CCM ina kazi kubwa sana ili kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini!

Uchambuzi wako uko sahihi. Siasa za Mbeya mjini ni upinzani wa kukomoana baina ya Wanyakyusa (wakuja wenye majidai na dharau dhidi ya wenyeji) na Wasafwa pamoja na wageni wengine (wanaodharauliwa kwa ufukara wao). Nimeishi na kufanya tafiti za kisiasa na kijamii Mbeya. Siasa za hapo ninazijua na ni za siku nyingi (historical). Msigano huo wa kijamii ndio mtaji wa Sugu (siyo Mnyakyusa). CCM wakitaka kulirudisha jimbo la Mbeya mjini waachane na Tulia (pengine wamtafutie jimbo jingine mkoani humo, kama hapana budi). Atafutwe Msafwa au mgeni mwingine apambane na Sugu. Chadema ni coincidental beneficiary wa Siasa za kikabila na kudharauliana za Mbeya.
Umeongea point kubwa sana. Kwa wasio zijua siasa za Mbeya hawawezi kukuelewa. Ukitazama hata ushindi wa Sugu 2010 ni kwa sababu CCM Mbeya waliziba masikio na kuendelea na ujinga wao . CCM Mbeya sio wasikivu na hawajifunzi kutokana na makosa. Sugu anatumia sana advantage ya udhaifu wa CCM kuwateka wana Mbeya.

Kumsimamisha Shitambala 2015 ilikua ni kosa kubwa sana na hata zile kura 60k walizipata kwa wanaCCM kindakindaki tu. Na kosa kubwa sana ni kumfunga sugu bila kujua wanamuongezea Kiki kwa wananchi.

Katika majimbo yanayopata tabu kwa hizi siasa za CHADEMA/CCM basi Mbeya ni ya kwanza. Limekua Jimbo yatima kwa sababu serikali haitaki kufanya chochote kwa kuwa wakifanya Kitu credit atapata sugu na CHADEMA. Hizi siasa zimetuletea madiwani wadhaifu sana kwa sababu raia waliamua kuikomoa CCM kwa kuchagua CHADEMA hata kama wengi wa wagombea wao hawakua na sifa. Mfano mzuri ni kata ya Isanga ilikua inapiga hatua kimaendeleo ila hizi chuki za CCM/CHADEMA zimeirudisha sana nyuma baada ya kumpiga chini diwani wao mzuri wa CCM.

Kati ya NSSF au NHC walikua tayari kujenga Mall kubwa pale lilipokua Soko la uhindini lakini hizi siasa za majitaka zimepelekea mpaka leo lile eneo lipolipo tu. Sasa wakienda kujenga mkoa mwingine tutaanza kulalamika kuwa watu/mashirika hawataki kuwekeza Mbeya Kumbe hatuna Sera nzuri tu.

Hata timu ya Mbeya city imekumbwa na huu msukosuko. Inakwepa kushuka daraja kabla hata msimu haujaanza. Ikifika 2020 utaona wanasiasa watakavojipendekeza kuipa msaada wakati saizi ina ukata utafikiri ni timu ya walalahoi kama majimaji.

Kama 2020 Sugu (CHADEMA haina ubavu wa kusimamisha mgombea tofauti na yeye ) atapita na CHADEMA ikashika tena halimashauri basi maendeleo Mbeya yatabaki kuwa ndoto za mchana. Japo tunaichukia CCM lakini CHADEMA Mbeya sio mbadala sahihi wa CCM. Yaani wave of change iliwabeba sana CDM na athari tunaiona saizi.

Japo hatupendi ila hii ndio hali halisi ya Mbeya
 
Kwa maoni yangu, kwa uchaguzi wa mwaka 2020, jimbo pekee ambalo CCM itapata taabu sana kulikomboa ni jimbo moja tuu la Zitto, kwa sababu determinant ya ushindi sio sera, sio chama wala sio wapigakura bali ni mtu wao.
P
Kuna majimbo mengi tu ambayo CCM itapata shida sana kushinda!

Kwamba Zitto ni mtu wao! Siwezi kukubishia sana kwa angalizo lako!

What will happen when Zitto goes roque?
 
Kwa maoni yangu, kwa uchaguzi wa mwaka 2020, jimbo pekee ambalo CCM itapata taabu sana kulikomboa ni jimbo moja tuu la Zitto, kwa sababu determinant ya ushindi sio sera, sio chama wala sio wapigakura bali ni mtu wao.
P
mku p. hakuna jimbo gumu kwa ccm 2020, kwa ushirikiano wa tume, polis. na uvccm na makada wengine kama sehemu ya wasimamizi wa tume. unakosea sana kuamini ccm inatishwa na foleni za wapiga kura. kwo kikubwa karani anayeandika matokeo. pia mawakala wa zitto wataswagwa nje.
 
