na Martin Malera
VIGOGO kadhaa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakiwamo wabunge machachari wanakabiliwa na hatari ya kufukuzwa uanachama kwa tuhuma za kujihusisha na Chama Cha Jamii (CCJ) ambacho kina usajili wa muda.
Habari zinasema baadhi yao wamekuwa wanachunguzwa kwa muda sasa, na Rais Jakaya Kikwete anataka kuwatoa kafara kama njia ya kuwatisha wenzao wanaodaiwa kuhujumu CCM katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Mmoja wa wabunge wanaotajwa tajwa sana kuhusiana na ukaribu wake na viongozi wa CCJ, amekuwa mwiba mkali kwa CCM katika miezi kadhaa ya hivi karibuni; na amekuwa anadaiwa kuwahamasisha wana CCM kujiunga na CCJ.
Habari ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata zinasema kuwa baadhi ya vigogo walio hatarini kufukuzwa ni wabunge ambao wamejipambanua kuwa ni wapambanaji wa ufisadi, na wamekuwa mstari wa mbele kuwahamasisha wenzao kujiunga na CCJ.
Hatua hiyo inatarajiwa kufikiwa katika kikao cha dharura kilichoitishwa na Rais Kikwete ambaye kwa siku nne mfululizo zilizopita ametumia muda mrefu katika ofisi yake ya chama iliyopo katika ofisi ndogo ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya CCM vinasema kuwa Rais Kikwete aliweza kubaini nia ya vigogo wa CCM kujiunga na CCJ na ameamua kuitisha kikao cha dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM, (NEC); na anataka kukitumia kutisha wabunge wanaojihusisha na CCJ.
Hata hivyo, habari hizo zinasema baadhi ya vigogo wanaolengwa na hasira hizo za Kikwete ni wale wasioweza kuleta madhara makubwa au kukigawa chama.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, ili kurejesha hali ya utulivu na amani hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, Rais Kikwete ameamua kuitisha kikao cha NEC cha dharura ili kuwashughulikia wanachama hao, wakiwemo wabunge na viongozi wengine mbalimbali ndani ya chama.
Habari hizo zinasema kikao hicho kitafanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa Mliman City, na ajenda ya mkutano huo anayo Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Kikwete.
"Jana na leo, Kikwete aliongoza vikao vya sekretarieti na kesho ataongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa huku NEC, ikitarajiwa kukutana Aprili nane hadi tisa," kilisema chanzo chetu cha habari.
Hiki ni kikao cha kwanza cha dharura kuitishwa na Rais Kikwete tangu aliposhika nafasi ya mwenyekiti wa CCM taifa.
Kutokana na hali hiyo, wadadisi wa masuala ya siasa ndani ya CCM wanasema kwamba huenda kuna mambo mazito ambayo Rais Kikwete anataka kuyafanya, achilia mbali suala la kufukuzwa uanachama kwa baadhi ya wabunge, viongozi na wengine.
Tanzania Daima Jumapili, imepata taarifa iliyosambazwa kwa vyombo vya habari na Ofisi ya Katibu Mkuu wa CCM, ikibainisha ajenda zitakazojadiliwa na kikao hicho kilichobainishwa kuwa ni cha kawaida.
Ajenda zitakazojadiliwa katika kikao hicho ni maandalizi ya CCM kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, mapendekezo ya wanachama watakaogombea nafasi ya Katibu Mwenezi wa mkoa wa Dar es Salam na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini.
Kikao hicho ambacho wajumbe wake tayari wameshafika jijini Dar es Salaam, kitapata fursa ya kupokea na kujadili taarifa mbalimbali zihusuzo masuala ya ndani ya chama.
Tangu kuanzishwa kwa CCJ, baadhi ya vigogo ndani ya CCM, wamekuwa wakihusishwa nacho. Hali hiyo ilimfanya Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, kutoa waraka nchi nzima kuwaonya makada wake wanaojihusisha na chama hicho ambacho kimejipatia umaarufu mkubwa kabla ya hata ya kupata usajili wa kudumu.
Baadhi ya vigogo waliotajwa kuhusika na CCJ na ambao mara kadhaa wamejitokeza hadharani kukanusha ni pamoja na Spika wa Bunge Samuel Sitta na wabunge wengine waliokuwa wanajipambanua kama wapiganaji wa vita dhidi ya ufisadi.
Hata hivyo, CCJ kilizinduliwa wiki iliyopita bila kuwepo kwa vigogo hao waliotarajiwa.
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa wanasema kuwa inawezekana kuna wabunge wa CCM wanataka kujiunga na CCJ lakini katika mazingira ya sasa hawawezi kufanya hivyo kwa kuhofia kupoteza viinua mgongo vyao. Fedha wanazopata wabunge kama kiinua mgongo ni zaidi ya sh mil. 40 ambazo zinawafanya wasite kuhama CCM, hasa katika mazingira haya ambapo CCJ bado hakijapata usajili wa kudumu.
