GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
Siku ya jumamosi tarehe 09.06.2012 CCM (M) Dar es salaam ulifanya mkutano wake wa kihistoria ulio hudhuriwa na maelfu lukuki ya watu. Ila katika siku hiyo sikupendezewa na mambo yafuatayo ambayo naweza kusema siku nyingine wasirudie kufanya mkutano kama huo tena.
- Kuweka coverage yakutosha kwa vituo viwili vikubwa vya ITV na TBC kuonyesha LIVE bila chenga, ambapo kila mtu aliona
- Ofisi ya CDM makao makuu siku hiyo ilifungwa kuanzia asubuhi tofauti na kawaida yao ambapo hufunguliwa nakufanya kazi. Wadadisi wa mambo walipo fuatilizia, mlinzi aliyekuwepo alidokeza kwa kusema hujui wenye Dar es salaam leo wanafanya mkutano wao.
- Mpangilio mzuri wa mkutano, yaani : uhamasishaji, uhudhuriaji wa umati wa watu tofauti na mkutano uliopita wa cdm wa kijiumati, mpangilio mzuri wa mkutano , kujibu kwa ufasaha wale wazungumzaji wote kwenye mambo ya msingi na kumaliza mkutano kwa amani na utulivu.
- Ni ukweli usiopingika CC Mina jeshi kubwa na lenye vipaji , kwani mkutanoni waliletwa wanajeshi wachache tu i.e Wassira, Mwakyembe, Maghembe, Tibaijuka na Magufuli. Lakini cheche zake zilisambaa Tanzania nzima. Hii inadhihirisha kuwa wakitawanya jeshi lote, hata sisimizi hawezi kupona.
- Kupendeza kwa uwanja, kwani siku hiyo Dar es salaam nzima ilikuwa kijani na njano. Na hapa ni kuwa uwezo wa vyama vingine kuwahudumia wanachama wao kwa kuwapa promotion material km T-shirt ni mdogo sana na hawawezi, ila wao wameweza. Kwani tumeshuhudia mashirika ya serikali na watu binafsi wakiwatengenezea wateja wao T- shirt kama njia yakujitangaza , CCM wamefanya hivyo , HUSDA ya CDM imejionyesha.
- Mitandao yote ikiwamo JF ilikuwa ni CCM tu inazungumziwa. Japokuwa baadhi ya thread za CCM ziliondolewa kwa sababu zisizo za msingi na MODS. Hii inaleta mushkiri kwenye mustakabali wa JF, kwa za CDM kitu km hicho ni nadra sana kutokea. Tujirekebishe , heshima yetu mbele ya jamii inazidi kuyeyuka km theluji ya mlima Kilimanjaro kwa mambo kama haya.