MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Ndugu zangu wanaCCM mlioko humu ndani na kwingineko, hali ni ngumu sana huyu mtu anatuzidi kwa kiasi kikubwa sana kwa ninavyotazama mimi na msema kweli mpenzi wa Mungu.
Huyu ni ambaye ni sawa na Faru aliyejeruhiwa yupo Energetic, anaongea mambo magumu yanayogusa ndani, anaijua sheria sana anajiamini. Naomba sana kuelekea mwishoni tujitathmini.
Tusijipe moyo kwakuwa sisi ni Chama dola kwa maana kwamba tuna uwezo wa kufanya lolote tusalie madarakani, tufahamu kwamba huyu bwana katika hotuba zake kuna zaidi ya dakika 30 za kuelimisha umma namna ya kuzijua haki zao wakati wa uchaguzi. Hawa watu wanaojitokeza kumwangalia ni wengi na Ikumbukwe kwamba uchaguzi uliopita wa serikali za mitaa watu walijitokeza kujiandikisha tena wengine wanalazimishwa na MaDC mwaka jana na wengi tunakumbuka vizuri. Kwahiyo waliojiandikisha ni wengi sana na serikali ilihamasisha hilo mwaka jana.
Tusijivunie wanachama wetu zaidi ya milioni 11 tulionao, wengi ni majeruhi wa kura za maoni wako nasi kwenye nyuso tu lakini moyoni hawapo na tunawaona. Huu umati ukimpiga kura nyingi huyu bwana hatutaweza kulazimisha kumzuia tutaumiza watu. Kama kuna makosa ya kimkakati naona tunataka kuchelewa Muda unayoyoma chama ndio halitajwi sana siyo mitandaoni wala mitaani zaidi utamsikia Tundu Lissu tu. Ukisikia CCM kinatajwa labda siku hiyo kuna kampeni mahali flani.
Mara nyingi CCM tumekua wagumu hatushauriani na tunajiona tunajua sana hasa katibu wetu wa Itikadi na wenezi , tunaenda kuumia na mimi naenda kukata tamaa walai.
Huyu ni ambaye ni sawa na Faru aliyejeruhiwa yupo Energetic, anaongea mambo magumu yanayogusa ndani, anaijua sheria sana anajiamini. Naomba sana kuelekea mwishoni tujitathmini.
Tusijipe moyo kwakuwa sisi ni Chama dola kwa maana kwamba tuna uwezo wa kufanya lolote tusalie madarakani, tufahamu kwamba huyu bwana katika hotuba zake kuna zaidi ya dakika 30 za kuelimisha umma namna ya kuzijua haki zao wakati wa uchaguzi. Hawa watu wanaojitokeza kumwangalia ni wengi na Ikumbukwe kwamba uchaguzi uliopita wa serikali za mitaa watu walijitokeza kujiandikisha tena wengine wanalazimishwa na MaDC mwaka jana na wengi tunakumbuka vizuri. Kwahiyo waliojiandikisha ni wengi sana na serikali ilihamasisha hilo mwaka jana.
Tusijivunie wanachama wetu zaidi ya milioni 11 tulionao, wengi ni majeruhi wa kura za maoni wako nasi kwenye nyuso tu lakini moyoni hawapo na tunawaona. Huu umati ukimpiga kura nyingi huyu bwana hatutaweza kulazimisha kumzuia tutaumiza watu. Kama kuna makosa ya kimkakati naona tunataka kuchelewa Muda unayoyoma chama ndio halitajwi sana siyo mitandaoni wala mitaani zaidi utamsikia Tundu Lissu tu. Ukisikia CCM kinatajwa labda siku hiyo kuna kampeni mahali flani.
Mara nyingi CCM tumekua wagumu hatushauriani na tunajiona tunajua sana hasa katibu wetu wa Itikadi na wenezi , tunaenda kuumia na mimi naenda kukata tamaa walai.