CCM mnatia shaka

CCM mnatia shaka

MAKASSY

Member
Joined
Jan 16, 2013
Posts
95
Reaction score
26
Ndugu wana-jf,ninajiuliza maana ya kauli hizi za viongozi wa ccm ikiongozwa na Rais,pale aliposema"KATIBA HII NI NZURI WANANCHI MUIPIGIE KURA YA NDIO".hii inatoa tafsiri gani?

Nijuavyo mimi katiba pendekezwa inatakiwa iletwe kwa Wananchi,kila mmoja apewe nakala yake na apate muda wa kisoma ili aweze kutoa maamuzi sahihi. Sasa nawauliza viongozi wa CCM mnaopanda majukwaani na kuipigia debe katiba pendekezwa; mnadhani mnafanya sahihi wakati bado hata wananchi hawajaisoma? Swali linakuja; Kwani mnawasiwasi gani mpaka mnaanza kuipigia debe katiba hiyo ikiwa kama imezingatia maoni yaliyotolewa na wananchi?

Nawaombeni sana,Tanzania ya mwaka 1977 sio Tanzania ya leo!mmezoea kudanganyadanganya umma bila kutumia akili sasa mnaishia kubaya! Tumieni japo akili ili muendelee kijenga heshima ya Taifa letu kwani Tanzania si ya Chama chochote bali ni ya Watanzania.
 
Umeshajiuliza na UKAWA kwanini wanasema katiba hii si nzuri na kuwaambia wananchi wapige kura ya hapana?
 
...ukionahivyo ujue yanapanga ufisadi,ngoja nikaicheki vizuri maana haki ya kumiliki ardhi kwa mwanamke kuna kifungu kinasema hawezi kuidai mahakamani,so ni kama haipo,em cheki uhuni huo...
 
Umeshajiuliza na UKAWA kwanini wanasema katiba hii si nzuri na kuwaambia wananchi wapige kura ya hapana?

Yes ukawa wanasema ipigwe kura ya hapana since mawazo yaliyokusanywa kwa wananchi yametupiliwa mbali hususani tunu za taifa zinazolinda maadili ya viongozi, pia ni rasimu ni batili since akidi haikutimia baada ya sitta kuforge hadi majina ya waliokufa.
 
Katiba hii ni ya wananchi. Lazima ipigiwe kura ya ndio ipite
 
Ndugu wana-jf,ninajiuliza maana ya kauli hizi za viongozi wa ccm ikiongozwa na Rais,pale aliposema"KATIBA HII NI NZURI WANANCHI MUIPIGIE KURA YA NDIO".hii inatoa tafsiri gani?nijuavyo mimi katiba pendekezwa inatakiwa iletwe kwa Wananchi,kila mmoja apewe nakala yake na apate muda wa kisoma ili aweze kutoa maamuzi sahihi.Sasa nawauliza viongozi wa CCM mnaopanda majukwaani na kuipigia debe katiba pendekezwa;mnadhani mnafanya sahihi wakati bado hata wananchi hawajaisoma?swali linakuja;Kwani mnawasiwasi gani mpaka mnaanza kuipigia debe katiba hiyo ikiwa kama imezingatia maoni yaliyotolewa na wananchi?nawaombeni sana,Tanzania ya mwaka 1977 sio Tanzania ya leo!mmezoea kudanganyadanganya umma bila kutumia akili sasa mnaishia kubaya!Tumieni japo akili ili muendelee kijenga heshima ya Taifa letu kwani Tanzania si ya Chama chochote bali ni ya Watanzania.
Hang over imekunyima usingizi ukakurupukia key board
 
Wewe hujui kuelewa hadi uambiwe na UKAWA? Hata baada ya kuambiwa bado huelewi kwamba katiba hiyo ni mbovu sana kwa wananchi?. UKAWA ni umoja na kutetea katiba ya wananchi siyo chama cha siasa kama ccm. Jfunze kutofautisha.

Good morning lakini?

Umeshajiuliza na UKAWA kwanini wanasema katiba hii si nzuri na kuwaambia wananchi wapige kura ya hapana?
 
