Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kuna jambo linasemwa humu ndani sijui kwa kutiwa chumvi au ni kwa kutokujua. Nchi hii (Tanganyika?) tangu ipate uhuru mwaka 1961 na kufuatiwa na mapinduzi ya Zanzibara mwaka 1964 hatimaye Muungano wa nchi hizo mbili uliozaa Tanzania imepita miaka 50. Tangayika kulikuwa na chama cha TANU na Zanzibar kulikuwa na chama cha ASP.
Vyama hivi viwili viliungana na kuwa chama kimoja kilichokuja kuitwa CCM hapo tarehe 5/2/1977. Kwa hiyo si sahihi kusema kwamba CCM ina miaka 50 madarakani kwani chenyewe kama chama kina miaka 34 tu tangu kuanzishwa kwake, sasa hiyo miaka 50 ya kutawala Tanzania inatoka wapi? Maana hata Tanzania yenyewe kama nchi ina miaka 47 sasa hiyo 50 ya CCM inatoka wapi?
Kuna watu wanadai kwamba hili limetokana na miaka ya CCM kuhesabiwa tangu enzi za TANU. Hoja hii huwa inanishangaza sana kwani ni lini tumeanza kuhesabu umri wa mtoto kwa kuchanganya na ule wa wazazi wake!! Nimeileta hoja hii kwani inatumiwa sana na wanasiasa wetu bila kujua kwamba wakija CCM wanakanusha kwamba chama chao hakina miaka 50 na badala yake kina miaka 34 tu. CCM huanza kwa kutumia hoja hiyo ya tofauti ya miaka kujenga hoja kwamba wapinzani ni waongo.
Vyama hivi viwili viliungana na kuwa chama kimoja kilichokuja kuitwa CCM hapo tarehe 5/2/1977. Kwa hiyo si sahihi kusema kwamba CCM ina miaka 50 madarakani kwani chenyewe kama chama kina miaka 34 tu tangu kuanzishwa kwake, sasa hiyo miaka 50 ya kutawala Tanzania inatoka wapi? Maana hata Tanzania yenyewe kama nchi ina miaka 47 sasa hiyo 50 ya CCM inatoka wapi?
Kuna watu wanadai kwamba hili limetokana na miaka ya CCM kuhesabiwa tangu enzi za TANU. Hoja hii huwa inanishangaza sana kwani ni lini tumeanza kuhesabu umri wa mtoto kwa kuchanganya na ule wa wazazi wake!! Nimeileta hoja hii kwani inatumiwa sana na wanasiasa wetu bila kujua kwamba wakija CCM wanakanusha kwamba chama chao hakina miaka 50 na badala yake kina miaka 34 tu. CCM huanza kwa kutumia hoja hiyo ya tofauti ya miaka kujenga hoja kwamba wapinzani ni waongo.