CCM inafaa kutuongoza tena mwaka 2020?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,330
33,954
Kwenye mjadala huu sizungumzii kama CCM "itashinda" tena mwaka 2020 bali najaribu kuona kama chama hcho kina uhalali wa kutuongoza tena kuanzia mwaka 2020 na kuendelea. Nimechagua kuzungumzia chama badala ya watu kwa kuwa inawezekana kabisa baadhi ya watu wasiwepo lakini naamini kwamba CCM itakuwepo mwaka 2020.

CCM ni zao la TANU na ASP na vyama hivyo ndivyo viliasisi Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Muungano uliohitimishwa na Muungano wa vyama hivyo viwili kwa kuundwa kwa CCM mwaka 1977. Na kwa utashi wa vyama hivyo Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977 ikaandikwa na kuidhinishwa kutumika.

Wakati mapinduzi ya Zanzibar yanafanyika mwaka 1964, Tanganyika ilikuwa tayari imeshapata Uhuru wake toka kwa wakoloni mwaka 1961 ikifuatiwa na Zanzibar mwaka 1963. Baada ya Mapinduzi kulikuwa hakuna vyama vingine vya siasa vilivyoruhusiwa Zanzibari zaidi ya ASP, na mwaka 1965 TANU ilipiga marufuku vyama vingine vya siasa Tanganyika. Kwa mtiririko huko utaona kwamba kama kuna jambo lolote baya kwenye nchi hii kuanzia mwaka 1965 mpaka leo, ni lazima chanzo chake kiwe ni CCM.

Kama katiba ya Tanzania ni mbaya, basi wa kulaumiwa ni CCM. Kama mfumo wa kuendesha nchi umekaa shaghalabagala basi ni CCM ndiyo wamesababisha. Kwa kuwa hakuna mahali chama kingine cha siasa kimewahi kuongoza nchi hii zaidi ya CCM. Kwa ivo maovu na mabaya yote yanatokana na CCM.Lakini ni kwa nini kila wakati wa uchaguzi CCM huomba nafasi ya kurekebisha maovu yaliyosababishwa na chama hicho siku za nyuma.

Kama Mwalimu alilea uzembe hadi aliyemfuatia Ali Hassan Mwinyi aje na kauli mbiu ya "fagio la chuma" ni kwa nini tena Mkapa akaja na kaulimbiu ya "Uwazi na Ukweli' iliyopigwa kumbo na kauli mbiu ya Kikwete ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu mpya" ambayo imefutwa na kaulimbiu ya Magufuli ya "Hapa kazi tu"?

Kwa nini kila Rais anayetokana na CCM huonesha kwamba Rais aliyetangulia amemwachia nchi "chafu ama dhaifu" wakati wao wote wanatoka kwenye chama kimoja cha CCM? Mwinyi alikuwa waziri kwenye serikali ya Mwalimu, Mkapa alikuwa waziri kwenye serikali ya Mwinyi, Kikwete alikuwa waziri kwenye serikali ya Mkapa na Magufuli naye alikuwa waziri kwenye serikali ya Kikwete. Kwa nini wakiwa mawaziri hawaoneshi kwamba hali ni mbaya kiasi hicho mpaka wawe marais?

Nadhani CCM hakuna mtu anayeweza kutatua matatizo yaliyosababishwa na chama hicho kuwa madarakani. CCM inapata wapi uhalali wa kuongoza tena Tanzania kutokea mwaka 2020 na kuendelea?
 
Hakuna anayeongozwa na CCM, isipokuwa kiongozi mahiri anayeongoza kupitia chama cha ccm. sisi hatuna shida na chama isipokuwa tunataka aina ya mtu yeyote kwa chama chochoteee. hivyo kusema ccm inaongoza sio kweli kwani ccm ni chama na kiongozi anayetuongoza anatakiwa kutuongozaaa.
Kwa hiyo shida sisi sio chama sisi tunataka kiongozi mwanye ujasiri kama JPM bila kujali katokea chama kipi ndugu yanguuu!!!! sawaaa??
 
Matamko yetu hayana maana yoyote kwa taifa. Haionyeshi upinzani wenye sera na falsafa ya kimaendeleo.Kwa ujumla ni kama NGO ya kupigania haki za watu.
Sera na falsafa za maendeleo zikoje na utazitambuaje? Halafu kuwa NGO ndiyo unakuwa huna sera au falsafa ya maendeleo?
 
IMG_20170808_132358.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huna lolote kwenye uandishi wako.
Maelezo yako ni bias totally. Unachotafuta humu ni kuungwa mkono ubumbavu wako uliouleta.

Hutakosa jamii yako humu jukwaani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye mjadala huu sizungumzii kama CCM "itashinda" tena mwaka 2020 bali najaribu kuona kama chama hcho kina uhalali wa kutuongoza tena kuanzia mwaka 2020 na kuendelea. Nimechagua kuzungumzia chama badala ya watu kwa kuwa inawezekana kabisa baadhi ya watu wasiwepo lakini naamini kwamba CCM itakuwepo mwaka 2020.

