Keil,
Mkuu haya maneno mazito sana..Mwakyembe na wenzake wanaweza kuruhusiwa kwenda mikoani kwa kuwa wao wanakwenda kwenye majimbo yao tu ama kwenye jimbo la mpambanaji mwenzao ili kumpiga tafu. Hawana hoja inayolenga nafasi kubwa na nyeti kama ya Rais kwa kuwa uwezo wao kifedha ni mdogo na pia nafasi yao ndani ya chama ni mdogo sana. On top of that kundi la wapiganaji wala si tishio kwa JK kama mgombea wa urais hapo 2010, bali ni tishio kwa kuivua nguo serikali kwa hiyo JK anacholilia sasa ni kuwa-control ili wasipige sana kelele, maana kelele za wapiganaji zinamfanya JK aonekane kuwa ni weak president ambaye ana watendaji wabovu lakini ameshindwa kuwawajibisha.