CCM mnatia shaka

CCM mnatia shaka

Katiba hii ni ya wananchi. Lazima ipigiwe kura ya ndio ipite
ifweero unasema katiba hii lazima ipite, una maana gani wakati wananchi hawajapiga kura ya maoni?

Au maccm ndiyo mnataka kutumia filosofia yenu mpya, kama ile mliyoitumia kwenye bunge la katiba, wakati mlipolazimisha akidi kwa upande wa Zanzibar, ili muipitishe katiba ya Sitta/Chenge katika kile kinachojulikana siku hizi kama kura zisipotosha ni lazima zitatoshelezwa?!
 
Kwahiyo wewe unataka nini,usitumie neno wazanzibar tena koma kabisa sema wewe na chagadema yako hakuna mzanzibar anayepinga katiba inayopendekezwa ukiacha malimu sefu ambaye ni wakala wa sultani wengi wote wanaiunga mkono katiba.

hahahajahahahahahahahahahahahahahahahahahahaha!umekosa cha kuandika juha!
 
Katiba hii ni ya wananchi. Lazima ipigiwe kura ya ndio ipite

Wananchi wepi hao? Unaongelea yale mafisadi yaliyoandika hicho kipeperushi ndio wananchi? Katiba ya wananchi ni ile tu itakayozingatia maoni yao kama yalivyokuwa katika rasimu ya pili na si hii iliyoyafinyanga,kuyabadili na kuyapindua ili tu yalinde mfumo fisadi na mafisadi.
 
Mkuu ungependa uletewe wapi hiyo katiba mbona watu wenye nia nayo karibu wote wanayo unataka ine nyumbani kwako ukiwa umekaa sebuleni au unatakaje,kwahiyo kwako wewe katiba isipogawiwa ndiyo inakuwa mbovu watu wengine kazi kweli.

Haramu Hata0isifiwe Namna Gani,itaendelea kuwa haramu tu! Mambo mengi mazuri yamenyofolewa ili kulinda mfumo fisadi ndio maana haina meno!
 
Kwahiyo wewe unataka nini,usitumie neno wazanzibar tena koma kabisa sema wewe na chagadema yako hakuna mzanzibar anayepinga katiba inayopendekezwa ukiacha malimu sefu ambaye ni wakala wa sultani wengi wote wanaiunga mkono katiba.

Jibu hoja acha kutokwa povu!
 
Katiba hii ni ya wananchi. Lazima ipigiwe kura ya ndio ipite

Kumbe ni kwa lazima sio hiari naona ccm mnaipeleka hii nchi huku
amaniiiiiii.jpg amani1.jpg
 
Uliishia darasa la ngapi? Au ushabiki maandazi umekufilisi akili kiasi hicho? Pole sana

Darasa langu hulipati hata ufanye nini, wakati sisi tunaanza chuo kabla ya primary nyinyi hamjui hata maana ya chuo ni nini.

Mimi ni Mtanzania wa kwanza, na sijui kama kuna mwingine baada yangu, kusoma (BNR) Bell Northern Research, Canada. Nioneshe mwingine kama yupo nijuane nae.
 
Kwa kua imeacha maoni yetu wananchi yaliyokuwemo ktk rasimu ya 2 iliyowasilishwa BMK

Na BMK ilikuwa ni wawakilishi wa wananchi.

Kama mlitaka maoni ndio yawe katiba kwanini mlikubali liwepo Bunge Maalum La Katiba?

Na hiy Katiba si inarudishwa kwa wananchi kupigiwa kura? kama huitaki si unasema hapana na wanayoittaka wanasema ndiyo! wakishinda wa hapana itakuwa hakuna katiba mpya mpaka iandikwe upya na wakishinda wa ndiyo, hapo ndiyo hauna ujanja uliyesema hapana, kwani demokrasia ndivyo ilivyo, wengi wape wachache wasikilize.
 
Wao wailete tuisome,na wajue tunajua namna ya kuisoma.

Tunachukua ile tuliyomuambia waryoba aandike tunaiweka mkono wa kulia,alafu na hiyo ya sasa mkono wa kushoto,alafu kalamu mkononi tunaanza ku cross read,kifungu kwa kifungu penye tofauti tunarudi kwenye randama ambazo zitakuwa mbele yetu.tunaangalia basis ya mabadiriko kama namna tulivyopendekeza.

.
 
Na BMK ilikuwa ni wawakilishi wa wananchi.

Kama mlitaka maoni ndio yawe katiba kwanini mlikubali liwepo Bunge Maalum La Katiba?

Na hiy Katiba si inarudishwa kwa wananchi kupigiwa kura? kama huitaki si unasema hapana na wanayoittaka wanasema ndiyo! wakishinda wa hapana itakuwa hakuna katiba mpya mpaka iandikwe upya na wakishinda wa ndiyo, hapo ndiyo hauna ujanja uliyesema hapana, kwani demokrasia ndivyo ilivyo, wengi wape wachache wasikilize.

Mama shikamoo,naomba unisaidie kitu kimoja, unaweza kutuwekea majina ya BMk wote idadi na majina yao hapa kabla ya bunge kuanza tena ukiweza utenge wale wa bara na znz? Inaonekana watz hawajui hesabu ndio maana hata akidi inawachanganya, upigwaji wa hiyo kura huko kwa wananchi utasimamiwa na tume ya aina gani? Na hiyo tume itatumia mfumo uleule wa S. 6 kupata matokeo? Yaani kura ya hapana ikishinda itaundwa kamati ya maridhiano na wananchi wa hapana ama kura ya ndio itajaziwa na marehemu wa nchi hii akiwepo baba wa taifa? Je watakaopiga kura ya hapana mtawapa adhabu gani maana AG wa znz mmefukuza kazi, je wananchi wa kura ya hapana mtawafukuza nchini ama adhabu gani?

Kwa umri wako nategemea utaweza kutetea vifungu vyenye utata, eti ni kweli katiba hii imewajali sana wananchi kama wakulima, wafugaji, wasanii nk lakini hawatakuwa na nguvu ya kuwawajibisha viongozi kupata haki hizo? Hii 50/50 kwenye uwakilishi ina tija sana? Na mpaka sasa hivi hatujafikia 50/50 kwa sababu katiba ya zamani iliweka 80% wanaume na wanawake 20%? Je tukisema mliojipa wajibu wa kuandika katiba mlibeba jukumu kwa hila na msiloliweza tutakuwa tunakosea? Mama wewe nakuaminia utaweza kujibu maswali yangu maana hao waliokuwa wajumbe wa BMK hatuwaoni wakitoa ufafanuzi zaidi ya kusema hii ni katiba ya wananchi ipigiwe kura ya ndio.
 
Katiba hii ni ya wananchi. Lazima ipigiwe kura ya ndio ipite

Kama KATIBA ni ya Wananchi basi ni hao hao ndio wenye hiyari ya kufanya nini wanataka maana zile pesa mlizolipwa wakati mnafanya upuuzi kule mjengoni na kufikia hata kucheza nadhani ndio mnazotaka kuwahadaa nazo raia ili wapige KURA ya NDIO mjue mmeumia maana huu upuuzi wenu wa kufikiria kuwa kila siku ni kama jana ndio itawa-cost haswaaaa na hatutaikubali kamwe
 
Wao wailete tuisome,na wajue tunajua namna ya kuisoma.

Tunachukua ile tuliyomuambia waryoba aandike tunaiweka mkono wa kulia,alafu na hiyo ya sasa mkono wa kushoto,alafu kalamu mkononi tunaanza ku cross read,kifungu kwa kifungu penye tofauti tunarudi kwenye randama ambazo zitakuwa mbele yetu.tunaangalia basis ya mabadiriko kama namna tulivyopendekeza.

.
Ufanyike mkakati maalum wa kuisambaza upya rasimu ya Warioba .
 
1.asilimia 50 ya wanawake na wanaume ktk madaraka hususan ktk siasa
2. haki za wakulima,wafugaji kutambuliwa rasmi kikatiba hatua itakayosaidia kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji na kuwawezesha kupata mikopo na kuboresha kilimo na ufugaji wao.
3. rais wa zanzibar kuwa makam wa rais hatua itakayoimarisha muungano mara dufu
4.uhuru wa vyombo vya habari kutambuliwa rasmi kisheria na zaidi haki za wasanii
1. 50/50 hata kama wanawake wenye sifa hawatoshi tutawapa hawara zetu wanaojua kusoma na kuandika
2. Haki za wakulima,wafugaji,wasanii lakini hawaruhusiwi kwenda mahakamani kuzidai hivyo watazipata watawala wakipenda
3. rais wa zanzibar kutawala tanganyika wakati watanganyika hawakushiriki kumchagua
4.Uhuru hewa wa vyombo vya habari na haki hewa za wasanii kama ilivyo kwa wakulima na wafugaji
Ifike mahali tuubali ukweli kuwa watawala hawawezi kukubali kupitisha sheria zinazowabana ndio maana wamenyonga maoni ya wananchi
 
Mama shikamoo,naomba unisaidie kitu kimoja, unaweza kutuwekea majina ya BMk wote idadi na majina yao hapa kabla ya bunge kuanza tena ukiweza utenge wale wa bara na znz? Inaonekana watz hawajui hesabu ndio maana hata akidi inawachanganya, upigwaji wa hiyo kura huko kwa wananchi utasimamiwa na tume ya aina gani? Na hiyo tume itatumia mfumo uleule wa S. 6 kupata matokeo? Yaani kura ya hapana ikishinda itaundwa kamati ya maridhiano na wananchi wa hapana ama kura ya ndio itajaziwa na marehemu wa nchi hii akiwepo baba wa taifa? Je watakaopiga kura ya hapana mtawapa adhabu gani maana AG wa znz mmefukuza kazi, je wananchi wa kura ya hapana mtawafukuza nchini ama adhabu gani?

Kwa umri wako nategemea utaweza kutetea vifungu vyenye utata, eti ni kweli katiba hii imewajali sana wananchi kama wakulima, wafugaji, wasanii nk lakini hawatakuwa na nguvu ya kuwawajibisha viongozi kupata haki hizo? Hii 50/50 kwenye uwakilishi ina tija sana? Na mpaka sasa hivi hatujafikia 50/50 kwa sababu katiba ya zamani iliweka 80% wanaume na wanawake 20%? Je tukisema mliojipa wajibu wa kuandika katiba mlibeba jukumu kwa hila na msiloliweza tutakuwa tunakosea? Mama wewe nakuaminia utaweza kujibu maswali yangu maana hao waliokuwa wajumbe wa BMK hatuwaoni wakitoa ufafanuzi zaidi ya kusema hii ni katiba ya wananchi ipigiwe kura ya ndio.

Kwa hiyo ukisusa wewe kwa kuwa ni wachache basi walio wengi wasiendelee na shughuli zao? wewe punguani kweli kweli.
 
Back
Top Bottom