CCM imedumaza uwezo wetu wa kufikiri, hadi wanaofikiri sawasawa wameanza kuchukiwa

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,330
33,951
Baada ya Mapinduzi (matukufu?) ya Zanzibar Mwaka 1964, chama cha ASP kikapiga marufuku vyama vingine vya siasa na kuharamisha viongozi wake. Ukiwa Zanzibar ilikuwa ama uwe ASP au uwe adui wa Mapinduzi. Kwa ivo kila mtu aliyetaka kufanya siasa Zanzibar ilibidi ajiunge na ASP ili afanye siasa na awe salama. Hapa kuna kumbukizi ya utata kwa watu kama Kina Kassim Hanga walikufaje na Salim Ahmed Salim ambaye ililazimika apewe Ubalozi wa Tanzania ili kumnusuru na hisia dhidi yake kwamba yeye ni Hizbu.

Tanganyika nako baada ya uchaguzi wa vyama vingi Mwaka 1965, TANU ilipiga marufuku vyama vingine vya siasa na kubakia peke yake. Hapo napo ndiyo kwenye ile misukosuko iliyowapata kina Abdalah Fundikira na baadhi ya wenzake. Kulikuwa kuna kundi kubwa sana ndani ya TANU ambalo lilikuwa halikubaliani na TANU lakini kwa kuwa vyama vingine vilikuwa vimepigwa marufuku, kundi hilo la watu ilibidi kuvumilia kubaki TANU.

TANU na ASP ziliunganisha nchi ya Tanganyika na Zanzibar lakini ilishindikana kuunganisha vyama vyao mpaka miaka 13 baadae walipoiunganisha ASP na TANU na kuzaliwa chama cha Mapinduzi-CCM. CCM ilirithi tabia ya TANU na ASP ya kutokutaka mawazo tofauti na wao. Na hapo ndipo walipoanzisha falsafa ya chama kushika hatamu.

Chama kushika hatamu ulikuwa ni mfumo kwa wananchi kutii bila ya kuuliza chochote dhidi ya mambo yote yanayotendwa na kuamuliwa na viongozi. Hali hiyo ndiyo imedumaza uwezo wetu watanzania kwenye kutumia akili zetu kujenga hoja.

Mtanzania anaweza kuwa na maneno meeengi lakini inakuwa taabu kwa msikilizaji au msomaji kujua msemaji anataka kusema nini. Kwa kweli watanzania wengi wamedumazwa uwezo wao wa kutumia akili zao kwenye kufikiri na kujenga hoja.

Kujenga hoja kunahitaji mantiki na mantiki haiwezi kujengwa na watu wasiotumia mbongo zao kufikiri kwa uhuru. Leo hii wanaofikiri kwa uhuru wameanza kuchukiwa kama ni maadui kwa kuwa eti ni kwa nini wao wanafikiri tofauti na viongozi, Ndipo ule msemo wa " Wewe unajua zaidi kuliko kiongozi" unapoibuka.

Tupo sehemu mbaya sana kama taifa. Hatuwezi kupiga hatua nzuri ya kimaendeleo kama hatutoruhusu mbongo zetu kufanya kazi kwa uhuru na kwa tafakuri jadidi. Matokeo yake mtu ana shahada tatu anafukuzwa ukuu wa Mkoa anaanza kutubu kama mwendawazimu mbele ya Kamera. Au ni sawa na Professa ambaye kwa hofu anamwita Rais "Mheshimiwa Mungu".
 
Huwa nasema bila machafuko tusitegemee kupata mabadiliko ya kweli. Maana wajinga wamefanikiwa kukamata madaraka na hawakubali kuachia, wanafanya lolote kuhakikisha wanabakia madarakani. Na sasa wanaweka hadi chawa kuwapigia debe waziwazi.
 
Changamoto inayokabili ni kwamba hakuna binadamu anayekubali kuwa anaweza kuwa na uwezo mdogo wa kutafakari, kuchambua, na kutoa suluhu yenye manufaa. Hata ukimwambia mara kwa mara, atakuwa na utetezi wa kujilinganisha na wengine, hata kama hawako katika nafasi yake. Hii inatokana na ubinafsi, ukosefu wa usawa, na tamaa ya kumiliki kila kitu, na kujipa haki ya kipekee ndani ya moyo wa binadamu.
 
Huwa nasema bila machafuko tusitegemee kupata mabadiliko ya kweli. Maana wajinga wamefanikiwa kukamata madaraka na hawakubali kuachia, wanafanya lolote kuhakikisha wanabakia madarakani. Na sasa wanaweka hadi chawa kuwapigia debe waziwazi.

Katiba mpya vipi haina msaada?..
Nashukuru mmeanza kuelewa sasa, siasa na wanasiasa hawawezi kuleta mabadiriko katika nchi hii.

Suluhu iko kwenye mikono ya raia wenyewe kuamua kufanya kitu.
 
Katiba mpya vipi haina msaada?..
Nashukuru mmeanza kuelewa sasa, siasa na wanasiasa hawawezi kuleta mabadiriko katika nchi hii.

Suluhu iko kwenye mikono ya raia wenyewe kuamua kufanya kitu.
Na kwenye hoja hii ya Katiba mpya naona ni kama tumekwama mahali. Ni kama kila wakati tunaulizana tutapikaje ugali wakati hatuna unga na wengine wanasema tatizo siyo unga bali hatuna kuni. Maana Kwani Katiba ni nini. Katiba isiyoanzia kwenye mbongo za wananchi ni uzushi na sawa na shrehe ya fashi fashi wakati wa sikukuu.

Kuna wakati hatutaki kutumia mbongo zetu kutunzia kumbukumbu za maana. Kulikuwa na mchakato wa Warioba ambao tulifikia mpaka kuwa na Bunge la Katiba. Alipokuja Magufuli mchakato mzima ukasimama. Lakini Samia naye alipoingia kikaundwa kikosi kazi cha kushauri mchakato uendaje.

Maajabu eti na waliokuwa kwenye tume ya Warioba nao waliitwa na hicho kikosi kazi kutoa maoni yao. Ina maana muda na rasirimali za taifa walizotumia wakati wa tume ya Warioba walikuwa wanazifuja bure? Utaona kama wangekuwa wanafikiri kwa makini jibu lao lingekuwa rahisi tu. Wangesema walitimiza wajibu wao na zamu ya wanasiasa wanaoongoza serikali kutimiza wajibu wao imefika.

Wengine wanasema hata tuwe na katiba nzuri kiasi gani nayo itavunjwa. Sasa si tutunge katiba na kuweka vipengere kwa atakayevunja ashughulikiwe? Yaani hatutafuti Katiba mpya kwa kisingizio kwamba hata hiyo haitaheshimiwa. Ina maana sisi tunawaheshimu sana wanaovunja Katiba kuliko tunavyotaka Katiba iheshimiwe??
 
Ha

Hayo matakataka yote kwisha kazi. Aggrey Mwanri, Kabudi, Kangi Lugora na Sheikh Alhad walijidhalilisha sana kwa kumfananisha Magufuli na mungu
Watanzania ni kama seti tupu zinazosubiri kujazwa kitu chochote kile!! Babu wa Loliondo ni mfano mmojawapo wa watu waliotokea na kufanikwa kujaza utupu kwenye mbongo za watanzania!!
 
Siyo ccm tu hadi hivyo vyama vingine havina msaada wowote kwa ustawi wa taifa hili zaidi ya kuwa wa Binafsi na wachumia tumbo, wanaungana na hao CCM kwa manufaa yao.
 
Siyo ccm tu hadi hivyo vyama vingine havina msaada wowote kwa ustawi wa taifa hili zaidi ya kuwa wa Binafsi na wachumia tumbo, wanaungana na hao CCM kwa manufaa yao.
Hii hoja ni mfano tu wa jinsi CCM ilivyodumaza akili zetu. Yaani hapa tunazungumzia CCM wewe unaleta vyama vingine. Unadhani kama tunatafuta suluhisho la udumavu tuliosababishiwa na CCM, hoja yako hii ingesaidia??
 
Hii hoja ni mfano tu wa jinsi CCM ilivyodumaza akili zetu. Yaani hapa tunazungumzia CCM wewe unaleta vyama vingine. Unadhani kama tunatafuta suluhisho la udumavu tuliosababishiwa na CCM, hoja yako hii ingesaidia??
Wote ni wale wale ni wa shirika wa CCM

Wangeamua kutonunuliwa na ccm, angalau ccm wangebadilika.

Unavyoona mbadala wa CCM tukimbilie wapi CUF ya Lipumba, ACT ya Zitto au CDM ya Mbowe?
 
Miaka yote CCM inasubiri vyama vingine ili ibadilike!!?? Kwa ivo yenyewe haina programu ya kujibadilisha na kuwa bora zaidi na hivi ilivyo??
Niambie chama mbadala baada ya CCM kuwa nje?

Jibu swali sio una QUOTE nusu nusu

Siku zote kwenye kutafuta majawabu lazima tuwe suluhisho, je chama kipi kitakuwa suluhisho? CUF ya Lipumba, ACT ya Zitto au CDM ya Mbowe?
 
Back
Top Bottom