Niambie mambo matatu ambayo ni mazuri na mapya ambayo hayakuwemo kwenye katikba ya 1977, na mimi nitakuambia mambo 10 yanayoifanya katiba mpya pendekezwa isitahilishe sita na tume yake kufunguliwa mashitaka ya ugaidi.

Naomba uje na majibu si matusi na ushabiki


Katiba hii ni ya wananchi. Lazima ipigiwe kura ya ndio ipite
 
Yes ukawa wanasema ipigwe kura ya hapana since mawazo yaliyokusanywa kwa wananchi yametupiliwa mbali hususani tunu za taifa zinazolinda maadili ya viongozi, pia ni rasimu ni batili since akidi haikutimia baada ya sitta kuforge hadi majina ya waliokufa.
Ukawa imeshakufa imebaki kutapatapa na urais
 
Niambie mambo matatu ambayo ni mazuri na mapya ambayo hayakuwemo kwenye katikba ya 1977, na mimi nitakuambia mambo 10 yanayoifanya katiba mpya pendekezwa isitahilishe sita na tume yake kufunguliwa mashitaka ya ugaidi.

Naomba uje na majibu si matusi na ushabiki
1.asilimia 50 ya wanawake na wanaume ktk madaraka hususan ktk siasa
2. haki za wakulima,wafugaji kutambuliwa rasmi kikatiba hatua itakayosaidia kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji na kuwawezesha kupata mikopo na kuboresha kilimo na ufugaji wao.
3. rais wa zanzibar kuwa makam wa rais hatua itakayoimarisha muungano mara dufu
4.uhuru wa vyombo vya habari kutambuliwa rasmi kisheria na zaidi haki za wasanii
 
Mkuu ungependa uletewe wapi hiyo katiba mbona watu wenye nia nayo karibu wote wanayo unataka ine nyumbani kwako ukiwa umekaa sebuleni au unatakaje,kwahiyo kwako wewe katiba isipogawiwa ndiyo inakuwa mbovu watu wengine kazi kweli.
 
Kabla sijaendelea:-

1. Hiyo asilimia 50 kwa hamsini inatija gani katika maendeleo ya taifa? Unaelewa maana na tafsiri yake halisi hasa ukizingatia viwango vye elimu ya Tanzania kwa sasa?

2. Kutajwa kwa haki za makundi maalumu yakiwemo uliyoyaorodhesha hapa 2 na 4 kunatazamiwe kuleta matokeo gani ya tofauti ikiwa mbele ya kuyataja, katiba pendekezwa imestipulate "...Hakutakuwa na MAHAKAMA WALA CHOMBO KINGINE CHOCHOTE CHA KISHERIA KITAKACHOSIMAMIA UPATIKANAJI AMA UKOSEKANAJI WA HAKI HIZO". ? Wewe hili kwako lina maana gani? Ni kwa namna gani hizo haki zitasimamiwa na kupatikana ikiwa "kuzidai popote ni kukiuka katiba? Huoni kwamba zimeorodheshwa tu kwa hila ili kuwanyamazisha wapiga kelele lakini hakuna lengo wala nia ya kuwapatia haki hizo? Na tena hii ni moja wapo ya matatizo 10 ya katiba ninayokwenda kukuorodheshea. Kwamba katiba ya 1977 ilikuwa kimya juu ya haya, lakini sasa hii pendekezwa, imeorodhesha na kuzuia kisheria haki ya kudai kwa haki hizo ili pasiwe na wapiga kelele tena. Kila aliyeorodheshwa hapo atakapokuwa anapiga kelele kudai haki hizo atakuwa ana commit constitutional offence!.. Sasa wasanii, walevamvu, wavuvi, waandishi, wafugaji, n.k, marufuku kupiga makelele ya kudai haki!. Cheki huo mziki!.

3. Raisi wa Zanzibar kuwa makamu wa raisi, litaimarisha muungano mara dufu ikiwa tu tatizo la muungano ni mgawanyo wa madaraka ya uongozi wa nchi na kwamba Zanzibar inakubali kuwa kwenye subordinate position ya kutoka makamu wa raisi bila kuwa na uwezekano wa kutoa raisi milele. Matatizo ya muungano hayalalamikisi sana bara kwa sababu ya udogo wa zanzibar na hivyo kudhirisha athari zake kwa Tanganyika.

Hili liko dhahiri, Wanzanzibar hawajaridhika na solutions zilizochorwa kwenye rasimu ya ccm kwa sababu hazija adress matatizo yao halisi kwa upana wake ambayo essentially ni ya kiutamaduni zaidi.

Kwa mantiki hii, ikiwa kutoa makam wa raisi milele ndilo hitaji la wazanzibar, basi ni haki kwa ccm kuifanya zanzibar koloni lao milele kwa sababu hawajitambui kitu ambacho si kweli.

Nasubiri mchango wako, ili sasa nianze kukuorodheshea yale masuala kumi niliyosema nayo tuyajadili.


1.asilimia 50 ya wanawake na wanaume ktk madaraka hususan ktk siasa
2. haki za wakulima,wafugaji kutambuliwa rasmi kikatiba hatua itakayosaidia kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji na kuwawezesha kupata mikopo na kuboresha kilimo na ufugaji wao.
3. rais wa zanzibar kuwa makam wa rais hatua itakayoimarisha muungano mara dufu
4.uhuru wa vyombo vya habari kutambuliwa rasmi kisheria na zaidi haki za wasanii
 
Kwako wewe katiba nzuri eti mpaka iwe na serikali tatu ukawa ujuha huu sijui mtafika nao wapi.
 
Kabla sijaendelea:-

1. Hiyo asilimia 50 kwa hamsini inatija gani katika maendeleo ya taifa? Unaelewa maana na tafsiri yake halisi hasa ukizingatia viwango vye elimu ya Tanzania kwa sasa?

2. Kutajwa kwa haki za makundi maalumu yakiwemo uliyoyaorodhesha hapa 2 na 4 kunatazamiwe kuleta matokeo gani ya tofauti ikiwa mbele ya kuyataja, katiba pendekezwa imestipulate "...Hakutakuwa na MAHAKAMA WALA CHOMBO KINGINE CHOCHOTE CHA KISHERIA KITAKACHOSIMAMIA UPATIKANAJI AMA UKOSEKANAJI WA HAKI HIZO". ? Wewe hili kwako lina maana gani? Ni kwa namna gani hizo haki zitasimamiwa na kupatikana ikiwa "kuzidai popote ni kukiuka katiba? Huoni kwamba zimeorodheshwa tu kwa hila ili kuwanyamazisha wapiga kelele lakini hakuna lengo wala nia ya kuwapatia haki hizo? Na tena hii ni moja wapo ya matatizo 10 ya katiba ninayokwenda kukuorodheshea. Kwamba katiba ya 1977 ilikuwa kimya juu ya haya, lakini sasa hii pendekezwa, imeorodhesha na kuzuia kisheria haki ya kudai kwa haki hizo ili pasiwe na wapiga kelele tena. Kila aliyeorodheshwa hapo atakapokuwa anapiga kelele kudai haki hizo atakuwa ana commit constitutional offence!.. Sasa wasanii, walevamvu, wavuvi, waandishi, wafugaji, n.k, marufuku kupiga makelele ya kudai haki!. Cheki huo mziki!.

3. Raisi wa Zanzibar kuwa makamu wa raisi, litaimarisha muungano mara dufu ikiwa tu tatizo la muungano ni mgawanyo wa madaraka ya uongozi wa nchi na kwamba Zanzibar inakubali kuwa kwenye subordinate position ya kutoka makamu wa raisi bila kuwa na uwezekano wa kutoa raisi milele. Matatizo ya muungano hayalalamikisi sana bara kwa sababu ya udogo wa zanzibar na hivyo kudhirisha athari zake kwa Tanganyika.

Hili liko dhahiri, Wanzanzibar hawajaridhika na solutions zilizochorwa kwenye rasimu ya ccm kwa sababu hazija adress matatizo yao halisi kwa upana wake ambayo essentially ni ya kiutamaduni zaidi.