VIGOGO kadhaa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakiwamo wabunge machachari wanakabiliwa na hatari ya kufukuzwa uanachama kwa tuhuma za kujihusisha na Chama Cha Jamii (CCJ) ambacho kina usajili wa muda.
Habari zinasema baadhi yao wamekuwa wanachunguzwa kwa muda sasa, na Rais Jakaya Kikwete anataka kuwatoa kafara kama njia ya kuwatisha wenzao wanaodaiwa kuhujumu CCM katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Mmoja wa wabunge wanaotajwa tajwa sana kuhusiana na ukaribu wake na viongozi wa CCJ, amekuwa mwiba mkali kwa CCM katika miezi kadhaa ya hivi karibuni; na amekuwa anadaiwa kuwahamasisha wana CCM kujiunga na CCJ.
Habari ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata zinasema kuwa baadhi ya vigogo walio hatarini kufukuzwa ni wabunge ambao wamejipambanua kuwa ni wapambanaji wa ufisadi, na wamekuwa mstari wa mbele kuwahamasisha wenzao kujiunga na CCJ.
Hatua hiyo inatarajiwa kufikiwa katika kikao cha dharura kilichoitishwa na Rais Kikwete ambaye kwa siku nne mfululizo zilizopita ametumia muda mrefu katika ofisi yake ya chama iliyopo katika ofisi ndogo ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya CCM vinasema kuwa Rais Kikwete aliweza kubaini nia ya vigogo wa CCM kujiunga na CCJ na ameamua kuitisha kikao cha dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM, (NEC); na anataka kukitumia kutisha wabunge wanaojihusisha na CCJ.
Hata hivyo, habari hizo zinasema baadhi ya vigogo wanaolengwa na hasira hizo za Kikwete ni wale wasioweza kuleta madhara makubwa au kukigawa chama.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, ili kurejesha hali ya utulivu na amani hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, Rais Kikwete ameamua kuitisha kikao cha NEC cha dharura ili kuwashughulikia wanachama hao, wakiwemo wabunge na viongozi wengine mbalimbali ndani ya chama.
Habari hizo zinasema kikao hicho kitafanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa Mliman City, na ajenda ya mkutano huo anayo Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Kikwete.
"Jana na leo, Kikwete aliongoza vikao vya sekretarieti na kesho ataongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa huku NEC, ikitarajiwa kukutana Aprili nane hadi tisa," kilisema chanzo chetu cha habari.
Hiki ni kikao cha kwanza cha dharura kuitishwa na Rais Kikwete tangu aliposhika nafasi ya mwenyekiti wa CCM taifa.
Kutokana na hali hiyo, wadadisi wa masuala ya siasa ndani ya CCM wanasema kwamba huenda kuna mambo mazito ambayo Rais Kikwete anataka kuyafanya, achilia mbali suala la kufukuzwa uanachama kwa baadhi ya wabunge, viongozi na wengine.
Tanzania Daima Jumapili, imepata taarifa iliyosambazwa kwa vyombo vya habari na Ofisi ya Katibu Mkuu wa CCM, ikibainisha ajenda zitakazojadiliwa na kikao hicho kilichobainishwa kuwa ni cha kawaida.
Ajenda zitakazojadiliwa katika kikao hicho ni maandalizi ya CCM kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, mapendekezo ya wanachama watakaogombea nafasi ya Katibu Mwenezi wa mkoa wa Dar es Salam na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini.
Kikao hicho ambacho wajumbe wake tayari wameshafika jijini Dar es Salaam, kitapata fursa ya kupokea na kujadili taarifa mbalimbali zihusuzo masuala ya ndani ya chama.
Tangu kuanzishwa kwa CCJ, baadhi ya vigogo ndani ya CCM, wamekuwa wakihusishwa nacho. Hali hiyo ilimfanya Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, kutoa waraka nchi nzima kuwaonya makada wake wanaojihusisha na chama hicho ambacho kimejipatia umaarufu mkubwa kabla ya hata ya kupata usajili wa kudumu.
Baadhi ya vigogo waliotajwa kuhusika na CCJ na ambao mara kadhaa wamejitokeza hadharani kukanusha ni pamoja na Spika wa Bunge Samuel Sitta na wabunge wengine waliokuwa wanajipambanua kama wapiganaji wa vita dhidi ya ufisadi.
Hata hivyo, CCJ kilizinduliwa wiki iliyopita bila kuwepo kwa vigogo hao waliotarajiwa.
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa wanasema kuwa inawezekana kuna wabunge wa CCM wanataka kujiunga na CCJ lakini katika mazingira ya sasa hawawezi kufanya hivyo kwa kuhofia kupoteza viinua mgongo vyao. Fedha wanazopata wabunge kama kiinua mgongo ni zaidi ya sh mil. 40 ambazo zinawafanya wasite kuhama CCM, hasa katika mazingira haya ambapo CCJ bado hakijapata usajili wa kudumu.