.
Jamani upinzani haupo kwa ajili ya kupinga tu, wanauchungu pia na nchi yao.
 
Mbunge wa CCM ameibuka na kuwajibu wapinzani wakati akichangia mjadala wa bajeti leo. Alimjibu Mbunge wa Mbozi kwa tiketi ya Chadema David silinde aliyesema kuwa ni miaka 50 sasa tangu uhuru na Tz haina maendeleo. Zungu amesema Tz inamaendeleo na mafanikio makubwa na isingekuwa hivyo basi hata yeye(Silinde) asingeweza fika bungeni angebakia huko huko na degree yake(mmmh, hapa kuna uhusiano kweli?) mimi nilivyomuelewa silinde au kwa mtazamo wangu ni kuwa maendeleo tuliyonayo Tz si kiwango stahiki, hatustahili kuwa hapa tulipo ukilinganisha na rasilimali kibao ambazo nyingi wanazichezea wachache walioko madarakani na zingine wageni wanagawiwa.
Jamani upinzani haupo kwa ajili ya kupinga tu, wanauchungu pia na nchi yao.

N inani mwenye akili timamu anaweza kuyaita haya ni maendeleo baada ya miaka 50 ya uhuru

wanaopata maji ya bomba nchi nzima ni asilimia 12%
ni asilimia 14% ya watanzania wenye umeme na kwa upande wa vijijini ni asilimia 4% tu .
This is a failure.
 
Hawa CCM wanaakili mgando,wafinyu wa mawazo na wanawaza kwa kutumia makamasi,wapoteshaji wa jamii,ANGUKO LA CCM LIMETIMIA
 
Unalinganisha uwezo wa kufikiri wa Zungu la unga na kijana msomi aliyemwangusha Dr. Siyame
 
Niliposoma takwimu alizoanika Zito kwenye hotuba yake nimeumia sana. Just emagine, 20% ya watanzania wanamiliki 42% ya utajiri wa nchi, walobaki ni kichekesho. Kweli maendeleo yapo ila yamekaliwa na wachache, jambo linalofanya kundi kubwa la watu kuwa katika lindi la umaskini.
CCM hawana huruma kwa sababu wao ndo wanamiliki utajiri mkubwa. Wenye uchungu na wananchi ndo hao wachache ambao wanawabeza na kuwaita wapinzani. Napendekeza jina UPINZANI lisitumike tena na badala yake waitwe WAKOSOAJI. Kama sio CDM mabadiliko mengi tunayoyaona kwa sasa yasingefanyika.
 
N inani mwenye akili timamu anaweza kuyaita haya ni maendeleo baada ya miaka 50 ya uhuru

wanaopata maji ya bomba nchi nzima ni asilimia 12%
ni asilimia 14% ya watanzania wenye umeme na kwa upande wa vijijini ni asilimia 4% tu .
This is a failure.

Swadakta! wao wakipanda ndege kutembea nchi za nje wakati walowaacha hata pesa ya kununulia baiskeli hawana - wanaona ni maendeleo. Ni upofu huo.
 
Wabunge mufilisi wanajulikana . Wananchi wameamka sasa wana kazi kweli ya kupata kura . Wataujua ukweli mwaka 2015 waache tu wapige miayo hapo wakidhani ndiyo points za kumtetea mtanzania wa jimboni kwake .
 
Wabunge wa CCM ni vilaza wa aina yake. mbunge mwenye akili timamu anasimama na kulinganisha maendeleo ya wakati wa mkoloni na ya sasa. Tunachowataka wabunge walinganishe iwe ni maendeleo kati ya TZ na nchi zilngine zilizopata uhuru sawa na TZ(Tanganyika)

Kulinganisha nyakati za mkoloni na sasa ni kuwakosea adabu Watanzania kwani, pengine hata mkoloni angelikuwepo hadi leo angekuwa amejenga hayo madarasa ambayo CCM inatamba nayo. Suala letu kubwa la kuangalia liwe ni kuwa je kwa miaka 50 ya uhuru tunapaswa kuwa hapo tulipo?
 
Great failure for our government with miagle thinking and arguing capacity
 
Mbunge wa CCM ameibuka na kuwajibu wapinzani wakati akichangia mjadala wa bajeti leo. Alimjibu Mbunge wa Mbozi kwa tiketi ya Chadema David silinde aliyesema kuwa ni miaka 50 sasa tangu uhuru na Tz haina maendeleo. Zungu amesema Tz inamaendeleo na mafanikio makubwa na isingekuwa hivyo basi hata yeye(Silinde) asingeweza fika bungeni angebakia huko huko na degree yake(mmmh, hapa kuna uhusiano kweli?) mimi nilivyomuelewa silinde au kwa mtazamo wangu ni kuwa maendeleo tuliyonayo Tz si kiwango stahiki, hatustahili kuwa hapa tulipo ukilinganisha na rasilimali kibao ambazo nyingi wanazichezea wachache walioko madarakani na zingine wageni wanagawiwa.Jamani upinzani haupo kwa ajili ya kupinga tu, wanauchungu pia na nchi yao.
Mie pia nilimsikia alipoongea usaha wake huo.Hivi anadhani tz ingeongozwa na machifu kufikia sasa bado tungetemea uchi! Mzembe kichwani.Namna ya kusurvive ipo tu ni natural...tunataka maendeleo baada ya miaka 50 ya uhuru.
 
Back
Top Bottom