Kwa mantiki hii, ikiwa kutoa makam wa raisi milele ndilo hitaji la wazanzibar, basi ni haki kwa ccm kuifanya zanzibar koloni lao milele kwa sababu hawajitambui kitu ambacho si kweli.

Nasubiri mchango wako, ili sasa nianze kukuorodheshea yale masuala kumi niliyosema nayo tuyajadili.
Kwahiyo wewe unataka nini,usitumie neno wazanzibar tena koma kabisa sema wewe na chagadema yako hakuna mzanzibar anayepinga katiba inayopendekezwa ukiacha malimu sefu ambaye ni wakala wa sultani wengi wote wanaiunga mkono katiba.
 
Umeshajiuliza na UKAWA kwanini wanasema katiba hii si nzuri na kuwaambia wananchi wapige kura ya hapana?
UKAWA wako sawa kwani maoni mengi yaliyotolewa na wananchi kuhusu namna wanavyotaka kuongozwa na viongozi wao yametupwa na hasa yale yaliyotufanya kudai katiba mpya
 
Kwahiyo wewe unataka nini,usitumie neno wazanzibar tena koma kabisa sema wewe na chagadema yako hakuna mzanzibar anayepinga katiba inayopendekezwa ukiacha malimu sefu ambaye ni wakala wa sultani wengi wote wanaiunga mkono katiba.
Yaani kweli mnajiaibisha hamna cha kutetea kwenye katiba kwa hoja dhidi ya jazba na kejeli. Ndio maana mnasema watu wasisomewe waelewe wenyewe lakini nyinyi mnataja vifungu kama haki za wakulima, wafugaji, wasanii nk, kama gia ya kuwachanganya wananchi wenye uelewa mdogo. Nilitarajia ungetoa ufafanuzi wa hizo haki na wapi katiba pendekezwa inataja wataweza kuzidai. Halafu sio wewe tu ambaye umepewa jukumu humu jamvini kutetea hiyo aibu bali hata hao wajumbe wa BMk hawajitokezi kutoa ufafanuzi wa haya maswali, bali wamebaki kusema katiba ni nzuri sana imewalenga wananch, na udhaifu huu wa kuitetea hii aibu na hila ya ccm uko kwenu wote kuanzia Rais, wajumbe wote wa Bmk kasoro wa kura za hapana hawatoi ufafanuzi wa vifungu hivi mnavyoita vizuri. Sasa kama ni vizuri na hamuwezi kuvitolea ufafanuzi je hivyo vibaya itakuwaje. Andaeni jeshi kupiga watz kupitisha huu upuuzi maana hautapita kwa utashi wa wananchi.
 
mambo makubwa yaliyosababisha kudaiwa katiba ni jinsi wananchi wanavyotaka kuongozwa na viongozi wao lakini maoni yote hayo yametupwa viongozi wameweka ya kwao wanavyotaka kuwaongoza wananchi,kwa hali hiyo katiba haifai,ukiwasikiliza kwa makini wanaotaka tuikubali hawazungumzii la uongozi wanaishia kutuambia tu, eti imewatambua wafugaji,wakulima,wachimba madini,wavuvi,wazee,vijana,wanawake kumili Ardhi inawa katiba ya zamani haijasema mwanamke haruhusiwi kumiliki Ardhi na mwisho kabisa wanamalizia kwa kusema 50 kwa 50 wanawake na wanaume. wala suala la muungano hawasemi na wakati ndio kero kubwa,yaani serikali ya Zanzibar ipo kama ilivyokuwa kabla ya muungano ila serikali ya Tanganyika ndio imekuwa serikali ya muungano hilo hawaliweki wazi
 
Umeshajiuliza na UKAWA kwanini wanasema katiba hii si nzuri na kuwaambia wananchi wapige kura ya hapana?

Kwa kua imeacha maoni yetu wananchi yaliyokuwemo ktk rasimu ya 2 iliyowasilishwa BMK
 
Back
Top Bottom