CCM mnatia shaka

CCM mnatia shaka

Kwa hiyo ukisusa wewe kwa kuwa ni wachache basi walio wengi wasiendelee na shughuli zao? wewe punguani kweli kweli.

Kwa bahati mbaya na wewe niliyekutegemea umeangukia kwenye udhaifu uleule wa wanaccm wote. Kujibu maswali na kujenga hoja imekuwa ni tatizo kubwa na matokeo yake ndio hapo jeshi la polisi kutumika kupiga watanzania wenye mtazamo tofauti na ccm. Hukuwa na haja ya kutukana na tena kutukana kwenyewe bora ungejenga hoja wangalau kidogo wa utetezi wa baadhi ya maswali yenye utata. Na kwa bahati mbaya sio wewe, rais, au mjumbe yoyote wa BMK kasoro wa kura za hapana anayejenga hoja kwenye maeneo hayo yenye maswali lukuki. Haya mama kwa jinsi ulivyoitetea katiba pendekezwa nimeamini ni nzuri sana.
 
Kwa bahati mbaya na wewe niliyekutegemea umeangukia kwenye udhaifu uleule wa wanaccm wote. Kujibu maswali na kujenga hoja imekuwa ni tatizo kubwa na matokeo yake ndio hapo jeshi la polisi kutumika kupiga watanzania wenye mtazamo tofauti na ccm. Hukuwa na haja ya kutukana na tena kutukana kwenyewe bora ungejenga hoja wangalau kidogo wa utetezi wa baadhi ya maswali yenye utata. Na kwa bahati mbaya sio wewe, rais, au mjumbe yoyote wa BMK kasoro wa kura za hapana anayejenga hoja kwenye maeneo hayo yenye maswali lukuki. Haya mama kwa jinsi ulivyoitetea katiba pendekezwa nimeamini ni nzuri sana.

Mtazamo wako ulio tofauti unatazamwa lakini hautekelezwi kwa kuwa katika demokrasia ni; wengi wape wachache wasikilize. Na naam Kikwete amekuwa msikivu sana, au hukumbuki vyama vya upinzani vya wachache vinapokaribishwa Ikulu kusikilizwa? nikupe ushahidi?
 
Mtazamo wako ulio tofauti unatazamwa lakini hautekelezwi kwa kuwa katika demokrasia ni; wengi wape wachache wasikilize. Na naam Kikwete amekuwa msikivu sana, au hukumbuki vyama vya upinzani vya wachache vinapokaribishwa Ikulu kusikilizwa? nikupe ushahidi?

Nashukuru kwa jibu lako, nimefurahi muda huu umejitahidi kutokuleta matusi bali kujibu hoja. Je sasa unaweza kunisaidia majibu ya yale maswali yangu ya msingi kule nyuma uliponijibu kwa jazba kidogo. Na kusherehesha hayo majibu yangu utaniwekea huo ushahidi unaotoka kunionyesha usikivu wa Kikwete ambao bila hata kuniambia najua na ninakubali anao. Hapo sasa nitakwenda na wewe kwenye ile kona ambao huwakimbiza wanaccm wasipopataka kwenye midahalo huru na kwa kiasi kikubwa ndipo tatizo letu kubwa la msingi. Ukiweza kunijibu leo nitafurahi ukishindwa leo nijibu tu nitaona kwenye notification.
 
Kwako wewe katiba nzuri eti mpaka iwe na serikali tatu ukawa ujuha huu sijui mtafika nao wapi.

Acha kujitoa fahamu wewe! Jaribu kusoma uchambuzi na mawazo ya wenzako siyo unakurupuka tu kama umepagawa na pepo.
 
Kwanza waulize viongozi wako wanaojiita ukawa wana maana gani kuwaambia wananchi wapige kura ya hapana ndio utaelewa kwa nini na sisi tunawaambia wananchi wapige kura ya ndiyo.... Hao wanaowaambia muikatae wamewaletea mkaisoma???? sasa kimuhemuhe cha nini kwa nini usiwe na saburi ukasubiri ukaipata ukajisomea halafu ndio ukaamua uchukue ya ukawa au uchukue ya wazalendo waliokuandikia na kukuingizia yale yote ambayo kijana au mzee wa leo anayahitaji na sio serikali tatu kama wanavyong'ang'ania
Ndugu wana-jf,ninajiuliza maana ya kauli hizi za viongozi wa ccm ikiongozwa na Rais,pale aliposema"KATIBA HII NI NZURI WANANCHI MUIPIGIE KURA YA NDIO".hii inatoa tafsiri gani?

Nijuavyo mimi katiba pendekezwa inatakiwa iletwe kwa Wananchi,kila mmoja apewe nakala yake na apate muda wa kisoma ili aweze kutoa maamuzi sahihi. Sasa nawauliza viongozi wa CCM mnaopanda majukwaani na kuipigia debe katiba pendekezwa; mnadhani mnafanya sahihi wakati bado hata wananchi hawajaisoma? Swali linakuja; Kwani mnawasiwasi gani mpaka mnaanza kuipigia debe katiba hiyo ikiwa kama imezingatia maoni yaliyotolewa na wananchi?

Nawaombeni sana,Tanzania ya mwaka 1977 sio Tanzania ya leo!mmezoea kudanganyadanganya umma bila kutumia akili sasa mnaishia kubaya! Tumieni japo akili ili muendelee kijenga heshima ya Taifa letu kwani Tanzania si ya Chama chochote bali ni ya Watanzania.
 
Kwanza waulize viongozi wako wanaojiita ukawa wana maana gani kuwaambia wananchi wapige kura ya hapana ndio utaelewa kwa nini na sisi tunawaambia wananchi wapige kura ya ndiyo.... Hao wanaowaambia muikatae wamewaletea mkaisoma???? sasa kimuhemuhe cha nini kwa nini usiwe na saburi ukasubiri ukaipata ukajisomea halafu ndio ukaamua uchukue ya ukawa au uchukue ya wazalendo waliokuandikia na kukuingizia yale yote ambayo kijana au mzee wa leo anayahitaji na sio serikali tatu kama wanavyong'ang'ania
Wale wanaowataka wananchi waipigie kura ya HAPANA hiyo katiba wanaeleza mapungufu yake ambayo hayana shaka hata kidogo kuyaelewa. Hivi kama katiba pendekezwa imetaja 50% kwa 50%,umilikaji wa ardhi kwa wanawake,haki za wakulima,wasanii,vyombo vya habari nk lakini wakaweka katazo la kudai au kuhoji haki hizo mahakamani au katika chombo chochote cha sheria,hiyo ni haki? Au kwako kumzuia mtu kikatiba kudai haki yake huo ndio UZALENDO? Bado safari ni ndefu.
 
Umeshajiuliza na UKAWA kwanini wanasema katiba hii si nzuri na kuwaambia wananchi wapige kura ya hapana?

Unatia aibu kama hujui Sitta na Chenge wame -rape katiba ya wananchi unatia aibu
 
Ndugu zangu acheni hasira!tusimamie kwenye ukweli wenyewe;mimi nasema ccm inatumia mabavu kuipitisha katiba iliyopendekezwa,kwa nini ccm wanaonekana na wasiwasi hii inatokana na nini kama hakuna (NYUMA YA PAZIA)haraka hii inasababishwa na nini?
 
Yaani kweli mnajiaibisha hamna cha kutetea kwenye katiba kwa hoja dhidi ya jazba na kejeli. Ndio maana mnasema watu wasisomewe waelewe wenyewe lakini nyinyi mnataja vifungu kama haki za wakulima, wafugaji, wasanii nk, kama gia ya kuwachanganya wananchi wenye uelewa mdogo. Nilitarajia ungetoa ufafanuzi wa hizo haki na wapi katiba pendekezwa inataja wataweza kuzidai. Halafu sio wewe tu ambaye umepewa jukumu humu jamvini kutetea hiyo aibu bali hata hao wajumbe wa BMk hawajitokezi kutoa ufafanuzi wa haya maswali, bali wamebaki kusema katiba ni nzuri sana imewalenga wananch, na udhaifu huu wa kuitetea hii aibu na hila ya ccm uko kwenu wote kuanzia Rais, wajumbe wote wa Bmk kasoro wa kura za hapana hawatoi ufafanuzi wa vifungu hivi mnavyoita vizuri. Sasa kama ni vizuri na hamuwezi kuvitolea ufafanuzi je hivyo vibaya itakuwaje. Andaeni jeshi kupiga watz kupitisha huu upuuzi maana hautapita kwa utashi wa wananchi.

Kwa kuongezea ungemkumbusha simiyu yetu ule wimbo wa CCM kuwa 'chama cha wakulima na wafanyakazi' umebadilishaje maisha ya wakulima na wafanyakazi zaidi ya miaka 50 sasa - kama sio kuwashibisha wenye chama wenyewe tu (watawala)? Ndio haya haya ya katiba inyopendekezwa inajali haki za wasanii, wavuvi, wakulima, wachangudoa, nk. Hapa ndipo ninawavulia kofia watawala kwa kucheza na akili za watanganyika mbumbumbu.
 