Kipimo rahisi tu wamshauri ajiuzulu ubunge kisha atangaze tena nia ya kugombea hapo kitakua kipimo tosha kuelekea 2020...
 
CCM bado inakabiliwa na kazi ngumu sana ya kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini ambalo linaongozwa na Mbunge kutoka CHADEMA, Joseph Osmund Mbilinyi maarufu Sugu pamoja na kupata ushindi wa Udiwani katika kata 3 kwenye uchaguzi mdogo uliomalizika jana katika Jimbo la Mbeya Mjini.

Ukichunguza utagundua kuwa matokeo ya kura za Madiwani yanaonyesha ni jinsi gani CCM bado ina safari ndefu sana katika kurudisha Jimbo la Mbeya Mjini. Matokeo ya Kata tatu ni angalizo linalojitoshereza kwa kiwango kikubwa kuchambua kwa undani mwonekano wa siasa katika Mkoa wa Mbeya hasa Jimbo la Mbeya Mjini.

Katika Kata 3, wagombea wa CCM walipata jumla ya kura 7,851 wakati wagombea wa CHADEMA walipata kura 6,115. Tofauti ya kura ni 1.736.

Kata ya Maanga, Newton Mwatujobe (CCM) alipata kura 1897 na kumshinda, Steven Mwashilindi (CHADEMA) ambaye alipata kura 1703.

Katika Kata ya Iwambi, Humphrey Ngalawa (CCM) alipata kura 2107 huku Elisha Mwandele (CHADEMA) akipata kura 1906.

Aidha katika Kata ya Nsalaga, Kasusura, David Ngogo (CCM) alipata kura 3847 wakati Reward Mshanga (CHADEMA) akipata kura 2506.

Matokeo haya yanaweza kuwafurahisha wanaCCM lakini ukichunguza kwa undani zaidi kwa kutumia sayansi ya siasa utagundua kuwa safari ya CCM kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini bado ni ndefu sana hasa ukichukulia kuwa ni mkoa ambao unaongoza kwa kuwa na vijana wengi wajasiliamali wasio na mitaji mikubwa.

Sijui ni nani atasimama kama mgombea wa CCM katika Uchaguzi Mkuu 2020, lakini kama CCM itaendekeza siasa za ‘’kubebana’’ katika mchakato wa kumpata mgombea wa kupambana na Mbunge Mbilinyi, sitashangaa kuona Jimbo likibaki mkononi mwa Mbunge wa sasa.

Nimemuona Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dr. Tulia Ackson Mwansasu akipita huku na kule Jijini Mbeya lakini ukichunguza zaidi utagundua anatafuta fursa ya kuchaguliwa na wanaCCM kuwa mgombea Ubunge. Ninaweza kuwa siko sahihi lakini historia inaonyesha kuwa ukiona mwanasiasa anafanya jambo fulani kwa jamii lazima atakuwa anatafuta maslahi zaidi ya kisiasa!

Baada ya kumsikia Dr. Tulia kwenye majukwaa ya kisiasa akijieleza, Sina uhakika kama huyu anaweza kupambana na kushinda ubunge katika Jimbo la Mbeya Mjini. Ninaweza pia kuwa siko sahihi kama ambavyo Waziri Mkuu wa Uingereza, Harold Wilson aliwahi kusema, ‘’a week is a long time in politics!’’

Kwa matokeo haya ya jana, CCM wanatakiwa wazichange vizuri karata zao za kisiasa kama kweli wanataka kulikomboa Jimbo la Mbeya Mjini.
Naona mbeya Mkurugenzi hajateuliwa na rais, na tume ya uchaguz ni huru kabisa
 
Tatizo langu ni muda katika kutimiza hiyo kazi kubwa ya CCM.

Jimbo la Mbeya Mjini lina vikwazo vingi sana kisiasa.
Niliona Monduli ndio jimbo lenye vikwazo hasa kuliko hata Mbeya Mjini!

Ila kilichofanyika Monduli katika uchaguzi wa Marudio ya Jumamosi nimebaki kinywa wazi!


Yani CHADEMA na LOWASSA nyumbani kwao, tena katika kabila lenye msimamo na mshikamano kama Masai eti anazawadiwa asilumia 3% ya kura zote zaidi ya elfu sitini?

Kama Monduli CCM wameweza sioni mahali ambapi watashindwa!

Huu ni uchaguzi uliokuwa na maajabu kuliko maajabu yale saba ya dunia!
 
mkuu. huko mbeya huo ushindi wa madiwani watatu umepatikana kws usaidizi wa polis, tume na wasimamizi. wa uchaguzi ambao ni uvccm. hata mwaka 2020 kazi itakuwa hiyo hiyo. uchakachuaji uchakachuaji. mawakala wa upinzani watawekwa pembeni marufuku kuingia vituoni.
Mkuu nashangaa sana watu wanajibaraguza hapa eti siasa za Mbeya...Demokrasia iko kwenye majaribu makubwa sana kwa sasa. Wana CCM wanatuhadaa hapa as if hawajui kinachotokea ndani ya vyumba vya kuhesabia kura. They know much. Mpaka sasa wanauhakika wa kuchukua majimbo yote isipokuwa Mbeya na kwa Zito....Pathetic.
 
