VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Tutalinda kura zetu katika Kata zote 26 (tukiiacha Mtae ya kule Lushoto). Tunaamini kuwa tutashinda kwa ushindi wa kimbunga katika Kata fulanifulani.Si zote.Zote haiwezekani.Lakini,tutashinda Kata nyingi-hasa za mkoa wa Pwani na Kusini.Na zile za vijijini mno.
Kule ambapo bado tunapendwa.Kule ambapo bado wananchi ni 'wetu'. Kule ambapo wananchi wanaamini kuwa Wajumbe wa Nyumba Kumi wana mamlaka kiserikali. Kule ambapo chopa za CHADEMA hazijafika au hazijafika mara nyingi.Kule ambapo tunaweza kusema na wanachi wakafanya bila kuhoji. Mahali pale ambapo kura zahesabiwa na pande nyingi zikiwa na lengo la mshindi yule yule.
Nasi leo hatulali.Tumepewa kazi ya kulinda kura zetu. Zisiibwe. Mimi naelekea Kata ya Magomeni Bagamoyo kwa shughuli za ulinzi. Nitakaa mita mia moja toka mlango wa kituo cha kuhesabia kura.Leo hatulali wala kusinzia. Tunataka ushindi.Tunataka kuendelea kuendelea kushika hatamu. Madaraka matamu jamani. Si rahisi kuyaachia.
Twende kazi
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Kule ambapo bado tunapendwa.Kule ambapo bado wananchi ni 'wetu'. Kule ambapo wananchi wanaamini kuwa Wajumbe wa Nyumba Kumi wana mamlaka kiserikali. Kule ambapo chopa za CHADEMA hazijafika au hazijafika mara nyingi.Kule ambapo tunaweza kusema na wanachi wakafanya bila kuhoji. Mahali pale ambapo kura zahesabiwa na pande nyingi zikiwa na lengo la mshindi yule yule.
Nasi leo hatulali.Tumepewa kazi ya kulinda kura zetu. Zisiibwe. Mimi naelekea Kata ya Magomeni Bagamoyo kwa shughuli za ulinzi. Nitakaa mita mia moja toka mlango wa kituo cha kuhesabia kura.Leo hatulali wala kusinzia. Tunataka ushindi.Tunataka kuendelea kuendelea kushika hatamu. Madaraka matamu jamani. Si rahisi kuyaachia.
Twende kazi
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam