CCM mnawakomoa wananchi, sio UKAWA!

CCM mnawakomoa wananchi, sio UKAWA!

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
25,995
Reaction score
25,388
Kitendo cha serikali ya CCM kuyapa kisogo majimbo yanayowakilishwa na UKAWA kinalenga kuwakomoa wananchi zaidi. Ipo mifano hai ya serikali kutoshughulikia kikamilifu miradi ya maendeleo iliyopo kwenye majimbo yanayoongozwa na wabunge wa upinzani ili kuwajengea wananchi dhana hasi kwamba wapinzani hawana lolote. Sina haja ya kuyataja majimbo hayo kwani yanajulikana wazi kwa kila mtanzania mwenye akili zilizotimia.

Kwa akili zao finyu wanadhani kwamba majimbo hayo yakikosa maendeleo wananchi watarejesha mioyo yao kwa CCM kumbe ndio wanazidi kujichimbia kaburi. Kila mtu ni shahidi jinsi wabunge wa UKAWA wanavyohangaika kuwaletea wananchi maendeleo lakini wanakosa ushirikiano kutoka serikali ya CCM. Kudhani kwamba kuwanyima wananchi maendeleo kutawafanya wawachukie UKAWA ni sawa na kuota ndoto ya mchana. Wananchi wa leo ni tofauti sana na wale wa enzi za "Zidumu fikra za Mwenyekiti".

CCM mkae mkijua kuwa kadri mnavyowanyima wananchi maendeleo ndio mnazidi kujichimbia kaburi la uongozi wa nchi.

:israel:
 
Kwani hao Wabunge wa upinzani si walisema kuwa watawaletea maendeleo wananchi? Inakuwaje wanaiangukia CCM?
 
Nawashauri wabunge wote wanaonyimwa miradi ya maendeleo kwa hila wawaeleze wananchi wao kinagaubaga na ikibidi wawatake wasilipe kodi, full stop. Kodi wanalipa wananchi wote na sio wanachama wa ccm tu.Tena ni lazima watoe hela ya maendeleo na wala sio ombi vinginevyo hakuna kulipa kodi.
 
Msituchanganye bana. Mnyika alisema kuwa ataleta maji Ubungo. Wala hakusema kuwa ataishirikisha serikali ya CCM kutekeleza hilo. Kama kazi imewashinda rudisheni majimbo kwa CCM
 
Nawashauri wabunge wote wanaonyimwa miradi ya maendeleo kwa hila wawaeleze wananchi wao kinagaubaga na ikibidi wawatake wasilipe kodi, full stop. Kodi wanalipa wananchi wote na sio wanachama wa ccm tu.Tena ni lazima watoe hela ya maendeleo na wala sio ombi vinginevyo hakuna kulipa kodi.
Mkuu, kuna fedha za mfuko wa jimbo ambazo zinasimamiwa na mbunge. Je wanazitumiaje?
 
Kumbe alisema ss pesa iliyopo serikalini kwani ni ya ccm au ya kwetu. Mbona kikwete alisema ataleta meli ziwa Victoria mpk leo hatujaiona mbaya zaidi na iliyopo ni mbovu.
 
Kwani hao Wabunge wa upinzani si walisema kuwa watawaletea maendeleo wananchi? Inakuwaje wanaiangukia CCM?

Kuwa muelewa. kama hujui jambo ni bora ukauliza kwanza. maendeleo huletwa na KODI na kodi hizi hukusanywa na serikali ya CCM. kazi ya mbunge ni kusimamia matumizi ya kodi za WANANCHI. kitendo cha serikali kukusanya kodi kutoka kwa wananchi wote (bila ubaguzi) na kuzitumia KIBAGUZI na kifisadi litakizika chama chenu na serikali yenu mnamo Oktoba. kama serikali haitaki kupeleka maendeleo kwenye majimbo ya UKAWA, basi iwaachie UKAWA wakusanye kwenye kodi kwenye majimbo yao na kuzitumia kwenye majimbo husika kwa manufaa ya walipakodi. je, wewe unaona serikali iko fair katika hili?
 
