CCM ina kazi kubwa sana ili kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini!

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,976
CCM bado inakabiliwa na kazi ngumu sana ya kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini ambalo linaongozwa na Mbunge kutoka CHADEMA, Joseph Osmund Mbilinyi maarufu Sugu pamoja na kupata ushindi wa Udiwani katika kata 3 kwenye uchaguzi mdogo uliomalizika jana katika Jimbo la Mbeya Mjini.

Ukichunguza utagundua kuwa matokeo ya kura za Madiwani yanaonyesha ni jinsi gani CCM bado ina safari ndefu sana katika kurudisha Jimbo la Mbeya Mjini. Matokeo ya Kata tatu ni angalizo linalojitoshereza kwa kiwango kikubwa kuchambua kwa undani mwonekano wa siasa katika Mkoa wa Mbeya hasa Jimbo la Mbeya Mjini.

Katika Kata 3, wagombea wa CCM walipata jumla ya kura 7,851 wakati wagombea wa CHADEMA walipata kura 6,115. Tofauti ya kura ni 1.736.

Kata ya Maanga, Newton Mwatujobe (CCM) alipata kura 1897 na kumshinda, Steven Mwashilindi (CHADEMA) ambaye alipata kura 1703.

Katika Kata ya Iwambi, Humphrey Ngalawa (CCM) alipata kura 2107 huku Elisha Mwandele (CHADEMA) akipata kura 1906.

Aidha katika Kata ya Nsalaga, Kasusura, David Ngogo (CCM) alipata kura 3847 wakati Reward Mshanga (CHADEMA) akipata kura 2506.

Matokeo haya yanaweza kuwafurahisha wanaCCM lakini ukichunguza kwa undani zaidi kwa kutumia sayansi ya siasa utagundua kuwa safari ya CCM kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini bado ni ndefu sana hasa ukichukulia kuwa ni mkoa ambao unaongoza kwa kuwa na vijana wengi wajasiliamali wasio na mitaji mikubwa.

Sijui ni nani atasimama kama mgombea wa CCM katika Uchaguzi Mkuu 2020, lakini kama CCM itaendekeza siasa za ‘’kubebana’’ katika mchakato wa kumpata mgombea wa kupambana na Mbunge Mbilinyi, sitashangaa kuona Jimbo likibaki mkononi mwa Mbunge wa sasa.

Nimemuona Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dr. Tulia Ackson Mwansasu akipita huku na kule Jijini Mbeya lakini ukichunguza zaidi utagundua anatafuta fursa ya kuchaguliwa na wanaCCM kuwa mgombea Ubunge. Ninaweza kuwa siko sahihi lakini historia inaonyesha kuwa ukiona mwanasiasa anafanya jambo fulani kwa jamii lazima atakuwa anatafuta maslahi zaidi ya kisiasa!

Baada ya kumsikia Dr. Tulia kwenye majukwaa ya kisiasa akijieleza, Sina uhakika kama huyu anaweza kupambana na kushinda ubunge katika Jimbo la Mbeya Mjini. Ninaweza pia kuwa siko sahihi kama ambavyo Waziri Mkuu wa Uingereza, Harold Wilson aliwahi kusema, ‘’a week is a long time in politics!’’

Kwa matokeo haya ya jana, CCM wanatakiwa wazichange vizuri karata zao za kisiasa kama kweli wanataka kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini.
 
Mkuu kumbuka hapo ameletwa Mkurugenzi wa Jiji ambaye ni Msimamizi wa Uchaguzi, ni KAMANDA WA POLISI, kaja kwa kazi maalum hivyo kathibitisha kazi ameanza vizuri sana kwa kuchukua viti vya udiwani
 
Tume ya uchaguzi,,,, jeshi la polisi la tanzania na chama cha mapinduzi wanatakiwa waungane kujenga chama kimoja chenye nguvu cha siasa tanzania ili kishindane pasipo na kificho na vyama vya upinzani kuonesha dhamira yao ya dhati kuijenga ccm yenye nguvu kama walivyoanza kuonesha ushirikiano wao ktk baadhi ya majimbo sioni wakipata shida maana huo ushirikiano wao umezaa matunda kazi nzuri wanafanya kura za raia haziitajiki ukiwa na combination hiyo.
 
CCM bado inakabiliwa na kazi ngumu sana ya kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini ambalo linaongozwa na Mbunge kutoka CHADEMA, Joseph Osmund Mbilinyi maarufu Sugu pamoja na kupata ushindi wa Udiwani katika kata 3 kwenye uchaguzi mdogo uliomalizika jana katika Jimbo la Mbeya Mjini.

Ukichunguza utagundua kuwa matokeo ya kura za Madiwani yanaonyesha ni jinsi gani CCM bado ina safari ndefu sana katika kurudisha Jimbo la Mbeya Mjini. Matokeo ya Kata tatu ni angalizo linalojitoshereza kwa kiwango kikubwa kuchambua kwa undani mwonekano wa siasa katika Mkoa wa Mbeya hasa Jimbo la Mbeya Mjini.

Katika Kata 3, wagombea wa CCM walipata jumla ya kura 7,851 wakati wagombea wa CHADEMA walipata kura 6,115. Tofauti ya kura ni 1.736.

Kata ya Maanga, Newton Mwatujobe (CCM) alipata kura 1897 na kumshinda, Steven Mwashilindi (CHADEMA) ambaye alipata kura 1703
Katika Kata ya Iwambi, Humphrey Ngalawa (CCM) alipata kura 2107 huku Elisha Mwandele (CHADEMA) akipata kura 1906.
Aidha katika Kata ya Nsalaga, Kasusura, David Ngogo (CCM) alipata kura 3847 wakati Reward Mshanga (CHADEMA) akipata kura 2506.

Matokeo haya yanaweza kuwafurahisha wanaCCM lakini ukichunguza kwa undani zaidi kwa kutumia sayansi ya siasa utagundua kuwa safari ya CCM kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini bado ni ndefu sana hasa ukichukulia kuwa ni mkoa ambao unaongoza kwa kuwa na vijana wengi wajasiliamali wasio na mitaji mikubwa.

Sijui ni nani atasimama kama mgombea wa CCM katika Uchaguzi Mkuu 2020, lakini kama CCM itaendekeza siasa za ‘’kubebana’’ katika mchakato wa kumpata mgombea wa kupambana na Mbunge Mbilinyi, sitashangaa kuona Jimbo likibaki mkononi mwa Mbunge wa sasa.

Nimemuona Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dr. Tulia Ackson Mwansasu akipita huku na kule Jijini Mbeya lakini ukichunguza zaidi utagundua anatafuta fursa ya kuchaguliwa na wanaCCM kuwa mgombea Ubunge. Ninaweza kuwa siko sahihi lakini historia inaonyesha kuwa ukiona mwanasiasa anafanya jambo fulani kwa jamii lazima atakuwa anatafuta maslahi zaidi ya kisiasa!

Baada ya kumsikia Dr. Tulia kwenye majukwaa ya kisiasa akijieleza, Sina uhakika kama huyu anaweza kupambana na kushinda ubunge katika Jimbo la Mbeya Mjini. Ninaweza pia kuwa siko sahihi kama ambavyo Waziri Mkuu wa Uingereza, Harold Wilson aliwahi kusema, ‘’a week is a long time in politics!’’

Kwa matokeo haya ya jana, CCM wanatakiwa wazichange vizuri karata zao za kisiasa kama kweli wanataka kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini.
Uchambuzi wako uko sahihi. Siasa za Mbeya mjini ni upinzani wa kukomoana baina ya Wanyakyusa (wakuja wenye majidai na dharau dhidi ya wenyeji) na Wasafwa pamoja na wageni wengine (wanaodharauliwa kwa ufukara wao). Nimeishi na kufanya tafiti za kisiasa na kijamii Mbeya. Siasa za hapo ninazijua na ni za siku nyingi (historical). Msigano huo wa kijamii ndio mtaji wa Sugu (siyo Mnyakyusa). CCM wakitaka kulirudisha jimbo la Mbeya mjini waachane na Tulia (pengine wamtafutie jimbo jingine mkoani humo, kama hapana budi). Atafutwe Msafwa au mgeni mwingine apambane na Sugu. Chadema ni coincidental beneficiary wa Siasa za kikabila na kudharauliana za Mbeya.
 
CCM bado inakabiliwa na kazi ngumu sana ya kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini ambalo linaongozwa na Mbunge kutoka CHADEMA, Joseph Osmund Mbilinyi maarufu Sugu pamoja na kupata ushindi wa Udiwani katika kata 3 kwenye uchaguzi mdogo uliomalizika jana katika Jimbo la Mbeya Mjini.

Kwa matokeo haya ya jana, CCM wanatakiwa wazichange vizuri karata zao za kisiasa kama kweli wanataka kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini.
Kwa maoni yangu, kwa uchaguzi wa mwaka 2020, jimbo pekee ambalo CCM itapata taabu sana kulikomboa ni jimbo moja tuu la Zitto, kwa sababu determinant ya ushindi sio sera, sio chama wala sio wapigakura bali ni mtu wao.
P
 
Yaani pamoja na kushinda kata hizo tatu bado huoni ni kiashiria cha uwezekano Wa CDM kupoteza!? Kwa nn usitumie fact hzo hzo za udiwani Ku justify kwamba CDM wanaweza kupoteza?
Mkuu,
Sijasema kuwa CCM hawawezi kulikomboa Jimbo. Nilichosema ni jinsi gani ilivyo vigumu sana kutokana na matokeo ya uchaguzi na mazingira ya kisiasa kwa sasa.
 
Acha utani wewe. Nilidhani utatuambiwa kuwa mwaka huo CCM itapata 95% kama Monduli. Maana kwa sasa sanduku la kura halina maana sana. Ni jinsi Mkurugenzi na NEC wanavyo amua kugawa kura (vote allocation) kwa mpendwa wenu mgombea kupitia CCM . Acha kuhadaa watu...Nitapiga kura tena baada ya Jiwe kumaliza kipindi chake ....otherwise big No
 
Uchambuzi wako uko sahihi. Siasa za Mbeya mjini ni upinzani wa kukomoana baina ya Wanyakyusa (wakuja wenye majidai na dharau dhidi ya wenyeji) na Wasafwa pamoja na wageni wengine (wanaodharauliwa kwa ufukara wao). Nimeishi na kufanya tafiti za kisiasa na kijamii Mbeya. Siasa za hapo ninazijua na ni za siku nyingi (historical). Msigano huo wa kijamii ndio mtaji wa Sugu (siyo Mnyakyusa). CCM wakitaka kulirudisha jimbo la Mbeya mjini waachane na Tulia (pengine wamtafutie jimbo jingine mkoani humo, kama hapana budi). Atafutwe Msafwa au mgeni mwingine apambane na Sugu. Chadema ni coincidental beneficiary wa Siasa za kikabila na kudharauliana za Mbeya.
Mkuu;
Ninakushukuru sana kwa kuzichambua vizuri siasa za Mbeya.

Nadhani mchakato wa kumpata mgombea wa CCM katika jimbo hilo ndio utakaochagiza ushindi au kushindwa.
 
mkuu. huko mbeya huo ushindi wa madiwani watatu umepatikana kws usaidizi wa polis, tume na wasimamizi. wa uchaguzi ambao ni uvccm. hata mwaka 2020 kazi itakuwa hiyo hiyo. uchakachuaji uchakachuaji. mawakala wa upinzani watawekwa pembeni marufuku kuingia vituoni.
 
Back
Top Bottom