voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,553
- 11,885
Uzi kutoka X, kina Lucas mwashambwa & company JF muisome na kujitambua
"Inawezekana ni jambo ambalo wengi hawajui kuwa linaendelea ndani ya CCM ,na sishangai kwa kuwa watanzania tuna tabia ya kutofuatilia mambo na kuyatafiti lakini kwa maamuzi haya ya Daniel Chongolo nadhani yabatia mashaka makubwa sana juuya uwezo wake wa kimaamuzi kama katibu mkuu wa CCM.
CCM inaajiri sasa makatibu wenezi kama ambavyo vikao vya chama viliagiza na Daniel Chongolo anatumia nafasi hiyo kuwapa madaraka makubwa sana watu kutoka CHADEMA bila kushindanishwa na kufanyiwa usaili kama ambavyo inatakiwa ifanyike kwa maagizo ya vikao vya chama chake.
Daniel Chongolo kama mwajiri mkuu ndani ya CCM na katibu mkuu wa chama tawala kwa mamlaka yake hayo ameamua kuajiri na kuwapa nafasi kubwa sana na za ndani sana za CCM makada wa CHADEMA. Jambo hili ni hatari na lina athari kubwa sana ndani ya CCM na mshikamano ndani ya CCM na wanachama wake.
Sidhani kama Chongolo anaona maumivu ya vijana wa UVCCM na wafia CCM wengine wenye sifa na waliokitumikia hiki chama kwa jasho na damu miaka nenda rudi halafu leo wanakuja kuona watu toka CHADEMA wanapewa vyeo vikubwa ndani ya chama tena bila kukijua chama hiki na kuishi imani ya chama hiki . Sidhani kama Chaongolo anaona hili ma madhara yake na uasi anaokuja kuusababisha ndani ya hiki chama.
Nilistushwa sana kumuona Ally Bananga akiongea kwenye vyombo vya habari na akitambulishwa kama Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Dar Es Salaam. Sina shida na yeye kuwa katibu mwenezi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam lakini nina shida ya jinsi ambavyo Chongolo kama katibu mkuu wa CCM anatazama mambo na kuyapima kabla hajaamua.
Yaani Bananga amempa jukumu la kupambania kura milioni 5 hivi zilizoko Dar Es Salaam ? Yaani Bananga anakuwa katibu mwenezi wa chama mkoa wa Dar Es Salaam ambaye ni mtu anajua mambo mengi sana ya kimkakati ndani ya chama ngazi ya mkoa na ngazi ya taifa huku ana mke ambaye yuko chama hasimu na CCM?
Hivi huyu Chongolo aliandaliwa kweli kuongoza hiki chama au alibahatika tu kupewa hii nafasi? Sielewi na sijaelewa na sitaelewa kama ni kweli CCM imekosa vijana ndani ya chama kuanzia huko mikoani mpaka Dar Es Salaam kwenyewe kupewa hii nafasi mpaka inafikia mtu wa nje ya chama na mtu aliyekulia nje ya chama hiki anapewa nafasi kubwa hivi. Bananga huyu si ndiyo alizunguka na Lissu nchi nzima kufanya kampeni? Huyu mara hii kaaminiwa ndani ya CCM mpaka kupewa nafasi kubwa hivi?
Ukiniuliza ntasema hapana hakutakiwa kupewa hii nafasi hasa kwa mkoa wa kimkakati kama Dar Es Salaam na ni makosa makubwa sana kwa Chongolo kufanya hivi na kama alimpenda sana na hakujisikia raha kutompa ajira basi angempa mkoa mwingine lakini siyo mkoa wa Dar Es Salaam. Nasema siyo Dar es Salaam na kwa vyovyote vile haikufaa hata kidogo kufanywa hivi.
Chongolo hajaishia hapo. Amekwenda mbali zaidi kaajiri afisa habari kwa siri ambaye alikuwa chama cha upinzani na cha kusikitisha zaidi ni kuwa unapokuwa afisa habari wa katibu mkuu wa CCM maana yake ni pana sana na kubwa sana. Anajua siri zote na kikakati yote ya chama ngazi zote za nchi.
Je, hivi kweli CCM hii mnaamini watu mapema kiasi hiki mpaka mnawapa mavyeo makubwa hivyo ndani ya chama kwa muda mfupi hivi? Hakuna vijana walioandaliwa ndani ya hiki chama kushika hizi nafasi?
Chongolo anatumia vibaya nafasi iliyoamriwa na vikao vya chama kuwa nafasi ya ukatibu uenezi ndaniya CCM itakuwa ni nafasi ya kuajiriwa na alichofanya Chogolo ni geresha tu ya kutaka watu waombe nafasi hiyo lakini alikuwa na jina la Bananga mfukoni.
Nina uhakika hili halikai sawa na wengi wa watu wa CCM hasa mkoa wa Dar es Salaam hawajalifurahia na athari za hili CCM watakuja kuliona kwenye uchaguzi ujao maana watu wa CCM watakwenda kwenye uchaguzi wakisikitika na kuna hatari ya kuhujumu chama.
Kwa maamuzi haya na mengine napata shida sana kuelewa kama Chongolo akiwa katibu mkuu wa CCM anaweza kuongoza kuweka mikakati na mipango ili CCM ishinde kwa kishindo kikubwa sana kwenye uchaguzi wa 2024 na uchaguzi mkuu wa 2025.
