CCM itatawala nchi kwa karne nzima

CCM itatawala nchi kwa karne nzima

Udhaifu uliopo kwenye vyama vya Upinzani ndio utafanya CCM itawale karne nyingi.
Huwezi kufanya kampeni kwa kutafuta kura za huruma. Mie binafsi naamini na mapungufu ya CCM kwasasa Tanzania hakuna chama mbadala ambacho kinafaa kupewa madaraka
 
Karne nzima itamtawala nani wakati rais watakuwa wamekwisha kwa kupigwa risasi Na kutekwa.
 
Baadhi ya watu, nikiwemo mimi, tumekuwa tukiamini kuwa mtaji mkubwa wa CCM katika ushindani wa kisiasa nchini ni ujinga wa wananchi.

Kwamba, kuna sehemu kubwa ya wananchi ambao ni wajinga ama kwa kutokutaka au kupenda kufuatilia mambo vizuri au kwa kuwa na uwezo mdogo wa kuchanganua mambo na hivyo kupelekea kurubuniwa na CCM pindi msimu wa uchaguzi unapokaribia ili wakipe kura chama hicho.

Tumekuwa tukiiamini sana nadharia hiyo kwa sababu tunaamini kuwa ni vigumu sana kwa mtu na akili zake timamu kuendelea kuiunga mkono CCM licha ya uborongaji wake.

Lakini, mimi binafsi nadhani mtaji wa kisiasa wa CCM si ujinga peke yake. Naamini pia uoga wa Watanzania nao ni bonge la mtaji kwao.

Sisi Watanzania ni waoga sana. Tunaogopa mno dola. Tukisikia tu polisi au jeshi, basi tunaanza kutetemeka.

Nyakati zingine huwa nikiangalia jinsi ambavyo watu wa mataifa mengine wanavyopambana na polisi huwa nabaki mdomo wazi.

Unakuta waandamanaji wanazipiga na polisi katikati ya barabara. Tena hawaogopi kabisa. Sasa mambo kama hayo hapa kwetu sidhani kama yanaweza kutokea. Na ndo maana huwa tukitishwa kidogo tu tunaogopa.

Hatuna kabisa ujasiri wa kuidindia serikali. Hatuna ujasiri wa kupigana na ma askari polisi kama wafanyavyo watu wa mataifa mengine.

Uoga wetu huu ndo unanifanya niamini kuwa CCM inaweza kutawala nchi hata kwa zaidi ya karne nzima.

Je, uoga tulionao nao ni sehemu ya ndivyo tulivyo ama?
Mwanaume kabisa unaandika mada kama hii?
 
Kwa kiasi uko sawa lakini utaipataje tume huru?! Amini usiamini ni mpaka damu tena ya kutosha!! CCM hawawezi kukubalia tume huru wanajuwa watakuwa wameisha!!

Pili ni kuhusu nchi zilizopiga hatua na hasa Africa ktk chaguzi huru na hata ki uchumi ni zile walizouana na kupinduana kwa sana . Nchi za Africa magharibi sasa hivi wako vizuri , mpinzani akishinda anapewa bila shida mf. Nigeria, Senegal, Ghana, na zile zilizojaribu kung'ang'ania viongozi walifurushwa na ECOWAS. Lakini Africa mashariki, tunajifanya tuna amani na huku tunaongozwa na madikteta, wasiotaka upinzani kwao sawa na uasi .
Sasa udikteta utauondoa kwa sala ???!!!!
mmmh.mzee hapo kwenye damu mtihani.
napenda nchi ifate sheria,miongozo na taratibu tulizojiwekea.lakini si kwa kushika mapanga.
ni kuamua tu kuisimamisha demokrasia na tuifate.
na kikubwa upinzani usichukuliwe kama ni uadui.
wote lengo letu ni kuijenga Tanzania.
tushirikiane.tukosoane.pia turekebishane pale tunapoona mambo hayaendi sawa.NEC NAO WATENDE HAKI
 
Ni vibaya sana kuishi kwa kubahatisha...nidhambi na niaibu kwani tumejaaliwa akili. Leo upinzani unagombea huku ukijua kwanza madarakani yupo mwenye chuki kuu nao na hataki kuwaona. Pili,usimamizi wote wa uchaguzi uko chini ya huyo anayewachukia. Wapinzani wangepaswa kudai katiba bora itayoleta usawa katika demokrasia. Leo hii huwezi laumu tena diwani ama mbunge anayehamia CCM kwani kimsingi ndiyo wenye nchi.
Yatupasa tuangalie kama kuna umuhimu tena wa hii demokrasia yakibabe na kibaguzi,twaweza ingia gharama kuubwa kufanya maigizo yakitoto na siasa za kiwendawazimu. Nikisikia tena wapinzani wanagombea mahali kwa mifumo na katiba hii nitawaona wasiokuwa na akili timamu.
 
Udhaifu uliopo kwenye vyama vya Upinzani ndio utafanya CCM itawale karne nyingi.
Huwezi kufanya kampeni kwa kutafuta kura za huruma. Mie binafsi naamini na mapungufu ya CCM kwasasa Tanzania hakuna chama mbadala ambacho kinafaa kupewa madaraka
mkuu kwani CCM kuongoza miaka yote NI KOSA?
tatizo linakuja wanaongoza vipi nchi.
KAMA WANANCHI WANAIKUBALI CCM NA KUIPENDA HATUWEZI TUKASEMA NI UJINGA.SI WANAKUBALIKA.
TATITO NI UDANGANYIFU KWENYE CHAGUZI NA KUIBA KURA.
kama CCM wakishinda kwa haki.
sisi upinzani hatutakuwa na neno si wananchi wameamua.waongozwe na CCM.kwani kuna ugomvi?
TATIZO WIZI WA KURA.
 
Watanzania sio waoga..ila WANAFIKI..Wanauwa mwizi Wa simu fisadi anachekewa
 
mmmh.mzee hapo kwenye damu mtihani.
napenda nchi ifate sheria,miongozo na taratibu tulizojiwekea.lakini si kwa kushika mapanga.
ni kuamua tu kuisimamisha demokrasia na tuifate.
na kikubwa upinzani usichukuliwe kama ni uadui.
wote lengo letu ni kuijenga Tanzania.
tushirikiane.tukosoane.pia turekebishane pale tunapoona mambo hayaendi sawa.NEC NAO WATENDE HAKI
Hawatatenda kama unavyofikiri hata siku moja. Omba uhai
 
Hata hizo nchi unazozisifia kwamba sio waoga, walianza taratibu, na kuna vitu vilipelekea wakafikia hiyo hatua.
Naamini hata hapa kwetu kama hivyo vitu viliyopelekea watu wakapoteza uoga vikiendelea, woga utaisha na usishangae yakatokea kama yanayoendelea mataifa mengine.

Lakini kwanini uoga uangaliwe kwenye eneo moja tu la kupambana hasa kupigana na polisi au vyombo vya dola? CCM inaweza kutolewa madarakani kwa njia nyingi tu bila hata kupambana na polisi kwa mabavu.

kwamaneno kuna njia nyingi zakuitoa ccm, kwa vitendo hakuna

kuitoa ccm ni sawa na kutoa vyombo vya usalama vyote, fikiri kama inawezekana
 
Hawatatenda kama unavyofikiri hata siku moja. Omba uhai
naamini demokrasia ya Zimbabwe na SA.IPO siku itafika kwetu.
siasa sio uadui.
SIO MPAKA TUUANE NDO TUONEKANE TUNATAKA KUIJENGA NCHI YETU.
kikubwa NEC huru.
MTU ashinde na kushindwa kihalali.
ugumu unatoka wapi?
 
Kwanini unataka kupigana na Polisi?

Polisi wanapiga kura?

Tatizo lako lipo ktk box la kura

Wapo wanaoipigia kura CCM na ni wengi.

Huwezi kushinda uchaguzi kwa kupigana na Polisi.
Nani anapigana na Polisi. Polisi ndio wanatumiwa na CCM. POLE
 
Pamoja na ujinga lakini kete kubwa ya CCM kutawala ni mabavu. Kutumia vyombo vya dola kujipa ushindi
 
naamini demokrasia ya Zimbabwe na SA.IPO siku itafika kwetu.
siasa sio uadui.
SIO MPAKA TUUANE NDO TUONEKANE TUNATAKA KUIJENGA NCHI YETU.
kikubwa NEC huru.
MTU ashinde na kushindwa kihalali.
ugumu unatoka wapi?
Si rahisi kwa ccm hawa kuachia Tume huru ya uchaguzi pna katiba itakayotoa fair kwa wapinzani wao !!
 
