voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,553
- 11,885
Inawezekana laana za "wabaya"sasa zimeanza kufanya kazi yake ndani ya CCM hii.kama mmefikia kujiita Chawa wa Taifa!
Halafu mnaamini Kwamba Sophia atakuwa bora majukwaani,katika kipindi ambacho Siasa za majukwaani zinaenda kuanza rasmi.
Na kwamba atamzidi Shaka aliyekuwepo? Ambaye hata yeye alikuwa ni mwepesi kama cream ya uso! Muda utaongea soon!
Tatizo ni kwamba CCM mnaishi kwa kukariri! Juzi sio jana, na jana sio leo. Na pia leo haitakuwa hivi mpaka 2025 au 2030!
Watu sasa hawaangalii majina ya wanasiasa. Bali watu wanamsikiliza mtoa hoja na sera makini, na inayogusa kile wanachokiishi huku site!
Maana tumejua rasmi kwamba,wengi wa wanasiasa ndani ya CCM. Mpo hapo kwa maslahi yenu na makundi yenu ya kimfumo.
Msidhani ni wakati ule wananchi walipokuwa wakishabikia vyama kama timu za mpira!
Kwamba yeyote atakayewekwa,ilimradi amesajiliwa na timu,basi atashangiliwa pia na wananchi, La hasha!
Mambo yamebadilika sana,tumejifunza mengi sana! Mnapobadilishana vyeo kama magari, mnapobadilishana bila kutafakari ni nani anaweza nini?
Na anaweza kwa kiasi gani kulisimamia jukwaa na kuongea na wananchi kwa kujua nini hasa wanakihitaji!
Mnapobadili viongozi, kwa kuangalia wanaowafaa nyinyi, kwa maslahi yenu.
Badala ya kuchagua kwa kuangalia wanaowafaa wananchi, kwa maslahi yao na maendeleo ya taifa letu!
Inaweza kuwa ndio anguko lenu linaanza kujitokeza.
Sio kwa hali hii,ambapo tunaona ufisadi ukirudi na kuitafuna CCM, kama ilivyokuwa kabla ya 2015.
Kama hamuamini,tumieni mfano wa kilichotokea juzi huko Mwanza,kati ya Mkurugenzi wa jiji, na kamati ya ulinzi na usalama mkoa.
Tangu siasa za 2015 huko upinzani na pia CCM,hadi 2020! Na kuja mpaka tulipo sasa!
Wananchi wamejifunza mengi sana kutoka matendo ya nyinyi viongozi wa kisiasa nchi hii.
Wameujua ukweli na uhalisia wenu kimatendo na nafsi zenu!
Tumewajua wauaji, tumewajua wezi,tumewajua wanasiasa CCM wanafiki na pia tumewajua wanasiasa wazuri,ambao wanabaniwa na vyama vyao.
Kwa sababu ya ukweli na uzalendo wao.
Kwa hiyo msitarajie wananchi kukurupukia mikutano,ambayo itakosa sera madhubuti ili kugusa utatuzi wa kero zao za kimaisha ya kila siku.
"Wananchi wanalia na mfumuko wa bei,pamoja na Tozo lukuki zinazowafilisi kila uchao huko mitaani."
"Wananchi wanalia na huduma mbovu za kijamii, kuanzia hospitalini mpaka Polisi na ofisi zote nyeti za Umma"
Wakati nyinyi mnagawiana magari ya kifahari ya milioni 500 kwa milioni 600. maofisini,mikoani hadi wilayani.
Wananchi nao wanataabika kuanzia mikoani hadi vijijini. Kwa mfumuko wa bei,ambao hauhusiani hata na vita ya Ukraine na Russia.
Nyama ya Ng'ombe,Mchele,Unga wa Mahindi ni mifano tosha wa hilo.
Tunawasubiri majukwaani na tutawapimia huko. Na pia majibu mtayapata huko huko.
Ilimradi msikae kwa kutegemea maguvu ya Dola mlioishikilia kwa sasa!
Kuweni fair na muache wananchi wawe huru kuamua mbichi na mbivu.
Jumapili njema!
Alamsikhi.
10101.
View attachment 2481544
Halafu mnaamini Kwamba Sophia atakuwa bora majukwaani,katika kipindi ambacho Siasa za majukwaani zinaenda kuanza rasmi.
Na kwamba atamzidi Shaka aliyekuwepo? Ambaye hata yeye alikuwa ni mwepesi kama cream ya uso! Muda utaongea soon!
Tatizo ni kwamba CCM mnaishi kwa kukariri! Juzi sio jana, na jana sio leo. Na pia leo haitakuwa hivi mpaka 2025 au 2030!
Watu sasa hawaangalii majina ya wanasiasa. Bali watu wanamsikiliza mtoa hoja na sera makini, na inayogusa kile wanachokiishi huku site!
Maana tumejua rasmi kwamba,wengi wa wanasiasa ndani ya CCM. Mpo hapo kwa maslahi yenu na makundi yenu ya kimfumo.
Msidhani ni wakati ule wananchi walipokuwa wakishabikia vyama kama timu za mpira!
Kwamba yeyote atakayewekwa,ilimradi amesajiliwa na timu,basi atashangiliwa pia na wananchi, La hasha!
Mambo yamebadilika sana,tumejifunza mengi sana! Mnapobadilishana vyeo kama magari, mnapobadilishana bila kutafakari ni nani anaweza nini?
Na anaweza kwa kiasi gani kulisimamia jukwaa na kuongea na wananchi kwa kujua nini hasa wanakihitaji!
Mnapobadili viongozi, kwa kuangalia wanaowafaa nyinyi, kwa maslahi yenu.
Badala ya kuchagua kwa kuangalia wanaowafaa wananchi, kwa maslahi yao na maendeleo ya taifa letu!
Inaweza kuwa ndio anguko lenu linaanza kujitokeza.
Sio kwa hali hii,ambapo tunaona ufisadi ukirudi na kuitafuna CCM, kama ilivyokuwa kabla ya 2015.
Kama hamuamini,tumieni mfano wa kilichotokea juzi huko Mwanza,kati ya Mkurugenzi wa jiji, na kamati ya ulinzi na usalama mkoa.
Tangu siasa za 2015 huko upinzani na pia CCM,hadi 2020! Na kuja mpaka tulipo sasa!
Wananchi wamejifunza mengi sana kutoka matendo ya nyinyi viongozi wa kisiasa nchi hii.
Wameujua ukweli na uhalisia wenu kimatendo na nafsi zenu!
Tumewajua wauaji, tumewajua wezi,tumewajua wanasiasa CCM wanafiki na pia tumewajua wanasiasa wazuri,ambao wanabaniwa na vyama vyao.
Kwa sababu ya ukweli na uzalendo wao.
Kwa hiyo msitarajie wananchi kukurupukia mikutano,ambayo itakosa sera madhubuti ili kugusa utatuzi wa kero zao za kimaisha ya kila siku.
"Wananchi wanalia na mfumuko wa bei,pamoja na Tozo lukuki zinazowafilisi kila uchao huko mitaani."
"Wananchi wanalia na huduma mbovu za kijamii, kuanzia hospitalini mpaka Polisi na ofisi zote nyeti za Umma"
Wakati nyinyi mnagawiana magari ya kifahari ya milioni 500 kwa milioni 600. maofisini,mikoani hadi wilayani.
Wananchi nao wanataabika kuanzia mikoani hadi vijijini. Kwa mfumuko wa bei,ambao hauhusiani hata na vita ya Ukraine na Russia.
Nyama ya Ng'ombe,Mchele,Unga wa Mahindi ni mifano tosha wa hilo.
Tunawasubiri majukwaani na tutawapimia huko. Na pia majibu mtayapata huko huko.
Ilimradi msikae kwa kutegemea maguvu ya Dola mlioishikilia kwa sasa!
Kuweni fair na muache wananchi wawe huru kuamua mbichi na mbivu.
Jumapili njema!
Alamsikhi.
10101.
View attachment 2481544