Kuwa muelewa. kama hujui jambo ni bora ukauliza kwanza. maendeleo huletwa na KODI na kodi hizi zinakusanywa na serikali ya CCM. kazi ya mbunge ni kusimamia matumizi ya kodi za WANANCHI. kitendo cha serikali kukusanya kodi kutoka kwa wananchi wote (bila ubaguzi) na kuzitumia KIBAGUZI na kifisadi litakizika chama chenu na serikali ya mnamo Oktoba. kama serikali haitaki kupeleka maendeleo kwenye majimbo ya UKAWA, basi iwaachie UKAWA wakusanye kwenye majimbo yao na kuzitumia kwenye majimbo husika. je, wewe unaona serikali iko fair katika hili?
Waulize hao Wabunge wako fedha wanazopewa za mfuko wa Jimbo wanazitumiaje
 
Msituchanganye bana. Mnyika alisema kuwa ataleta maji Ubungo. Wala hakusema kuwa ataishirikisha serikali ya CCM kutekeleza hilo. Kama kazi imewashinda rudisheni majimbo kwa CCM

wewe ni zombie kabisa. kama ni hivyo basi CCM acheni kukusanya kodi kwenye jimbo la UBUNGO na badala yake muwaachie UKAWA wakusanye na kuwahudumia wananchi wa majimbo yao. hivi wewe unajua source ya mapato ya serikali au unaropoka tu? ndio maana unaitwa Panya Road...akili zako ni sawa na za PANYA!
 
Last edited by a moderator:
Kwani hao Wabunge wa upinzani si walisema kuwa watawaletea maendeleo wananchi? Inakuwaje wanaiangukia CCM?

Kwa akili yako tu finyu mbunge ni nani ktk jammi na anapata je fulsa ya maendeleo?kama cyo gvmrnt……(ww inawrzekana ni kantanana)
 
Mkuu, kuna fedha za mfuko wa jimbo ambazo zinasimamiwa na mbunge. Je wanazitumiaje?

Fedha za mfuko wa jimbo ndizo zinajenga barabara, miundombinu ya maji, kujenga maabara na kila kitu? kama kazi yake ni hiyo, sasa kuna haja gani ya wananchi kuchangishwa fedha za maabara? ama kweli humu jf kuna mimburura mingi sana. wakuu BAK lusungo Mamndenyi, Elli, et al hebu piteni huku mnisaidie kutoa elimu ya uraia. kuna watu huku hawajui jinsi serikali inavyopata mapato yake na matumizi yake.
 
Last edited by a moderator:
Msituchanganye bana. Mnyika alisema kuwa ataleta maji Ubungo. Wala hakusema kuwa ataishirikisha serikali ya CCM kutekeleza hilo. Kama kazi imewashinda rudisheni majimbo kwa CCM

Hatu wez jua labda hazipo zote makund matatu ww
 
Fedha za mfuko wa jimbo ndizo zinajenga barabara, miundombinu ya maji, kujenga maabara na kila kitu? kama kazi yake ni hiyo, sasa kuna haja gani ya wananchi kuchangishwa fedha za maabara? ama kweli humu jf kuna mimburura mingi sana. wakuu BAK lusungo Mamndenyi, Elli, et al hebu piteni huku mnisaidie kutoa elimu ya uraia. kuna watu huku hawajui jinsi serikali inavyopata mapato yake na matumizi yake.
Mkuu, tutajie basi matumizi ya fedha za mfuko wa Jimbo
 
mwambieni mnyika tunataka maji ubungo alisema ndani ya mwezi mmoja akichaguliwa ataleta maji ubungo yako wapi sasa hayo maji aliyosema mnyika.
 
Fedha za mfuko wa jimbo ndizo zinajenga barabara, miundombinu ya maji, kujenga maabara na kila kitu? kama kazi yake ni hiyo, sasa kuna haja gani ya wananchi kuchangishwa fedha za maabara? ama kweli humu jf kuna mimburura mingi sana. wakuu BAK lusungo Mamndenyi, Elli, et al hebu piteni huku mnisaidie kutoa elimu ya uraia. kuna watu huku hawajui jinsi serikali inavyopata mapato yake na matumizi yake.

kwani kwa mawazo yako pesa ya mfuko wa jimbo inafanya kazi gani.
 
Waulize hao Wabunge wako fedha wanazopewa za mfuko wa Jimbo wanazitumiaje

fedha za mfuko wa jimbo ndio zinatekeleza miradi yote ya maendeleo katika jimbo? na bajeti ya serikali inayotengwa kila mwaka inafanya kazi gani? kazi yake ni kuliwa na mafisadi wa CCM?

CC gsu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom