tajirijasiri
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 2,864
- 3,851
Viongozi wengi wa CCM wana "U sisi Wasafi" na "U wao wachafu". Wale wa U sisi Wasafi wanaamini ni wazalendo na Wafia nchi na kwamba wale "U wao Wachafu" wanahisi kutengwa na kupuuzwa. Hawa wa "U wao Wachafu" wataondoka na kujiunga na Vyama Pinzani au kuanzisha Vyama vyao. Wakishaondoka wote, watabaki wa "U sisi wasafi".
Lakini kwa sababu dhambi ya Ubaguzi haijawahi kuacha mtu salama, basi hawa wa "U sisi Wasafi" watabaguana katika madaraja 1. "U sisi wasafi walio katibu na Mwenyekiti". 2. "U sisi wasafi tuliokatikati" na 3. "U sisi wasafi tulio mbali na Mwenyekiti". Wale wa daraja la kwanza watapambana dhidi ya wale wa daraja la pili kubakia/kusogea karibu na Mwenyekiti.
Mwisho wa mtifuano huo utapelekea kudhoofika na kuanguka kwa CCM na nchi itaongozwa na Chama kipyaa kabisa. Unabii wa Mwl. Nyerere utakuwa umetimia.
Lakini kwa sababu dhambi ya Ubaguzi haijawahi kuacha mtu salama, basi hawa wa "U sisi Wasafi" watabaguana katika madaraja 1. "U sisi wasafi walio katibu na Mwenyekiti". 2. "U sisi wasafi tuliokatikati" na 3. "U sisi wasafi tulio mbali na Mwenyekiti". Wale wa daraja la kwanza watapambana dhidi ya wale wa daraja la pili kubakia/kusogea karibu na Mwenyekiti.
Mwisho wa mtifuano huo utapelekea kudhoofika na kuanguka kwa CCM na nchi itaongozwa na Chama kipyaa kabisa. Unabii wa Mwl. Nyerere utakuwa umetimia.