VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Kuiga si kuzuri. Kuiga kuna madhara yake. Kuiga huonesha kukosekana kwa ubunifu na umakini.Hatuwezi kuwaacha viongozi wa chama chetu wakaiga kila kitu kutoka kwa wapinzani.Si kila mapambano yanahitaji kuiga.Tulipoamua kubaki Bungeni na UKAWA wakatoka nje ya Bunge tulikuwa sahihi kwa mitazamo yetu ya kichama.Kwanini sasa tunabadilika?
UKAWA wamechagua mapambano nje ya Bunge la Katiba. Tungewaacha waendelee na sisi tuendelee na misimamo ya kichama ya kuendelea kujadili Rasimu kadiri ya matakwa na misimamo ya kichama.Ya mbele tutajua hukohuko.Kubadilika sasa na kujaribu kufuta nyayo za UKAWA ni kuonesha kuwa sasa chama kinatikisika na kutishika. Ni kuonesha kuwa,nasi tulipaswa kususia Bunge!
CCM si 'photocopy machine'.Ni chama chenye Idara nyeti na zilizokamilika.Iweje Idara inayohusiana na ubunifu wa kisera isibuni aina tofauti ya mapambano ya kisiasa badala ya kufuata kila kinachofanywa na upinzani!? Tukishindwa na mikutanoni itakuwaje? Kuna kushindwa kazi.Kuna kubaki nyuma.Kuna kufika mwisho wa ufikiri na ubunifu. Si jambo la kuchewa kichama.Linatudhalilisha.Linatufifisha.
Tafadhali tubaki na misimamo yetu.Tubaki njia kuu.Michepuko (kuigaiga) siyo dili!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
UKAWA wamechagua mapambano nje ya Bunge la Katiba. Tungewaacha waendelee na sisi tuendelee na misimamo ya kichama ya kuendelea kujadili Rasimu kadiri ya matakwa na misimamo ya kichama.Ya mbele tutajua hukohuko.Kubadilika sasa na kujaribu kufuta nyayo za UKAWA ni kuonesha kuwa sasa chama kinatikisika na kutishika. Ni kuonesha kuwa,nasi tulipaswa kususia Bunge!
CCM si 'photocopy machine'.Ni chama chenye Idara nyeti na zilizokamilika.Iweje Idara inayohusiana na ubunifu wa kisera isibuni aina tofauti ya mapambano ya kisiasa badala ya kufuata kila kinachofanywa na upinzani!? Tukishindwa na mikutanoni itakuwaje? Kuna kushindwa kazi.Kuna kubaki nyuma.Kuna kufika mwisho wa ufikiri na ubunifu. Si jambo la kuchewa kichama.Linatudhalilisha.Linatufifisha.
Tafadhali tubaki na misimamo yetu.Tubaki njia kuu.Michepuko (kuigaiga) siyo dili!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam