Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Mkurugenzi ahamishwa kwa kukataa bao la mkono
na Moses Mseti, Mwanza
Inadaiwa kuwa mkurugenzi huyo ameondolewa katika jiji hilo baada ya kukataa kucheza bao la mkono, huku akituhumiwa kumuunga mkono Mgombea Urais wa Chadema, Edward Lowassa anayeungwa mkono na Muungano wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Inaelezwa kuwa Hida kabla ya kuondolewa katika nafasi hiyo na kupewa kazi nyingine serikalini, baadhi ya viongozi wakubwa wa mkoa huo, waliitisha vikao vya kumlazimisha kucheza bao la mkono jambo ambalo alipingana nalo na kibarua chake kuota mbawa.
Hata hivyo baada ya mkurugenzi huyo kukataa mchezo huo hatari, viongozi hao wa juu wa juu walianza kuwasiliana na viongozi wa kitaifa wakiomba kuondolewa kwake jambo ambalo halikuchukua muda mrefu na kuhamishwa.
Mtoa taarifa hizi amesema mkurugenzi huyo aliondolewa kutokana na kuwagomea viongozi hao wanaodaiwa kuunda mbinu chafu za kulazimisha ushindi katika jimbo la Nyamagana ambalo historia ya wabunge waliowahi kuongoza wamekaa kwa awamu moja.
Mtoa taarifa aliendelea kudai Chama cha Mapinduzi kimejipanga kulazimisha ushindi wowote ule hata kama ni wa kumwaga damu lakini washinde jimbo hilo kitendo ambacho kitasababisha uvunjifu wa Amani.