Nonsense ! Hawa wadanganyika watakapoamka kutoka usingizi wa pono na ganzi ya mwenge it will be impossible for CCM kutawala it’s just a natural law! The communist party of the then Soviet Union refused to reform matokeo yake it ruled for 70 years and it’s now distinct na hata CCM ikikaribia 70 it’s now 64 itasambaratika na makaburi ya waanzilishi yatafukuliwa na kubomolewa and itakuwa kilio na kusaga meno kwa watoto wa viongozi and they shall have no where to hide!
 
Baadhi ya watu, nikiwemo mimi, tumekuwa tukiamini kuwa mtaji mkubwa wa CCM katika ushindani wa kisiasa nchini ni ujinga wa wananchi.

Kwamba, kuna sehemu kubwa ya wananchi ambao ni wajinga ama kwa kutokutaka au kupenda kufuatilia mambo vizuri au kwa kuwa na uwezo mdogo wa kuchanganua mambo na hivyo kupelekea kurubuniwa na CCM pindi msimu wa uchaguzi unapokaribia ili wakipe kura chama hicho.

Tumekuwa tukiiamini sana nadharia hiyo kwa sababu tunaamini kuwa ni vigumu sana kwa mtu na akili zake timamu kuendelea kuiunga mkono CCM licha ya uborongaji wake.

Lakini, mimi binafsi nadhani mtaji wa kisiasa wa CCM si ujinga peke yake. Naamini pia uoga wa Watanzania nao ni bonge la mtaji kwao.

Sisi Watanzania ni waoga sana. Tunaogopa mno dola. Tukisikia tu polisi au jeshi, basi tunaanza kutetemeka.

Nyakati zingine huwa nikiangalia jinsi ambavyo watu wa mataifa mengine wanavyopambana na polisi huwa nabaki mdomo wazi.

Unakuta waandamanaji wanazipiga na polisi katikati ya barabara. Tena hawaogopi kabisa. Sasa mambo kama hayo hapa kwetu sidhani kama yanaweza kutokea. Na ndo maana huwa tukitishwa kidogo tu tunaogopa.

Hatuna kabisa ujasiri wa kuidindia serikali. Hatuna ujasiri wa kupigana na ma askari polisi kama wafanyavyo watu wa mataifa mengine.

Uoga wetu huu ndo unanifanya niamini kuwa CCM inaweza kutawala nchi hata kwa zaidi ya karne nzima.

Je, uoga tulionao nao ni sehemu ya ndivyo tulivyo ama?
Hivi mnahamasishana kuanza kupigana na serikali! Mmechoka na amani?
 
Nakubaliana na wewe 100%. Na wanaoongoza kwa uoga ni wasomi. Intellectual prostitution.
 
Baadhi ya watu, nikiwemo mimi, tumekuwa tukiamini kuwa mtaji mkubwa wa CCM katika ushindani wa kisiasa nchini ni ujinga wa wananchi.

Kwamba, kuna sehemu kubwa ya wananchi ambao ni wajinga ama kwa kutokutaka au kupenda kufuatilia mambo vizuri au kwa kuwa na uwezo mdogo wa kuchanganua mambo na hivyo kupelekea kurubuniwa na CCM pindi msimu wa uchaguzi unapokaribia ili wakipe kura chama hicho.

Tumekuwa tukiiamini sana nadharia hiyo kwa sababu tunaamini kuwa ni vigumu sana kwa mtu na akili zake timamu kuendelea kuiunga mkono CCM licha ya uborongaji wake.

Lakini, mimi binafsi nadhani mtaji wa kisiasa wa CCM si ujinga peke yake. Naamini pia uoga wa Watanzania nao ni bonge la mtaji kwao.

Sisi Watanzania ni waoga sana. Tunaogopa mno dola. Tukisikia tu polisi au jeshi, basi tunaanza kutetemeka.

Nyakati zingine huwa nikiangalia jinsi ambavyo watu wa mataifa mengine wanavyopambana na polisi huwa nabaki mdomo wazi.

Unakuta waandamanaji wanazipiga na polisi katikati ya barabara. Tena hawaogopi kabisa. Sasa mambo kama hayo hapa kwetu sidhani kama yanaweza kutokea. Na ndo maana huwa tukitishwa kidogo tu tunaogopa.

Hatuna kabisa ujasiri wa kuidindia serikali. Hatuna ujasiri wa kupigana na ma askari polisi kama wafanyavyo watu wa mataifa mengine.

Uoga wetu huu ndo unanifanya niamini kuwa CCM inaweza kutawala nchi hata kwa zaidi ya karne nzima.

Je, uoga tulionao nao ni sehemu ya ndivyo tulivyo ama?
Tatizo sio kutawala Karne au karne mbili. Tatizo jee itatuletea yale maendeleo tunayoyatarajia wengi?
 
Baadhi ya watu, nikiwemo mimi, tumekuwa tukiamini kuwa mtaji mkubwa wa CCM katika ushindani wa kisiasa nchini ni ujinga wa wananchi.

Kwamba, kuna sehemu kubwa ya wananchi ambao ni wajinga ama kwa kutokutaka au kupenda kufuatilia mambo vizuri au kwa kuwa na uwezo mdogo wa kuchanganua mambo na hivyo kupelekea kurubuniwa na CCM pindi msimu wa uchaguzi unapokaribia ili wakipe kura chama hicho.

Tumekuwa tukiiamini sana nadharia hiyo kwa sababu tunaamini kuwa ni vigumu sana kwa mtu na akili zake timamu kuendelea kuiunga mkono CCM licha ya uborongaji wake.

Lakini, mimi binafsi nadhani mtaji wa kisiasa wa CCM si ujinga peke yake. Naamini pia uoga wa Watanzania nao ni bonge la mtaji kwao.

Sisi Watanzania ni waoga sana. Tunaogopa mno dola. Tukisikia tu polisi au jeshi, basi tunaanza kutetemeka.

Nyakati zingine huwa nikiangalia jinsi ambavyo watu wa mataifa mengine wanavyopambana na polisi huwa nabaki mdomo wazi.

Unakuta waandamanaji wanazipiga na polisi katikati ya barabara. Tena hawaogopi kabisa. Sasa mambo kama hayo hapa kwetu sidhani kama yanaweza kutokea. Na ndo maana huwa tukitishwa kidogo tu tunaogopa.

Hatuna kabisa ujasiri wa kuidindia serikali. Hatuna ujasiri wa kupigana na ma askari polisi kama wafanyavyo watu wa mataifa mengine.

Uoga wetu huu ndo unanifanya niamini kuwa CCM inaweza kutawala nchi hata kwa zaidi ya karne nzima.

Je, uoga tulionao nao ni sehemu ya ndivyo tulivyo ama?

Nyani Ngabu, Watanzania siyo waoga, ila Watanzania wengi hawajui haki zao na pia bado hawajafahamu kiundani kabisa maamuzi ya kisiasa yana athahri gani katika maisha yao, Wengi wanaichukulia Siasa kama mchezo wa kishabiki tu kama mpira wa Simba na Yanga kwa hiyo hawako tayari kusimama kidete katika mambo ya siasa kama vile demokrasia etc

Ila sasa polepole tunapokwenda, Elimu ya uraia inaongezeka , watu wengi sana watafahamu mwanasiasa na siasa zake zinamuathiri yeye mwananchi katika maisha yake, Watu watajua haki zao, Wakishazijua vizuri kabisa, na wakatambua maamuzi ya kisiasa yanawaumizaje basi Hii dhana ya Uoga wa Watanzania utashangaa kuwa siyo kweli!.

Kwa hiyo ni suala la Elimu tu (Education), Watanzania walio wengi siku Wakielimika ipasavyo juu ya haki zao za kikatiba, lakini pia wakielimika kwa kufahamu dhahiri kuwa Maamuzi ya kisiasa yanagusa moja kwa moja maisha yake na ya familia yake, Ogopa brother, things will never be the same again.
 
Back
Top Bottom