Kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi, naomba kuwatakia Ramadhani Njema wale wote watakaoshiriki ibada hii muhimu!
Nasihi wafanya biashara wote nchini kutopandisha bei ya vitu muhimu hasa vyakula ili kuwezesha wanaofunga kukamilisha hili kwa amani na furaha!
Serikali ihakikishe inasimamia na kudhibiti wanaotaka kuchuma faida kubwa za duniani kwa kupandisha bei ya vyakula badala ya kutumia mwezi huu kuvuna baraka za mwenyezi Mungu kwa kutenda haki!
Wana CCM tuongoze kwa kuwa mfano bora kwa kutenda haki kwenye biashara zetu! Kwakuwa CCM ndio chama tawala, basi sisi tukiongoza kwa kutenda haki nchi yetu itapata baraka kubwa zinazotokana na mwezi huu mtukufu!
NAWATAKIA RAMADHANI NJEMA!
Nape Moses Nnauye
Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi Taifa
Nasihi wafanya biashara wote nchini kutopandisha bei ya vitu muhimu hasa vyakula ili kuwezesha wanaofunga kukamilisha hili kwa amani na furaha!
Serikali ihakikishe inasimamia na kudhibiti wanaotaka kuchuma faida kubwa za duniani kwa kupandisha bei ya vyakula badala ya kutumia mwezi huu kuvuna baraka za mwenyezi Mungu kwa kutenda haki!
Wana CCM tuongoze kwa kuwa mfano bora kwa kutenda haki kwenye biashara zetu! Kwakuwa CCM ndio chama tawala, basi sisi tukiongoza kwa kutenda haki nchi yetu itapata baraka kubwa zinazotokana na mwezi huu mtukufu!
NAWATAKIA RAMADHANI NJEMA!
Nape Moses Nnauye
Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi Taifa