Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,443
- 113,452
Kwa vile Uchaguzi wa 2010 bado, kuandika kuwa CCM imeishashinda, Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar, itaonekana kama ni utabiri, huu sio utabiri bali ni mwelekeo halisi wa kitakachotokea kutokana na kinachoendelea sasa kwa mujibu wa historia ya siasa za Zanzibar.
Nikiwa Sekondari ya Tambaza miaka ile, hakuna cha kuchagua masomo ya sayansi wala arts, ni kusoma yote mumo kwa mumo. Nlipomaliza nikajikuta combi zote zimekubali, kuanzia PCM, PCB, PGM,EGM, ECA, CBG, HGE, HGK, NA HGL, mimi nilichagua HGL kwa sababu tuu ya kulipenda somo la Historia na kijiunga Ilboru.
History is the study of the past in relation to the present to determine the future. Yaani Historia ni somo la kuangalia mambo ya zamani na kuyahusianisha na mambo ya sasa ili kujua mambo yajayo. Kwa kifupi ni kuangalia tulikotoka tukilinganisha na tulipo ili tujue tunapokwenda.
Historia ya siasa za Zanzibar inaonyesha hakuna ushindi uso hila, tangu ule wa 1963 ulioleta uhuru uliodumu kwa mwezi mmoja, ukafuatiwa na Mapinduzi ambayo yameendesha siasa za kibabe mpaka uliporudi mfumo wa vyama vingi, yanajirudia yale yale ya kabla ya uhuru.
Uchaguzi wa 1995, nilibahatika kuwako Zanzibar, nikayashuhudia niliyoyashuhudia, mwaka 2000 nikawa tena Zanzibar na kuona nilichoona, 2005 nilifanya kusikia nilichosikia, na 2010 ndio nawaelezeni kinachofuatia.
Ili chama chochote kishinde Zanzibar, hakuna ushindi safi wa kwenye kisahani cha chai, ushindi kule ni mbinu ziwe safi au chafu almuradi akeshatangazwa mshindi, mshindwa ni kugojelea miaka mitano mengine.
CCM wana jua mbinu walizotumia 1995, za 2000 na za 2005 zisingeweza kufua dafu kwa 2010, hivyo wana historia wenye kuona mbali, wakalitumia Baraza la Wawakilishi kuwaingiza mkenge CUF kwa kupitisha sheria ya ukaazi ambayo sasa ndio mpini wa ushindi wa CCM Zanzibar na kinachotokea Pemba sasa, ni juhudi za kunyanganyana kisu huku CCM ameshika mpini. CUF kwenye makali, matokeo yake ni CUF kujikata, au kukatwa kwa risasi, vifaru, mabomu ya machozi, maji ya upupu na wengi kuishia magerezani na mshindi ni CCM.
Hivi hao wawakilishi wa CUF walipokubali haki ya msingi ya kikatiba ya kuruhusu Wazanzibari kushiriki uchaguzi, itiwe mfukoni na sheria ya ukaazi, hawakuliona hilo?. Hivi hawakujiuliza "What was the motive behind? Habari ndio hiyo!.
CCM walijua kwa njia ya kawaida hawashindi, wanaitumia sheria ya ukaazi kuhakikisha CUF hawaandikishwi ili hata wapigakura jimbo zima wakibaki wawili, au mbunge amechaguliwa kwa kura moja, huyo huyo mwenye kura moja ndio mshindi , tena mbunge halali wa CCM!.
CUF nadhani somo hilo limeeleweka, ukweli umeanza kujulikana, naona mnachotaka kukifanya Pemba ni kupafanya pawe hapaliki wala hapalaliki, ama hapakaliki wala hapatawaliki. Ingekuwa ni enzi za Zambibar huru, CUF nanyi mgefanya mapinduzi yenu ya kisiwa cha Pemba na kujitangazia uhuru, lakini sasa Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT, mutaletewa majamaa wa UWT, jeshi na Polisi na kudhibitiwa mpaka mtu kwa mtu mkose pa kupumulia ali murad CCM iendelee kutawala.
Kwa maoni yangu, kama hamtaweza kutumia njia halali kukifuta kipengele cha sheria kandamizi ya ukaazi, hesabuni uchaguzi 2010 umeisha, jikusanyeni, mjipange upya kwa 2015 tena ziwe enzi za kina Juma Duni sasa maana Wazee waacheni wapumzike.