Yaani pamoja na kushinda kata hizo tatu bado huoni ni kiashiria cha uwezekano Wa CDM kupoteza!? Kwa nn usitumie fact hzo hzo za udiwani Ku justify kwamba CDM wanaweza kupoteza?
Ana maana kuwa kwa kuangalia kwa undani nguvu kubwa iliyotumika ya Polisi+NEC+DC&RC, bado ushindi ni kiduchu hivyo.......

Imagine kuwa 2020 kuna uchaguzi nchi nzima hivyo hawawezi kujigawa!

Hiyo ndiyo tafsiri yake
 
Ana maana kuwa kwa kuangalia kwa undani nguvu kubwa iliyotumika ya Polisi+NEC+DC&RC, bado ushindi ni kiduchu hivyo.......

Imagine kuwa 2020 kuna uchaguzi nchi nzima hivyo hawawezi kujigawa!

Hiyo ndiyo tafsiri yake
Wana uwezo wa kumteka mgembea wa Chadema ili asirudishe form ili mgombea wa CCM atangazwe mshindi kupungunza bugudha....it is possible too.
 
Ukitaka kujua CCM iliamua kwa dhati kabisa kukomboa majimbo na kata zilizoenda upinzani, angalia matokeo ya chaguzi za marudio.
 
Umeongea point kubwa sana. Kwa wasio zijua siasa za Mbeya hawawezi kukuelewa. Ukitazama hata ushindi wa Sugu 2010 ni kwa sababu CCM Mbeya waliziba masikio na kuendelea na ujinga wao . CCM Mbeya sio wasikivu na hawajifunzi kutokana na makosa. Sugu anatumia sana advantage ya udhaifu wa CCM kuwateka wana Mbeya.

Kumsimamisha Shitambala 2015 ilikua ni kosa kubwa sana na hata zile kura 60k walizipata kwa wanaCCM kindakindaki tu. Na kosa kubwa sana ni kumfunga sugu bila kujua wanamuongezea Kiki kwa wananchi.

Katika majimbo yanayopata tabu kwa hizi siasa za CHADEMA/CCM basi Mbeya ni ya kwanza. Limekua Jimbo yatima kwa sababu serikali haitaki kufanya chochote kwa kuwa wakifanya Kitu credit atapata sugu na CHADEMA. Hizi siasa zimetuletea madiwani wadhaifu sana kwa sababu raia waliamua kuikomoa CCM kwa kuchagua CHADEMA hata kama wengi wa wagombea wao hawakua na sifa. Mfano mzuri ni kata ya Isanga ilikua inapiga hatua kimaendeleo ila hizi chuki za CCM/CHADEMA zimeirudisha sana nyuma baada ya kumpiga chini diwani wao mzuri wa CCM.

Kati ya NSSF au NHC walikua tayari kujenga Mall kubwa pale lilipokua Soko la uhindini lakini hizi siasa za majitaka zimepelekea mpaka leo lile eneo lipolipo tu. Sasa wakienda kujenga mkoa mwingine tutaanza kulalamika kuwa watu/mashirika hawataki kuwekeza Mbeya Kumbe hatuna Sera nzuri tu.

Hata timu ya Mbeya city imekumbwa na huu msukosuko. Inakwepa kushuka daraja kabla hata msimu haujaanza. Ikifika 2020 utaona wanasiasa watakavojipendekeza kuipa msaada wakati saizi ina ukata utafikiri ni timu ya walalahoi kama majimaji.

Kama 2020 Sugu (CHADEMA haina ubavu wa kusimamisha mgombea tofauti na yeye ) atapita na CHADEMA ikashika tena halimashauri basi maendeleo Mbeya yatabaki kuwa ndoto za mchana. Japo tunaichukia CCM lakini CHADEMA Mbeya sio mbadala sahihi wa CCM. Yaani wave of change iliwabeba sana CDM na athari tunaiona saizi.

Japo hatupendi ila hii ndio hali halisi ya Mbeya
Ninapenda sana watu wanaodadavua masuala ya kisiasa kama ulivyofanya.

Tatizo linalokumba kwa sasa hili jukwaa la siasa hapa Jamiiforums ni kuwa na wachangiaji wa sentesi moja yenye kutafuta LIKES za wajinga!

Kwa sasa watu wenye uelewa mpana wanasoma heading na thread tu halafu wanaenda kwenye thread nyingine kwa sababu ni kupoteza muda kusoma michango ya wachangiaji wa thread kutokana na michango ya kitoto au kijinga.

Usichoke kutoa elimu kwa faida yetu tunaopenda kusoma michango yenye kufikirisha zaidi.
 
Back
Top Bottom