Mkuu umenikumbusha Enzi zile tunacheza mpira wa mchangani Enzi za utoto... kama huna viatu lwako,mwenye njumu sawa, mwenye fwato (viatu vya matairi)sawa, mwenye kuvua shati sawa, yaani kila mtu na anavyojiskia na mpira unachezwa hadi nyuma ya goli...golikipa anabadilishwa kila goli likiingia anabadilishana na mchezaji wa ndani anayembadili ukipa... mwenye mpira tu ndio mbabe...mkimzingua anabeba mpira huyoooo anaondoka zake na mechi inaishia hapo...sanasana mnabadili mchezo, wenye kuruka sarakasi haya, wenye kudaka panzi haya, wenye kurudi makwao haya.... Kweli CCM imenikumbusha mbali maana kumbe bado inacheza ile michezo ya kitoto na ukubwa wote huu