CCM ni zao la TANU na ASP na vyama hivyo ndivyo viliasisi Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Muungano uliohitimishwa na Muungano wa vyama hivyo viwili kwa kuundwa kwa CCM mwaka 1977. Na kwa utashi wa vyama hivyo Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977 ikaandikwa na kuidhinishwa kutumika.

Wakati mapinduzi ya Zanzibar yanafanyika mwaka 1964, Tanganyika ilikuwa tayari imeshapata Uhuru wake toka kwa wakoloni mwaka 1961 ikifuatiwa na Zanzibar mwaka 1963. Baada ya Mapinduzi kulikuwa hakuna vyama vingine vya siasa vilivyoruhusiwa Zanzibari zaidi ya ASP, na mwaka 1965 TANU ilipiga marufuku vyama vingine vya siasa Tanganyika. Kwa mtiririko huko utaona kwamba kama kuna jambo lolote baya kwenye nchi hii kuanzia mwaka 1965 mpaka leo, ni lazima chanzo chake kiwe ni CCM.

Kama katiba ya Tanzania ni mbaya, basi wa kulaumiwa ni CCM. Kama mfumo wa kuendesha nchi umekaa shaghalabagala basi ni CCM ndiyo wamesababisha. Kwa kuwa hakuna mahali chama kingine cha siasa kimewahi kuongoza nchi hii zaidi ya CCM. Kwa ivo maovu na mabaya yote yanatokana na CCM.Lakini ni kwa nini kila wakati wa uchaguzi CCM huomba nafasi ya kurekebisha maovu yaliyosababishwa na chama hicho siku za nyuma.

Kama Mwalimu alilea uzembe hadi aliyemfuatia Ali Hassan Mwinyi aje na kauli mbiu ya "fagio la chuma" ni kwa nini tena Mkapa akaja na kaulimbiu ya "Uwazi na Ukweli' iliyopigwa kumbo na kauli mbiu ya Kikwete ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu mpya" ambayo imefutwa na kaulimbiu ya Magufuli ya "Hapa kazi tu"?

Kwa nini kila Rais anayetokana na CCM huonesha kwamba Rais aliyetangulia amemwachia nchi "chafu ama dhaifu" wakati wao wote wanatoka kwenye chama kimoja cha CCM? Mwinyi alikuwa waziri kwenye serikali ya Mwalimu, Mkapa alikuwa waziri kwenye serikali ya Mwinyi, Kikwete alikuwa waziri kwenye serikali ya Mkapa na Magufuli naye alikuwa waziri kwenye serikali ya Kikwete. Kwa nini wakiwa mawaziri hawaoneshi kwamba hali ni mbaya kiasi hicho mpaka wawe marais?

Nadhani CCM hakuna mtu anayeweza kutatua matatizo yaliyosababishwa na chama hicho kuwa madarakani. CCM inapata wapi uhalali wa kuongoza tena Tanzania kutokea mwaka 2020 na kuendelea?
Upo sahihi 100%

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mwananyaso kama andiko langu halina lolote usingejibu ulivyojibu. Ufipa-Kinondoni sioni ajabu kwa mbunge kwenda Ikulu ama rais kwenda kwenye jimbo la mbunge wa chama kingine. Hapa Iringa Magufuli alikataliwa kwa kura, lakini bado atakuja kama kutimiza majukumu yake ya kibunge.

Halafu wengine mnaosema CHADEMA walifuata juice ikulu ni kama mnaidhalilisha Ikulu yetu kwamba huwa inahonga watu. Hata hivyo kwenye hilo kundi ni nani ambaye hawezi kujinunulia Juice yake mwenyewe? Ikulu ni nyumbani na ofisini kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania.

Nimeipenda picha ya Mbowe. Mtu yeyote mwenye akli timamu kuna wakati huwa anazama kwenye lindi la mawazo akiitafakari hatma yake!
 
Ccm ina uhalali wa kungoza kwa sababu, angalau unaweza kuelewa kilipotutoa, tulipo na tunapokwenda.
tunafahamu kwamba ccm kwa kiasi kikubwa walilea mafisadi na uovu mwingi wa nchi hii na ndo waliotufikisha hapa tulipo,
tunafahamu kwamba ccm chini ya jpm inajitahidi (si kwa nadharia) bali kwa vitendo, kuondoa mafisadi na kila aina ya uovu ktk nchi hii,
Hivyo basi angalau unaona welekeo kwamba tunakwenda wapi.
Tofauti na chadema ambao wameprove failure hata kabla ya kushika dola kwa sababu zifuatazo,
- kutetea watu ambao miaka mingi walituaminisha kwamba ni mafisadi papa.
-kutokuwa na uzalendo na nchi yetu kwa kuwataka nchi wahisani wasitishe kutupatia fedha.
-kupoteza welekeo kabisa kama chama, na kuchagua kupinga kila kitu ambacho kinafanywa na serikali iliyopo madarakani, hata kama kina manufaa kwa taifa.
 
Back
Top Bottom