CCM, JamiiForums ni watu siyo Mashine!!

CCM, JamiiForums ni watu siyo Mashine!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,176
Reaction score
48,460
Kila wakati CCM wakizidiwa kwenye mijadala humu JF hukimbilia kusema kuwa "CCM haipendwi JF tu lakini mitaani inapendwa"

Niwafahamishe CCM kwamba sisi tunaochangia humu tunaishi mitaani na siyo mashine (Robot) bali ni watu halisi.

Sisi tumo mitaani na wakati mwingine maoni tunayoyatoa ni ya watu wengi walioko "mitaani" CCM inakosema inaungwa mkono!

Kama mnaungwa mkono mitaani na mnapingwa kwenye mitandao ya kijamii, ni kwa nini basi msiruhusu huko mitaani CHADEMA nao wafanye siasa ili ionekane wanavyokataliwa na watu wa mitaani?
 
Upepo umegeuka CCM JFwameingia mitini
kJZWYia.gif
 
Kila wakati CCM wakizidiwa kwenye mijadala humu JF hukimbilia kusema kuwa "CCM haipendwi JF tu lakini mitaani inapendwa"

Niwafahamishe CCM kwamba sisi tunaochangia humu tunaishi mitaani na siyo mashine (Robot) bali ni watu halisi.

Sisi tumo mitaani na wakati mwingine maoni tunayoyatoa ni ya watu wengi walioko "mitaani" CCM inakosema inaungwa mkono!

Kama mnaungwa mkono mitaani na mnapingwa kwenye mitandao ya kijamii, ni kwa nini basi msiruhusu huko mitaani CHADEMA nao wafanye siasa ili ionekane wanavyokataliwa na watu wa mitaani?
Jibu rahisi wanaloweza kutoa ni kuwa wana Jf ni vibaraka wa mabeberu!
 
USA/EU zimewapiga chini JF wameikimbia tunazisubiri na MAASKOFU na MASHEHE nao WAWAKANE halafu lile kundi la MEMBE na NNAPE na JANUARY BASHE wamalizie kazi Masikia Akaunti inafunguliwa Kenya ili kumuondoa huyu bwana Mbabe.
 
Nani atawapenda CCM chama cha wauaji na wanyang’anyi!? Wasojitambua tu na akili za kushikiwa ndiyo wanaweza kufanya hivyo. Hata muasisi wa CCM alishaanza kuiponda miaka ile na wakati ule hali ndani ya chama hicho haikuwa ya kutisha kama ilivyo sasa.
 
Maccm sijui hata tuyatukane kwa matusi gani ndo yagutuke usingizini kaka!
Kuna shida kubwa sana hapa. Kwahiyo hizi ndio hoja zinazoongelewa. Matusi!. Tunasubiri 2020 mtukane ili tuone kama mtashinda uchaguzi. Huo utakuwa ubunifu wa kipekee kutoka Tanzania.
 
Back
Top Bottom