hamna namna nyingine ccm life au kipone
Anakatwa? Hakatwi? Hahaaa
Yangu macho niuone ujasiri wa karne ya 21
Hakuna anaempenda lowasa, ananunua na kufanya propaganda nyingi kulaghai wa tanzania aonekane anakubalika. CCM kupitia wabunge wake walishakosa imani nae wakamwangusha uwaziri mkuu, Wakimleta tena kwa wananchi na kuanza kumsafisha katika kashfa ambazo wao CCM walishindwa kumvumilia itakuwa maajabu sana na itabidi waibe kura maana watashindwa, wananchi wataonyesha hasira zao kwenye sanduku la kura.
CCM iteuwe mtu safi mwadilifu, mchapakazi asiye na ma kashfa mengi then wamnadi na kumfanyia kampeni kama chama.
Mpaka sasa kamati ya maadili ya Chama Cha Mapinduzi CCM bado iko njia panda katika kufanya maamuzi magumu juu ya wanachama wake waliofungiwa kwa kuanza kampeni mapema.
Imebainika kuwa sababu kubwa inayowafanya wajumbe kamati hiyo inayoongozwa na Philip Mangula kuwa wakati mgumu kutona na kwamba viongozi wa juu wa chama hicho kushinikiza jina la Lowassa kutwa.
Kinachosumbua mpaka sasa ni ushawishi mkubwa wa mh. Lowassa ndani ya chama na nje ya chama hicho na imegundulika kuwa si kweli kwamba kamati hiyo inajadili majina yote ya waliofungiwa inasema kuwa muda mwingi zaidi ya asilimia 70% ya muda wote kamati inapo kutana ni kumjadili Lowassa tu.
Tatu,vijina wenye mapenzi mema na nchi wameanza kujiorganize nchi nzima kuhakikisha kuwa nchi inatawaliwa na mtu mwenye maamuzi magumu na ya uhakika wamechoka kubuluzwa.
Hapa mawili LOWASSA RAIS AU MWISHO WA CCM.
Ni wazi kuwa Mzee Lowassa anaungwa mkono na wenyeviti wa CCM wa zaidi ya Mikoa saba, nikitaja kwa uchache, Geita, Singida, Arusha, Manyara, Shinyanga, Mara, Kilimanjaro, Dar es salaam.
Watu hawa wana nguvu na ushawishi mkubwa na ndio nguzo ya kampeni ya chama Mikoani na Wilayani, jaribio lolote la kumkata Lowassa, litashusha kishindo kikuu Mikoani ambapo zitaendeshwa kampeni za kumpinga au kumdhoofisha yeyote atakayeteuliwa.
Mpaka sasa Lowassa ana kura milioni moja kutoka kwa wana CCM wachache, hii inatokana na wengi kukosa nafasi ya kumdhamini.
Akikatwa ni wazi kura milioni moja zimekwenda, achilia mbali za mamilioni kadhaa wasio wana CCM ambao ni washabiki wake.
Taarifa zinaeleza kwamba kama angepata muda wa kutosha, Lowassa alikuwa na uwezo wa kupata wadhamini milioni nne ndani ya CCM pekee.
watu kibao tuko CCM kwa sababu ya EDL tu.
in absence of nyerere,mhuni yoyote anaweza kupeperusha bendera ya ccm ya urais...imagine membe naye eti!!!!!!
*Kwannini lowasa alitajwa list of shem?
*Kwanini lowasa alitakawa kuvuliwa gamba ndani ya siku 90 ??
Nikipata haya majibu kwa ufasaha naweza kubadili msimamo wangu
Spidi 200 Kwa kilometa ndio Spidi gani mkuu?Ni Dua ya Kuku haimpati Mwewe; UKAWA mtazidi kuweweseka, CCM inasonga mbele kwa spidi 200 kwa kilometa
Wana Jamii Forum nauona mwisho wa CCM ndio umefikia tamati.CCM hawakujua kuwa kila,chenye mwanzo kina mwisho wake.Kama,ambavyo JK amehitimisha bunge jana hivyohivyo anakwenda na chama chake.Ishara moja ya dhahiri ni,hii ukimpitisha Lowasa chama kinagawanyika.Usipompitisha vilevile chama,kimegawanyika.Kwahiyo sioni nafuu yoyote.CCM ilianza kama mtoto hatimaye ikawa kijana na baadaye imezeeka kinachofuata,nini.Nukuu Jaji Warioba,Jaji Manento,Butiku,Polepole na Waraka wa Kakobe kwa JK