Natafakari lakini kiukweli hana uwezo.
"Inawezekana ni jambo ambalo wengi hawajui kuwa linaendelea ndani ya CCM ,na sishangai kwa kuwa watanzania tuna tabia ya kutofuatilia mambo na kuyatafiti lakini kwa maamuzi haya ya Daniel Chongolo nadhani yabatia mashaka makubwa sana juuya uwezo wake wa kimaamuzi kama katibu mkuu wa CCM.
CCM inaajiri sasa makatibu wenezi kama ambavyo vikao vya chama viliagiza na Daniel Chongolo anatumia nafasi hiyo kuwapa madaraka makubwa sana watu kutoka CHADEMA bila kushindanishwa na kufanyiwa usaili kama ambavyo inatakiwa ifanyike kwa maagizo ya vikao vya chama chake.
Daniel Chongolo kama mwajiri mkuu ndani ya CCM na katibu mkuu wa chama tawala kwa mamlaka yake hayo ameamua kuajiri na kuwapa nafasi kubwa sana na za ndani sana za CCM makada wa CHADEMA. Jambo hili ni hatari na lina athari kubwa sana ndani ya CCM na mshikamano ndani ya CCM na wanachama wake.
Sidhani kama Chongolo anaona maumivu ya vijana wa UVCCM na wafia CCM wengine wenye sifa na waliokitumikia hiki chama kwa jasho na damu miaka nenda rudi halafu leo wanakuja kuona watu toka CHADEMA wanapewa vyeo vikubwa ndani ya chama tena bila kukijua chama hiki na kuishi imani ya chama hiki . Sidhani kama Chaongolo anaona hili ma madhara yake na uasi anaokuja kuusababisha ndani ya hiki chama.
Nilistushwa sana kumuona Ally Bananga akiongea kwenye vyombo vya habari na akitambulishwa kama Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Dar Es Salaam. Sina shida na yeye kuwa katibu mwenezi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam lakini nina shida ya jinsi ambavyo Chongolo kama katibu mkuu wa CCM anatazama mambo na kuyapima kabla hajaamua.
Yaani Bananga amempa jukumu la kupambania kura milioni 5 hivi zilizoko Dar Es Salaam ? Yaani Bananga anakuwa katibu mwenezi wa chama mkoa wa Dar Es Salaam ambaye ni mtu anajua mambo mengi sana ya kimkakati ndani ya chama ngazi ya mkoa na ngazi ya taifa huku ana mke ambaye yuko chama hasimu na CCM?
Hivi huyu Chongolo aliandaliwa kweli kuongoza hiki chama au alibahatika tu kupewa hii nafasi? Sielewi na sijaelewa na sitaelewa kama ni kweli CCM imekosa vijana ndani ya chama kuanzia huko mikoani mpaka Dar Es Salaam kwenyewe kupewa hii nafasi mpaka inafikia mtu wa nje ya chama na mtu aliyekulia nje ya chama hiki anapewa nafasi kubwa hivi. Bananga huyu si ndiyo alizunguka na Lissu nchi nzima kufanya kampeni? Huyu mara hii kaaminiwa ndani ya CCM mpaka kupewa nafasi kubwa hivi?
Ukiniuliza ntasema hapana hakutakiwa kupewa hii nafasi hasa kwa mkoa wa kimkakati kama Dar Es Salaam na ni makosa makubwa sana kwa Chongolo kufanya hivi na kama alimpenda sana na hakujisikia raha kutompa ajira basi angempa mkoa mwingine lakini siyo mkoa wa Dar Es Salaam. Nasema siyo Dar es Salaam na kwa vyovyote vile haikufaa hata kidogo kufanywa hivi.
Chongolo hajaishia hapo. Amekwenda mbali zaidi kaajiri afisa habari kwa siri ambaye alikuwa chama cha upinzani na cha kusikitisha zaidi ni kuwa unapokuwa afisa habari wa katibu mkuu wa CCM maana yake ni pana sana na kubwa sana. Anajua siri zote na kikakati yote ya chama ngazi zote za nchi.
Je, hivi kweli CCM hii mnaamini watu mapema kiasi hiki mpaka mnawapa mavyeo makubwa hivyo ndani ya chama kwa muda mfupi hivi? Hakuna vijana walioandaliwa ndani ya hiki chama kushika hizi nafasi?
Chongolo anatumia vibaya nafasi iliyoamriwa na vikao vya chama kuwa nafasi ya ukatibu uenezi ndaniya CCM itakuwa ni nafasi ya kuajiriwa na alichofanya Chogolo ni geresha tu ya kutaka watu waombe nafasi hiyo lakini alikuwa na jina la Bananga mfukoni.
Nina uhakika hili halikai sawa na wengi wa watu wa CCM hasa mkoa wa Dar es Salaam hawajalifurahia na athari za hili CCM watakuja kuliona kwenye uchaguzi ujao maana watu wa CCM watakwenda kwenye uchaguzi wakisikitika na kuna hatari ya kuhujumu chama.
Kwa maamuzi haya na mengine napata shida sana kuelewa kama Chongolo akiwa katibu mkuu wa CCM anaweza kuongoza kuweka mikakati na mipango ili CCM ishinde kwa kishindo kikubwa sana kwenye uchaguzi wa 2024 na uchaguzi mkuu wa 2025.
Natafakari lakini kiukweli hana uwezo.