Hata kusema wananchi wakaisome bado ni uhuni na ulaghai,mie ninapoishi hakuna mwananchi wa kawaida ameiona hata hiyo mbovu iliyolazimishwa kupita,wengine hawajuhi hata zinapatikana wapi,hakuna matangazo wala nini ila chanjo ya rubela inatangazwa mpaka chooni lakini katiba zinapatikana wapi ahahaa.Pili tusijidanganye,kuielewa vilivyo ni zaidi ya kuisoma gazeti la kiu ama hadithi za abunuwasi,sasa huko vijijini ni watanzania wa aina gani na kiwango kipi wataweza kusoma ibara zote 19 na kuzielewa kimantiki? ccm wanawasakizia wananchi kwa kisingizio cha waisome huku wakijua fika watanzania wengi ni kayumba,tunawaomba ukawa muitafsiri katiba kwenye mikutano yenu ili wananchi waielewe
 
Hakuna ambae hiyo title ya Umarehemu ataiepuka.

Kama huna hoja katika mambo mengine, nakushauri uwe msomaji badala ya kuandika utumbo.

Faiza hoja yangu ni kuwa ilikuwaje marehemu akapiga kura? utumbo ni marehemu kupiga kura au mimi kuhoji, hebu nifafanulie wewe mwenye hoja.
 
Hakuna katazo kama hilo...huo ni uzushi wako tu...baada ya katiba ambayo ndiyo seria mama kinachofuata ni kutungwa kwa sheria na kanuni ambazo ndio mwongozo wa masuala yote...Hayo makatazo ni hadithi za lissuslaa na sio za waliobobea kama akina profesa na madokta waliojaa kwenye bunge maalum.
Wale wanaowataka wananchi waipigie kura ya HAPANA hiyo katiba wanaeleza mapungufu yake ambayo hayana shaka hata kidogo kuyaelewa. Hivi kama katiba pendekezwa imetaja 50% kwa 50%,umilikaji wa ardhi kwa wanawake,haki za wakulima,wasanii,vyombo vya habari nk lakini wakaweka katazo la kudai au kuhoji haki hizo mahakamani au katika chombo chochote cha sheria,hiyo ni haki? Au kwako kumzuia mtu kikatiba kudai haki yake huo ndio UZALENDO? Bado safari ni ndefu.
 
Wewe ulikuwepo wakati amrehemu akipiga kura?? au ni yale mnayoyadaka tu kutoka vinywani mwa lissuslaa? Huwezi mdanganya hata mtoto wa chekechea kuwa marehemu alipiga kura na ikahesabiwa....fungua tovuti ya BMK na utaona kura zote zilivyopigwa na hapo utatuambia marehemu ni nani kati ya hao waliopiga kura
Faiza hoja yangu ni kuwa ilikuwaje marehemu akapiga kura? utumbo ni marehemu kupiga kura au mimi kuhoji, hebu nifafanulie wewe mwenye hoja.
 
Msipoangalia hiyo katiba haitasambazwa kwa wananchi kwa mkusudi kabisa wanaogopa wanajua vijana wameshituka na wataisoma ndo maana presidaa ameanza kupiga debe mapema.
 
Wewe ulikuwepo wakati amrehemu akipiga kura?? au ni yale mnayoyadaka tu kutoka vinywani mwa lissuslaa? Huwezi mdanganya hata mtoto wa chekechea kuwa marehemu alipiga kura na ikahesabiwa....fungua tovuti ya BMK na utaona kura zote zilivyopigwa na hapo utatuambia marehemu ni nani kati ya hao waliopiga kura

Na yule wa Zenji ambaye hakupiga kura lakini jina lake likawemo kwenye orodha unaliteteaje? we tuyaache ndugu...
 
Typographic error....na hakuhesabiwa bali jina lake lilionekana kwenye orodha....kama angehesabiwa basi kura zingezidi
Na yule wa Zenji ambaye hakupiga kura lakini jina lake likawemo kwenye orodha unaliteteaje? we tuyaache ndugu...
 
Faiza hoja yangu ni kuwa ilikuwaje marehemu akapiga kura? utumbo ni marehemu kupiga kura au mimi kuhoji, hebu nifafanulie wewe mwenye hoja.

Marehemu wengi sana wameshapiga kura walipokuwa hai na kura zao huhesabiwa hata kama wamekufa/

Unafikiri wapiga kura wote wa Tanzania wanakuwa hai zinapohesabiwa kura, hakuna anaekufa? fikiri!
 
Marehemu wengi sana wameshapiga kura walipokuwa hai na kura zao huhesabiwa hata kama wamekufa/

Unafikiri wapiga kura wote wa Tanzania wanakuwa hai zinapohesabiwa kura, hakuna anaekufa? fikiri!

Sawa bibie, kura zilitoshelezeshwa naona, nimekusoma
 
Back
Top Bottom