Nikiwa Sekondari ya Tambaza miaka ile, hakuna cha kuchagua masomo ya sayansi wala arts, ni kusoma yote mumo kwa mumo. Nlipomaliza nikajikuta combi zote zimekubali, kuanzia PCM, PCB, PGM,EGM, ECA, CBG, HGE, HGK, NA HGL, mimi nilichagua HGL kwa sababu tuu ya kulipenda somo la Historia na kijiunga Ilboru.
History is the study of the past in relation to the present to determine the future. Yaani Historia ni somo la kuangalia mambo ya zamani na kuyahusianisha na mambo ya sasa ili kujua mambo yajayo. Kwa kifupi ni kuangalia tulikotoka tukilinganisha na tulipo ili tujue tunapokwenda.
Historia ya siasa za Zanzibar inaonyesha hakuna ushindi uso hila, tangu ule wa 1963 ulioleta uhuru uliodumu kwa mwezi mmoja, ukafuatiwa na Mapinduzi ambayo yameendesha siasa za kibabe mpaka uliporudi mfumo wa vyama vingi, yanajirudia yale yale ya kabla ya uhuru.
Uchaguzi wa 1995, nilibahatika kuwako Zanzibar, nikayashuhudia niliyoyashuhudia, mwaka 2000 nikawa tena Zanzibar na kuona nilichoona, 2005 nilifanya kusikia nilichosikia, na 2010 ndio nawaelezeni kinachofuatia.
Ili chama chochote kishinde Zanzibar, hakuna ushindi safi wa kwenye kisahani cha chai, ushindi kule ni mbinu ziwe safi au chafu almuradi akeshatangazwa mshindi, mshindwa ni kugojelea miaka mitano mengine.
CCM wana jua mbinu walizotumia 1995, za 2000 na za 2005 zisingeweza kufua dafu kwa 2010, hivyo wana historia wenye kuona mbali, wakalitumia Baraza la Wawakilishi kuwaingiza mkenge CUF kwa kupitisha sheria ya ukaazi ambayo sasa ndio mpini wa ushindi wa CCM Zanzibar na kinachotokea Pemba sasa, ni juhudi za kunyanganyana kisu huku CCM ameshika mpini. CUF kwenye makali, matokeo yake ni CUF kujikata, au kukatwa kwa risasi, vifaru, mabomu ya machozi, maji ya upupu na wengi kuishia magerezani na mshindi ni CCM.
Hivi hao wawakilishi wa CUF walipokubali haki ya msingi ya kikatiba ya kuruhusu Wazanzibari kushiriki uchaguzi, itiwe mfukoni na sheria ya ukaazi, hawakuliona hilo?. Hivi hawakujiuliza "What was the motive behind? Habari ndio hiyo!.
CCM walijua kwa njia ya kawaida hawashindi, wanaitumia sheria ya ukaazi kuhakikisha CUF hawaandikishwi ili hata wapigakura jimbo zima wakibaki wawili, au mbunge amechaguliwa kwa kura moja, huyo huyo mwenye kura moja ndio mshindi , tena mbunge halali wa CCM!.
CUF nadhani somo hilo limeeleweka, ukweli umeanza kujulikana, naona mnachotaka kukifanya Pemba ni kupafanya pawe hapaliki wala hapalaliki, ama hapakaliki wala hapatawaliki. Ingekuwa ni enzi za Zambibar huru, CUF nanyi mgefanya mapinduzi yenu ya kisiwa cha Pemba na kujitangazia uhuru, lakini sasa Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT, mutaletewa majamaa wa UWT, jeshi na Polisi na kudhibitiwa mpaka mtu kwa mtu mkose pa kupumulia ali murad CCM iendelee kutawala.
Kwa maoni yangu, kama hamtaweza kutumia njia halali kukifuta kipengele cha sheria kandamizi ya ukaazi, hesabuni uchaguzi 2010 umeisha, jikusanyeni, mjipange upya kwa 2015 tena ziwe enzi za kina Juma Duni sasa maana Wazee waacheni wapumzike.
Last edited by a moderator: