CCM tumeiga au hatujui tunachokifanya?

CCM tumeiga au hatujui tunachokifanya?

Aiseee
Kimsingi cdm ni wabunifu na ndio hasa wanaopendwa kwakuwa ni chama cha kizazi hiki. Ccm ni chama kizee za kizazi kilichopita hivyo hakina ubunifu na wala hakina mvuto. Wanachofanya ni kuwaiga cdm kwakuwa ndio wabunifu na mvuto, ili na wao wapate mvuto. Hao ccm nawafananisha na mwanamke mzee anayevaa mavazi ya vijana ili na yeye aonekane bado ni mrembo. Ukweli ni kuwa hata ccm ifanye nini na iige nini, sio rahisi kupata mvuto kwani watu wamekichoka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*Anaandika Askofu Benson Bagonza*

Unawezaje kusema tuna judicial independence wakati:

Jana wapinzani walienda kutoa watu wao, Bwana jela akasema yuko kikaoni, wadhaminiwa wakalala. Lakini Polepole alienda bila risiti akapewa mfungwa wake.

Leo wapinzani wamezuiwa kuingia kumpokea Msigwa, lakini Polepole ameruhusiwa kuingia na gari.

Jr
 
Slow learners.. Huwa wana elewa baada y akufanya kosa. Learning through mistakes.. Na wao Ccm kumchangia ng'ombe alie katwa mkia wanaona ni ujiko kumbe on the other hand wanaisaidia Chadema ku prove kwamba ile hukumu haikuwa sawa ndio maana na wao wakawa na huruma na mwanachama wao ambae alionewa akiwa chama cha upinzani.
Hawa ndio viongozi wanao msaidia Mwenyekiti wa Chama chetu..

Sent using Jamii Forums mobile app
Wana ccm huwa wanaanza kutenda then wanafikiri.
 
Ni Jambo la aibu sana,yaani hakuna atakaye jibu hayo maswali
 
Kesho kutwa Kangi Lugola akihukumiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi nawashihi wanaCCM wachangishe pesa za kumkomboa gerezani.
Kwann wasiwatoe wanachama wao waliojela wawambie mfungwa yeyeto ccm mwenye kadi aandikishe jina kuliko ya dabo standard Masinji ni ccm wa juzi hali ndani wako wanachama ccm wakongwe tu
 
CCM imejaa wapumbavu watupu
Na Thadei Ole Mushi

Huwa napenda Sana kumchallenge Mwenezi wa Chama changu CCM, Rafiki yangu Ndugu Humfrey Polepole. Naamini Ni mjenzi mzuri wa Hoja na Logic hebu tu build Logic hapa from the ground.

Mashinji na kina Mbowe waliandamana na Kusababisha Kifo cha Mtoto ambaye ni very Innocent Akwilina, Kitendo kile kichukuliwa na Jamhuri kuwa Ni uvunjifu mkubwa wa amani na uchochezi kwa jamii. Wakashitakiwa na kukutwa na Makosa 12. Mashinji Ni mwanachama wa kawaida kabisa wa CCM ambaye alivunja Sheria za Nchi Kama wanaccm wenzake. Tuna logic tatu hapa za kujenga;-

1. CCM inashiriki Sasa Moja kwa Moja kusupport uvunjifu wa amani? Maana Chadema wao wanachangishana kwa kuwa hawakubaliani na Hukumu je tumeiga tu na sisi tuonekane tumo?

2. Ni Wana CCM wangapi wapo magereza waliotakiwa kulipa tu faini ya Milioni Kumi? Huyu Mashinji amepataje uspesho wa Mara Moja ndani ya chama au tumeiga tu Chadema?

3. Kwa kuwa Chadema inamchangia Mbowe na Viongozi wengine wa Chama Chao kwa sababu hawakubaliani na Hukumu ya makosa yao je hatuoni na sisi tunapingana na Jamhuri? Sio kwamba tumiega tu Chadema?

Hizi fedha angelipiwa tu kimya kimya Tena aonekane anaomba omba kila mahali kuonyesha hatukupendezwa na Uchochezi ule.

Tumejitofautishaje na Chadema kwenye Kesi ile Sasa? Nawaona vijana wa CCM wanakimbizana na mwenezi kuonyesha wao Ni wa Kwanza kulipa fain ya mashinji ila wameaacha kufanya hesabu ndogo Sana huku njee.

Ole Mushi
0712702602

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom